Mangula na Kinana mmejidhalilisha

Mangula na Kinana mmejidhalilisha

ki ukweli chama tawala kimepoteza mwelekeo kimebaki na siasa za majitaka kwa sasa hakuna alienauwezo wa kukinadi akaeleweka wote ni uchafu mtupu, ndio maana wakawaona mtela na shonza kama dhahabu kwao wasijue kuwa wanatumia moto wa mabua ukizimika unazimika kweli
 
Jamani vijana na wazee wa CDM humu JF, tafadhalini sana msimuamshe aliyelala waachen waendelee kutumia majembe yao ili CDM ipate upenyo kirahisi. Tena ikiwezekana wasifieni sana na hasa hiki kidada sijui ndo kinaitwa Fyonza na huyu jamaa anaetaka kulewa Mwampamba aka Mwisho wa matusi.
 
FUSO; Hakika kina Mangula na Kinana wamewaangusha wana CCM kwani walitegemea mikakati bora ya kukinusuru chama badala yake mikakati yenyewe imekuwa kuwapandisha jukwaani wasanii kina Diamond na kuimba nyimbo za "Nataka kulewa" badala ya kueleza sera!
 
Last edited by a moderator:
Wana jf

CCM chini ya Mzee wa pembe za ndovu imepanga mipango mikali sana jamaa wa ndani sana amenitonya kama ifuatavyo:
1. Wanasema kuwa lazima CHADEMA ife kabla ya zoezi la kuteu wagombea wa uraisi na ubunge kutoka vyama kwa uchaguzi 2015 halijafika wala kukaribia, kwa kuwa eti ikifikiwa wakati huo na CDM kikiwa na nguvu iliyonayo sasa hivi, eti
CCM itasambaratika yenyewe na ndio itakuwa mwisho wake.Hii wanasema ni kutokana na mgawanyiko uliopo sasa hivi,Kwa mtazamo huo jamaa kaniambia wamekuja na plan A na B. Plan A ni kuwabambika kesi viongozi wote wa CHADEMA ili wawe wanahangaika na kesi na fedha zote ziishie kwenye kesi wakose muda wa kufanya mikutano ya kushawishi wananchi,kuongea na wamiliki wa vyombo vya habari kupunguza kabisa kuandika habari ya CDM na kuanzisha vipindi kwenye redio wakati wa asubuhi na jioni vyenye lengo ya kuzunguzia amani kwa lengo la mlango wa nyuma wa kuiponda CHADEMA. Kuwatumia baadhi ya viongozi wa upinzani kuiponda chadema hasa class mate wangu pale UDSM Mbatia. Jamaa akaniambia kama plan A itashindikana plan B watadili na Dr Slaa moja kwa moja watadili naye vipi hakunitonya. Tafakari chukua hatua.

....uonevu unapozidi huruma inajitokeza dhidi ya anayeonewa, hii ndo hulka ya mwanadamu.....na ndicho kilichotokea Kenya kwa Uhuru Kenyatta na Makamu wake kushinda uchaguzi ule.....huruma za Wakenya kwa viongozi hao dhidi ya uonevu wa ICC......CCM tafakari, then chukua hatua ila mwisho wa yote kubalini matokeo....

......hata GOLIATI hakuweza kumshinda DAUDI licha ya Maguvu yake....Sababu ni nguvu ya MUNGU iliyokuwa kwa DAUDI.....
 
ktk miaka 36 ya chama cha mapinduzi hakijapa bahati ya kuwa na nondo km hao, huo ndio ukweli whether you like o not CCM kinakimbiwa na wasomi wote makini na kiliobakiwa nao wote ni wababaishaji wasiojielewa ata kidogo period.

mkuu tutake radhi. Tumebakiwa na wasomi wapiga chabo wazee wa vibomu kina savimbi kuna yule dada ambaye hata anachoandika hakijui maana yake.
 
Mimi ni mwana CCM mfu, mleta mada ktk hili la hawa watu wawili kujiuzulu siafikiani na wewe hapa hawa wazee ni watu makini ktk chama na hawa ndiyo watatufikisha mahali tunataka, Kinana akiwa mahali akashirikiana na Mangula mambo yote yanakwenda sawa.
Vijana wetu hawana tatizo ni kukaza uzi tu hawa Chadema tunawaondoa hapo Arusha 2015 wana CCM wenzangu tusiwe na wasiwasi kama ni safu tumejipanga vizuri.
 
Kuhusu kwamba alishaurina na nani nadhani hao walipewa ili nao waonyeshe kwamba vijana wana nafasi katika chama kumbe vijana wenyewe ni wahovyo. Hawana uwezo wa kujenga hoja hasa huyu Mwigulu!!!

Sema mikakati ya kushinda kama serikali inahitaji uwe na mbinu kali zaidi maana watu wanapima hata utendaji wako wakati wapinzani wao ni kuongea tu.

