Yusuf Manji amshitaki Reginald Mengi, adai fidia Sh1/-

Hawawezi kumpeleka Slaa mahakamani au kumdai fidia ,ndugu napenda uelewe kuwa kinachotokea hapa ni mapambano ya kambi ndani ya CCM na si kingine chochote kile ,na wala si kwamba wanaupigania ufisadi ,hio ni tiketi tu ya kugandamizana ndani ya chama chao ,au kwa zaidi ni amjungu ya wao kwa wao ,hivi unataka kutuambia Mengi alikuwa hawafahamu hao mafisadi tokea walipokuwa hawajatajwa na walipotajwa na akina Slaa ? Na kwa nini alikuwa Bubu mida yote hiyo mpaka juzi na jana jambo ambalo limeshapigiwa makelele zaidi ya mwaka sasa na kesi za rangi za kinyonga na miondoko yakobe zipo mahakamni.

Kitu kimoja ambacho inabidi mukielewe ikiwa mpo WaTz mnaofuatilia siasa za Tanzania ,Hamasi ni chama kilichoasisiwa na Wayahudi(Kama mnaifuatilia) ili kujipenyeza ndani ya kambi za wapelestina kwa kasi na kujua mambo ya ndani ya Wapalestina lakini baada ya kupenyeshwa kikageuka na kugeuza kibao ingawa bado kuna majasusi wanatumika wakiwemo ndani ya Hamasi lakini sehemu kubwa imebadilika na kuwa na itikadi za Kipalestina na hivyo kuwapa tabu wayahudi.

Sasa Hapa petu moja ya ujasusi uliopenyezwa ni hiki CHADEMA ,hiki kinasemekana ni pandikizi la CCM katika vyama vya Upinzani ,hapo awali yake lakini katika kutamukiwa kumetokea mapinduzi na kuibadili nia iliyokusudiwa na Chama Tawala kusoma harakati za vyama vya upinzani lakini ndani yake humo Chadema kuna waliowatiifu na kwa za CCM kwa maana wamebaki na nia ile ile japo huwezi kuwaelewa kwa kuwa dili limebadilika inabidi wajifiche na kuonekaana ni CHadema damdamu .

Sasa kumetokea mpasuko ndani ya CCM (Kambi za ndani ya CCM) ,hapa wale majasusi inabidi waonyeshe ni upande gani walioko ambao kusaidia kwao kambi hiyo ndiko kunakojitokeza hivi sasa ,hivyo angalieni sana mtaona kuwa maficho na rangi ya CHADEMA huwa inajitokeza tokeza na kufifia kwa maana WACHADEMA wamechanganyikiwa hawajui wapi pa kushika ila inaonekana kuwa CHADEMA wapo upande wa mafisadi kila awapo Kikwete na Chadema unaikuta kuwepo huko ,Zitto alikubali mitambo inunuliwe ,hapa palitokea kutofahamiana na Slaa ,Mengi nae anawapinga mafisadi na kumuunga mkono Kikwete Slaa anaonekana kumuunga mkono Mengi ,hivyo utaona migongano hii inatokana na kuwepo majasusi ndani ya Chadema ambao wanatoa sapoti kwa kiasi fulani pale mambo yanapoonekna yanataka kuingia doa ,tutaona makubwa tu maana ,kuna watu wamekaa pembeni wanaangalia miondoko ya Chadema na kumsifia pamoja na kumkingia kifua Mengi CCM nambari one.

Acha spinning & trying to confuse some people man with your Party-politics conspiracy theories.

Inahitaji courage fulani kukusanya vyombo mbalimbali vya habari (havikuwa vya IPPMedia kama walivyodanganya wakuu fulani) na kumtaja mtu kama RA, kwani influence yake inafahamika. Ni kama King-maker vile.

Watu wamekuwa wakimtaja kwenye mazungumzo. Mengi amekuwa wa kwanza kupata courage ya kumtaja hadharani. Ingawa unajaribu kudai angesema mapema zaidi, nani mwingine ametamka kabla ya Mzee Mengi?

Much respect Mengi. Tunasubiri kesi ya Manji ili uanike uozo wote!
 
