Wana jf
CCM chini ya Mzee wa pembe za ndovu imepanga mipango mikali sana jamaa wa ndani sana amenitonya kama ifuatavyo:
1. Wanasema kuwa lazima CHADEMA ife kabla ya zoezi la kuteu wagombea wa uraisi na ubunge kutoka vyama kwa uchaguzi 2015 halijafika wala kukaribia, kwa kuwa eti ikifikiwa wakati huo na CDM kikiwa na nguvu iliyonayo sasa hivi, eti
CCM itasambaratika yenyewe na ndio itakuwa mwisho wake.Hii wanasema ni kutokana na mgawanyiko uliopo sasa hivi,Kwa mtazamo huo jamaa kaniambia wamekuja na plan A na B. Plan A ni kuwabambika kesi viongozi wote wa CHADEMA ili wawe wanahangaika na kesi na fedha zote ziishie kwenye kesi wakose muda wa kufanya mikutano ya kushawishi wananchi,kuongea na wamiliki wa vyombo vya habari kupunguza kabisa kuandika habari ya CDM na kuanzisha vipindi kwenye redio wakati wa asubuhi na jioni vyenye lengo ya kuzunguzia amani kwa lengo la mlango wa nyuma wa kuiponda CHADEMA. Kuwatumia baadhi ya viongozi wa upinzani kuiponda chadema hasa class mate wangu pale UDSM Mbatia. Jamaa akaniambia kama plan A itashindikana plan B watadili na Dr Slaa moja kwa moja watadili naye vipi hakunitonya. Tafakari chukua hatua.