Mzee Mwanakijiji,

Na wewe kwa upotoshaji kweli umekubuhu,

Well.. tuangalie upotoshaji wangu hapa kwani maneno yangu yote yapo hapa hapa. Kati ya mimi na wewe tutaona nani anayejaribu kupotosha watu licha ya ukweli kuwa mbele yetu.


ukija pewa nafasi sitashangaa nikiona unakuwa worse kuliko hata hao akina Rweyemamu.

Tofauti kati ya mimi na wewe ni kuwa sitaki nafasi yoyote ile. Sitoshangaa wewe ukijija kupata nafasi unaweza kuwa worse kuliko wale tunaoshindana na leo ambao hawako tayari kuukiri ukweli hata kama unawakodolea macho.

Katika mjadala wote huu sijaona mahali popote palipokufanya uje na conclusion kama hiyo unless kama lengo ni ku SPIN.

Hilo ndilo tatizo lako; kwa sababu hujaona basi unafikiri hakuna! Itakuwa furaha yangu kukumbusha tulikoanzia.

Mimi nilisema hivi kwenye ukurasa wa sita (6) wa thread hii (nimeweka msisitio wa point of contention):

Manji ameenda mahakamani amefanya jambo jema.. kwa sababu huko atatueleza kwanini yeye arudishe fedha za Kagoda ambazo zilichotwa kwa wizi? Mahakama itabidi iite ushahidi wa Kagoda.... na kutaka Mwanyika na wenzie wawe mashahidi upande wa Mengi..

Hili wala siyo gumu.. Hili siyo suala la Manji kama wengi wanavyofikiria ni katika kutaka kuifunua Kagoda....

that is whats up.. didn't I say time is up? It is.. Namshauri na Rostam afanye hivyo hivyo.. pleaaasse!!!

Hoja yangu hapo juu ilikuwa na msingi kuwa:

a. Mengi kwa vile amefikishwa mahakamani atatakiwa ajitetea. Katika kujitetea kwake atasema Manji anahusika na x,y. Mahakama itauliza unaushahidi gani? Mengi atasema ushahidi uko kwa b and c ambao walifanya uchunguzi na Manji alifanya m n katika uchunguzi huo na hivyo kumhusisha na wizi wa Kagoda! (Kampuni ya Kagoda haitaji familia ya Manji au jina la Manji).

b. Kwamba Mahakama ina nguvu ya kisheria ya kuita huo ushahidi au mashahidi wa upande wowote ule.

HIYO: ndiyo ilikuwa hoja. Hapo sijazungumzia uzito wa ushahidi au kwa namna yoyote kuhojia utaratibu wa kuendesha mashtaka. Nimezungumzia a specific legal issue. Kitu ambacho Dillunga alikielewa.

Alikielewa na ndiyo sababu kwenye ukurasa huo huo alikuja na kunijibu hivyo na akijibu the exact point of contention:

Kesi ya Mengi na Manji, mahakama haiwezi kuita shahidi aje kumsaidia Mengi ua Manji.

Manji akishatoa vielelezo vya vipengele vya madai (elements of the course of action) kwamba Mengi kanichafua, mzigo unahamia kwa Mengi, sio kwa mahakama, kwa Mengi, kuthibitisha uchafu wa Manji au kuthibitisha kwamba hakusema Manji fisadi papa.

Au unasemaje, ewe mkufunzi wa sheria wa jamvi, Mkuu Mwanakijiji?

Jibu la Dilunga linasema kuwa:

a. Mahakama haina uwezo wa kuita shahidi (ndiyo maana ya neno "haiwezi").

b. Mashahidi hao hawawezi kuitwa na mahakama kwa upande wowote kuusaidia upande huo.

Hapo ndipo mgogoro wote ulipo. Kitu ambacho bila ya shaka hukielewi kwa sababu kama ulivyosema hapa chini kuwa:

Kama nilivyosema mimi sio mwanasheria

Sasa licha ya kukiri kuwa wewe si mwanasheria unadai kujua kile ambacho sheria inasema kwa uhakika!

Inashangaza unajenga hoja nyepesi kama hii:
ila nimeona cases nyingi tu ambazo mashahidi wanaotakiwa na upande mmoja au mwingine hawafiki mahakamani na case inaendelea.

Kuona mashahidi hawafiki na kesi inaendelea mbona siyo jambo la kuishangaza dunia! si shahidi wa kesi ya Zombe kafa na kesi inaendelea? Kuna mashahidi ambao wanajitolea kuwa mashahidi lakini kuna mashahidi wanaoweza kuitwa na mahakama (summons) na watatakiwa kufika na wakigoma wanaweza kushtakiwa kwa kudharau mahakama (contempt of court). Kwa vile mashahidi wengi yawezekana uliowaona ni wale ambao kwa hiari yao wamejitolea kuwa mashahidi haina mahakama kama kuna shahidi mbishi (hostile witness) ambaye ni muhimu kwa kesi halafu akaitwa na mahakama na kesi ikaendelea!

Mfano juzi tu hapa case ya Prof. Mahalu ambayo mashahidi mbalimbali wa serikali wameshindwa kwenda mahakani na hakimu akaamua case iendelee.

Ndiyo; siyo la kushangaza..

Angalia pia Milosovic naye alitaka mashahidi kibao lakini akaambiwa wao sio relevant kwenye cases husika.

of course.. mashahidi lazima wawe relevant! Itakuwa ni upuuzi kumlazimisha mtu ambaye hana relevance kwenye kesi aje kutoa ushahidi!

Mimi nakumbuka hata wakati wa case ile ya wale waliotaka kumpindua Nyerere, mashahidi wengi ambao waliomba waje mahakamani, hawakwenda.

Shahidi anayeomba hana ulazima wa kwenda mahakamani!

Sasa nitashangaa kweli kwenye case ya madai kama utaweza kumuita mtu yeyote unayemtaka bila kuonyesha sababu za msingi za kuwepo kwake.

Ndio maana naweza kuona upotoshaji wako hapa; ni wapi nimesema umuite mtu bila "sababu ya msingi za kuwepo kwake"?


Dillunga alisema madai haya ambayo yaliendelea mjadala wetu juu ya nguvu za mahakama za kuita mashahidi wanaohusiana na hiyo kesi kwa upande wowote.
Nimeeleza hivi, narudia:

Unakosea na kupotosha kutamka kwamba mahakama itajiingiza kuita mashahidi kuthibitisha madai ya Mengi. Ya yeyote, si ya Manji, si ya Mengi.

Manji akishatoa vielelezo vya vipengele vya madai (elements of the course of action) kwamba Mengi kanichafua, mzigo unahamia kwa Mengi, sio kwa mahakama, kwa Mengi, kuthibitisha uchafu wa Manji au kuthibitisha kwamba hakusema Manji fisadi papa.

Kesi ya Mengi na Manji mahakama haijiingizi kusaidia kuleta ushahidi wa Kagoda, wa Mwanyika, wa DPP, kusaidia kesi ya Mengi au Manji. Sasa Mkufunzi wa sheria wa jamvi, nifafanulie zaidi, wapi nakosea.

Hapa anarudia kile kile ambacho wewe unakiunga mkono; kuwa mahakama haijiingizi kwenye suala la kuleta mashahidi kuusaidia upande wowote ule unaoshindana. Akaniomba nimuoneshe ni wapi anakosea.

Jibu langu la ombi lake la kiungwana lilikuwa hili (kwenye Ukurasa wa 7 wa thread hii)

unakosea pale unaposema mahakama haijiingizi kama haijiingizi kwanini kwenda mahakamani? The whole purpose ya kwenda mahakamani ni kuihusisha mahakama. Lakini kosa lako linazidi kuonekana unaposema kuwa "mahakama haijiingizi kuleta ushahidi".. umewahi kusikia kitu kinachoitwa subpoena au warrant?

Hapa tukaingia kwenye suala la ushahidi; nikaendelea kwenye jibu langu pale-
Mengi atasema, "Mheshimiwa Jaji ushahidi upo na sehemu ya ushahidi huo unapatikana katika utendaji kazi wa tume ya Mwanyika ambapo Manji alirudisha fedha ambazo azieleze ametoa wapi na amerudisha kama nani, ndiyo maana nimemuita fisadi."

Akisema hivyo, Mahakama itasema nini "kawalete kina Mwanyika"? au Mahakama ina uwezo wa kucompel witness kutokea mahakamani? Sasa Mengi akisema Mahakama imuagize Mwanyika, DPP, Polisi n.k kuja mahakamani mahakama itakataa kwa sababu "haijingizi kuleta ushahidi"?

Utaona ninarudisha hoja kwenye point ya contention (hoja tunayobishania) ambayo inahusu nguvu au uwezo wa mahakama kucompel witness kuja mahakamani. Suala tulilolizungumzia toka awali hapa ni juu ya UWEZO WA MAHAKAMA KUITA MASHAHIDI AU USHAHIDI KWA UPANDE WOWOTE ULE NA KUWA MENGI ANAWEZA KUTUMIA HAKI HIYO KUWAITA MASHAHIDI ANAOWATAKA NA MAHAKAMA IKAWAITA UNDER THREAT OF PUNISHMENT.


Kwa mfano ili uweze kusema Manji ndiye alirudisha pesa za Kagoda lazima uwe na ushahidi kuonyesha hivyo, ushahidi ambao umepatikana kwa njia halali. Hapo ni bank iliyopokea au wale waliokuwa wanapokea hizo pesa, vinginevyo mahakama itakataa kumwita shahidi huyo.

Ndiyo; Rais aliunda tume ya kuchunguza wizi wa EPA. Tukaambiwa kuwa watu fulani wamerudisha fedha walizoiba. Kwa upande wa Kagoda fedha zilirudishwa na mtu fulani. Mtu huyo anajulikana kuwa ni Manji. Manji karudisha fedha za wizi anayejua juu ya kurudishwa huko ni Mwanyika na watumishi wengine wa hiyo timu.

Ili kufikia kiwango cha kukubalika kisheria, Mahakama itamuita Mwanyika aje na ripoti ya wale wote waliorudisha fedha za wizi na kiasi cha walichorudisha. Akikataa, (kumbuka ni relevant witness) Mengi hana kesi, huwezi kumdai mtu wakati unamnyima nafasi ya kuleta mashahidi watakaoprove utetezi wake.

Huo ni mfano mmoja tu.

Mkorogo wa hoja ya awali ulitokea pale ambapo WoS alipoingiza element nyingine kabisa kwenye mjadala huu: Yeye alisema hivi:

Asante Mkuu kwa kufafanua nami niongezee kuwa Kesi hii siyo kama za jinai ambapo serikali ( republic) inatakiwa kuthibitisha pasina shaka, bali ushahidi ni on a balance of probability baina ya mdai na mdaiwa.


Kukusaidia ni kuwa element nyingine iliyoletwa hapa ni uzito wa ushahidi unaotumika kumkuta mtu na hatia katika kesi za madai. Hii haikuwa hoja yangu toka awali. Hoja yangu ilikuwa kwenye uwezo wa mahakama kuiita ushahidi au mashahidi. WoS alionesha kwa usahihi na wala sikubishana naye kwenye hilo kwani ni kweli kuwa kiwango cha uzito wa ushahidi kwenye kesi za madai (daawa) ni cha chini kulinganisha na kesi za jinai.

BUT THAT WAS NOT THE ISSUE. Hatukuwa tunazungumzia ni ushahidi gani unaweza kumsaidia Mengi au Manji..

Nilimuuliza WoS a point blank question: Je mdaiwa ana haki ya kuita mashahidi au kutaka ushahidi uletwe mahakamani?

JIbu lake ni hili:

Anayo haki na ni juu yake kuwaleta yeye mwenyewe.

Hapa ndipo nikagongana naye na nikaenda kwa kirefu kugusa sheria ya Mwenendo wa Mashtaka ya Madai (CPC 49/1966).

Nikaonesha Ibara ya 25 inaposema:
"25. Subject to such conditions and limitations as may be prescribed,
the court may, at any time, either of its own motion or of application
of any party
-
(a) make such orders as may be necessary or reasonable, in all
matters relating to the delivery and answering of interrogatories,
the admission of documents and facts, and the discovery, inspection,
production, impounding , and return of documents or other,
material objects producible as evidence;"

Nikaonesha kuwa mahakama ina uwezo hata bila kuombwa na upande wowote ule kuita ushahidi au kuagiza urudishwe. Na nikaonesha kuwa hata ibara ya 26 na 27 inayohusu mashahidi inawafunga mashahidi hao na ibara ya 25. Kwani ibara hiyo inasema:

26. The Provisions of sections 23 and 24 shall apply to summonses
witness to give evidence or to produce documents or other material objects.
27. The court may compel the attendance of any person to whom
a summons has been issued under section 25 and for that purpose may-
Penalty for
default
(a) issue a warrant for his arrest;
(b) attach and sell his property;
(c) impose a fine upon him not exceeding one thousand shillings;
(d) order him to furnish security for his appearance and in default
commit him as a civil prisoner.

Sasa hiyo ndiyo ilikuwa issue. Pamoja na hayo watu bado wakaendelea kudai (na bado wewe unaendelea kudai) kuwa mahakama haina uwezo wa kusema nilichosema. Na wengine nao wamekukubalia huu upotoshaji mkubwa wa sheria. NI kwa sababu ya kugundua kuwa ni ubishi usio na tija nikaamua kukubaliana nanyi kuwa nilikuwa nimekosea kwenye point of contention.

Je mahakama katika kesi za madai kwa kuangalia sheria za Tanzania ina uwezo wa kuita ushahidi au mashahidi. Kutokana na utaalamu wa nyinyi jibu ni kuwa hapana.. mashahidi wataenda kwa kujitolea tu na wakijisikia hawawezi kulazimishwa na mahakama kutokea. Nikawakubalia!!!!

Sasa kati ya mimi na wewe ni nani mpotoshaji mkuu wa hoja? Nitawaacha wengine waamue.
 
Sasa nitashangaa kweli kwenye case ya madai kama utaweza kumuita mtu yeyote unayemtaka bila kuonyesha sababu za msingi za kuwepo kwake.

Kwa hiyo kama utaonyesha sababu za msingi za kuwepo kwake unaweza kumwita - sasa hapa sioni tatizo liko wapi ama you are convinced mhusika hawezi kuwa na sababu za msingi.

Kwa mfano ili uweze kusema Manji ndiye alirudisha pesa za Kagoda lazima uwe na ushahidi kuonyesha hivyo, ushahidi ambao umepatikana kwa njia halali.

Kama anao ushahidi unaoonyesha Manji anahusika, ubishi uko wapi - ama mwenzetu tayari unayo habari kuwa hana ! Kwa taarifa yako mashahidi wapo, twasubiri tu kuitwa mahakamani.

Hapo ni bank iliyopokea au wale waliokuwa wanapokea hizo pesa, vinginevyo mahakama itakataa kumwita shahidi huyo.

Una maana pesa hazikurudishwa na kama zilirudishwa si kuna aliyezipokea - au tayari mnapanga kumkolimba - yale yale ya Mohamed Enterprises na mchele mbovu ? Kumbuka kuwa baada ya Safari ile kuumwa na nyoka, safari hii ..... twasubiri watangulie mahakamani.

Case ya mafisadi ingekuwa na maana kama Mengi na wengine tunaopinga mafisadi ndio tungeifungua case na sio vinginevyo.

Mengi tayari kafungua kesi kwenye mahakama ya wananchi na hivi sasa kesi inasikilizwa na mashahidi wanajitokeza. Hii ni baada ya vyombo vya dola kusalimu amri na kutamka hadharani kuwa vinawaogopa mafisadi. Hata humu ndani ya JF mashahidi wa pande zote wanajitokeza na kesi inaendelea, upo ?

Kwasasa kazi kubwa ya kuhakikisha madai ya ufisadi iko kwa Mengi na wala sio kwa hao mafisadi.

Hapa nimeshindwa kuelewa kinachoongelewa ni nini hasa - tafadhali fafanua.

Pia Mengi ni wrong person kupigana hii vita ya ufisadi kwasababu ni rahisi sana kuonyesha kwamba kwa njia moja ama nyingine kuna ugomvi na wahusika hasa Manji.

Ugomvi wake na Manji unakujaje hapa - huu ni ugomvi kati ya watanzania wanaoibiwa mali zao dhidi ya wezi. Mengi kaamua kuwa msitari wa mbele kwenye hii vita pamoja na wengine wengi tu kama Dr. Slaa - na wengine wengi tu tuko nyuma yao.

Huo ugomvi wao binafsi whether ni kwenye biashara au huko Yanga, sio tu unawagawa watu bali pia unashusha uzito wa case.

Siamini kuwa hili tamko linatoka kwa mzalendo mwenye uchungu na mali yake kuliwa na wenye meno.

Hawa mafisadi ilitakiwa wafikishwe mahakamani na watu ambao wako clean kwenye suala zima.

Wasafi ndio kina nani - wewe ! na kwa msingi huo kwa nini wewe usiwafikishe mahakani ama huoni ufisadi wao.

Ninakuwa na wasiwasi kweli na hawa watu wanaowashauri viongozi wetu au wafanyabiashara maarufu.

Hakuna hatari kama ya mtu ambaye hudhani anajua na wengine wote hawajui huku yawezekana yeye ndiye hajui. Hapa tukubali kuna pande mbili - ule unaokubaliana na alichofanya Mengi na usiokubaliana na hatua yake hiyo. Kama Mengi katenda kosa achukuliwe hatua na wahusika, aburuzwe mahakamani - hili wengine twalisubiri kwa hamu.

Huenda kwasababu hao viongozi wetu hawaambiliki au washauri wetu ni opportunists na wanaangalia boss anataka nini kisha kwenda na wazo kama hilo.

Yale yale, lakini viongozi gani unawaongelea hasa hapa ? Vipi na wale washauri wa mafisadi nao - wana tofauti gani na sisi, mimi na wewe.

Mshauri ambaye ni huru angeweza kabisa kumwambia Mengi timing sio nzuri.

Mshauri wa mafisadi bila shaka ataona hii timing sio nzuri maanake makombora yarushwa kutoka kila upande na kibano hakilegezwi, hakuna kulala mpaka kieleweke.

Vinginevyo hata mimi nasubiri hiyo case.

Sisi wengine tayari tunaendesha kesi na hivi sasa tuko mbioni kukusanya ushahidi zaidi.

Tatizo tu Mengi akishindwa tayari atakuwa ameua case nzima na hawa mafisadi na itakuwa ngumu sana kwa mtu mwingine kuwavaa.

Mengi spoke on behalf of millions of Tanzanians even if you are not amongst them. Tusubiri hiyo kesi itakayotua mahakamani kama itaweza kutengua ushindi wa wananchi dhidi ya hawa wezi na wauaji.
 
Mag3,
Usipotoshe nilichoandika, anayeamua kama shahidi au ushahidi ni relevant kwenye case husika sio mshitakiwa au mshitaki, ni mahakama. Kwahiyo hata kama wewe utaona huyo mtu ni muhimu, mahakama ndio itaamua kama ni muhimu.

Wakiona kuna umuhimu basi ndio shahidi anaitwa. Kwa case hii sitegemei kuona wahusika wakubwa kwenye ufisadi wakienda mahakamani kutoa ushahidi, unless Mengi awe na ushahidi mkubwa na ambao umepatikana kihalali.

Any way hii case haiko mbali na tutajua ukweli muda sio mrefu. Tatizo shauri ya ushabiki watanzania watajengwa matumaini ya ajabu na kisha kuja kuwa dissapointed.
 
Mwanakijiji na Mtanzania, tafadhali sana kaka naomba muache kufananishana mambo mnayofanya hapa kwa kuandika na yale ambayo mngefanya kwenye really life zenu. Nakusihi mbishane au kujadiliana bila kufananishana. Akhsanteni.

SteveD.
 
Mwanakijiji na Mtanzania, tafadhali sana kaka naomba muache kufananishana mambo mnayofanya hapa kwa kuandika na yale ambayo mngefanya kwenye really life zenu. Nakusihi mbishane au kujadiliana bila kufananishana. Akhsanteni.

SteveD.

yote ni maisha.. kufanana na na kufananishwa...
 
Mag3,
Usipotoshe nilichoandika, anayeamua kama shahidi au ushahidi ni relevant kwenye case husika sio mshitakiwa au mshitaki, ni mahakama. Kwahiyo hata kama wewe utaona huyo mtu ni muhimu, mahakama ndio itaamua kama ni muhimu.

Wakiona kuna umuhimu basi ndio shahidi anaitwa. Kwa case hii sitegemei kuona wahusika wakubwa kwenye ufisadi wakienda mahakamani kutoa ushahidi, unless Mengi awe na ushahidi mkubwa na ambao umepatikana kihalali.

Any way hii case haiko mbali na tutajua ukweli muda sio mrefu. Tatizo shauri ya ushabiki watanzania watajengwa matumaini ya ajabu na kisha kuja kuwa dissapointed.


this make no sense.. sasa ubishi wote ule ulikuwa wa nini? Mmoja kasema mahakama "haijiingizi" humu halafu mnairudisha mahakama tena.? Nimesema mahakama inaita uwezo wa kuita ushahidi au mashahidi mkabisha; kwamba ushahidi ni lazima uwe relevant nilisema kurasa kadhaa huko nyuma that is not even an issue here kwa sababu hata mtoto wa siku moja kwenye darasa la sheria anajua maana ya umuhimu wa ushahidi katika kesi husika.

Kwamba Mengi awe na ushahidi mkubwa uliopatikana kihalali.. pia siyo somo geni, kwa sababu ushahidi usio halali hauingii mahakamani. Ushahidi uliokusanywa na Timu ya mwanyika ni halali!
 
.. sasa ubishi wote ule ulikuwa wa nini? Mmoja kasema mahakama "haijiingizi" humu halafu mnairudisha mahakama tena.?

Wewe si mkweli. Hakuna aliyesema mahakama hajiingizi. Ilisemwa hivi: "Kesi ya Mengi na Manji mahakama haijiingizi kusaidia kuleta ushahidi kusaidia kesi ya Mengi au Manji..."

Kwa nini husemi ukweli Mwanakijiji?

Halafu si ulisema hutaki "ligi nyingine." Sasa umerudi?

Mzee Mwanakijiji said:
... maana ligi nyingine mimi siwezi kwa kweli.

Nimekubali sijui sheria kwa sababu nasoma kama novel!! Nimekubali kushindwa handedly
 
Wewe si mkweli. Hakuna aliyesema mahakama hajiingizi. Ilisemwa hivi: "Kesi ya Mengi na Manji mahakama haijiingizi kusaidia kuleta ushahidi kusaidia kesi ya Mengi au Manji..."

Kwa nini husemi ukweli Mwanakijiji?

Halafu si ulisema hutaki "ligi nyingine." Sasa umerudi?

kwa sababu kuwaachia muendelee kupotosha siwezi..! "haijiingizi kusaidia kuleta ushahidi kusaidia kesi ya Mengi au Manji" ndio imefafanua nini? Hujasema kitu tofauti ya nilichodai umesema..!
 
Then he should have produced it. If he hasn't he comits criminal libel underthe pena code of Tanzania. Whi is he anyway to behave like this, the President or just an aspiring one?
 
Then he should have produced it. If he hasn't he comits criminal libel underthe penal code of Tanzania. Who is he anyway to behave like this, the President or just an aspiring one?
 
Hamjamuelewa Manji
Du makubwa inamaana uharibifu aliofanyia pamoja na heshima yake kwenye jamii plus reputation ya makampuni anayoyaongoza gharama yake ni shilingi moja. Sikutegemea kama anaweza kuwa hana thamani kiasi hicho sasa naamini kuwa ufisadi unamshusha mtu thamani ya utu wake.
 
Back
Top Bottom