Dr. Benson Bana ndiye mshauri mkuu wao, ataenda kushika hatamu yeye kukiokoa chama!
 
Tatizo wote walishajichokea wamelazimishwa kurudi uongozini. Kinana alishasema anastaafu ili aendelee na biashara zake. Mangula alishachoka akijilimia nyanya kijijini kwake. Kwakuwa hakuna mwenye maono ndani ya CCM wakaenda kuwachukuwa wastaafu hao. Mangula alianza na gia ya kuwaondoa wote waliopata uongozi ndani ya CCM kwa njia za rushwa. Alijigamba kuwa atafanya hayo ndani ya miezi 6. Badala ya kushughulikia ahadi yake, akaenda kwanza kuoa. Miezi 6 imepita akiwa HONEY MOON. Juzi anastuka hajamtoa hata mmoja! Amejiongezea tena miezi 6. Wakati huo huo watuhumiwa wanaendelea kuchanja mbuga wengine wakijiandaa kwa urais. Hakuna lolote analoweza kufanya. Atawaondoaje waliomuweka hapo. Tena kumkomoa wakampa kura asilimia 100. Ashukuru wamemtoa kwenye kilimo cha nyanya aje mjini kufaidi keki ya ufisadi ili amalizie maisha yake kwa raha.
 
Wajilaumu kwa kuajiri Consultant mbovu aliyewashauri kumuachia a free hand the devil re-incarnate Mwigulu Nchemba (may he burn in hell!!) kuwa chief strategist wa CCM na kuendesha shughuli zote za CCM atakavyo na wao wakaamua kuchukua back seat!

Mbinu za Nchemba za matusi, vitisho na mabomu ya moto, kujifanya IGP wa kuiamuru polisi kusigina utashi wa umma ndio zinakiua chama chao
Hawa wazee wakae na JK (chaguo la Mungu) ili waandae mikakati mbadala! The sooner they realise that Nchemba is the devil within the better for them or else the longer they wait and procrastinate wataja kuta mwali si wao! CDM is growing in strength; strategically and popularity by the day.
 
Yani Mangula wa watu alikua anajilimia viazi mviringo huko Iringa aliemshawishi arudie matapishi sijui nani? kwanza walimtupa, wakamgalagaza, wakamsahau, now wanajifanya kulipa fadhira.....ndo kwanza ccm wanamtumbukiza shimoni, kuhusu Kinana kwani nani asiejua kua siasa zake zimezeeka na hili ndo mtaji wetu mkubwa CHADEMA kuendelea kushinda.
MY TAKE; Mwigulu na Kinana wabaki kupigia debe ccm ili CHADEMA wazidi kupeta.
 
Kinana na Mangula

aibu hii ni kubwa sana maana ulikua ni mpira wa miguu mmefungwa mabao 136 kwa sifuri. Yaani mmefungwa mechi zote (vituo vyote) hamkuweza kuzuia au walau kupata ushindi kwenye kituo kimoja.

kama ingekua ngumi za kulipwa ni technical knockout kwenye mechi zote.


je hamna wanachama walau hata 500 kwenye kituo kimoja Arusha? Je ule mtaji wa wanachama takriban 10millioni kumi mnajita,ba nao uko wapi?

kinana na Mangula uongozi wote wa mkoa ulishindwa kuwashawishi wanachama wenu walau mshinde kituo kimoja tu, hii tafsiri yake watendaji katika ngazi ya mkoa na wilaya hawtaki kuwapa ushirikiano. Hivyo kwa nini msiwaachie chama chao mkalinda heshima yenu?

Mangula na Kinana, mmeona baadhi ya viongozi waandamizi hasa Mgulu akitaamka wazi wazi mgombea urais wa CCM uchaguzi ujao ni lowasa ilihali chama bado hakijampitisha wala mchakato huo haujaanza. Na kama chama mlikataza wenye nia hiyo wasianze kujipitisha kabla ya muda na bado mmeshindwa kumwajibisha je hamuoni huo ni udhaifu mkubwa sana katika utendaji wenu kwa kutoa tamko na kushindwa kulitekeleza kama katiba yenu inavyosema? Je kwa nini msijiuzulu mkatunza heshima yenu
 
Mimi ni mwana CCM mfu, mleta mada ktk hili la hawa watu wawili kujiuzulu siafikiani na wewe hapa hawa wazee ni watu makini ktk chama na hawa ndiyo watatufikisha mahali tunataka, Kinana akiwa mahali akashirikiana na Mangula mambo yote yanakwenda sawa.
Vijana wetu hawana tatizo ni kukaza uzi tu hawa Chadema tunawaondoa hapo Arusha 2015 wana CCM wenzangu tusiwe na wasiwasi kama ni safu tumejipanga vizuri.



hahahahaha umeona Juliana alichosema ... CCM arusha ni sawa na Mchicha by 2015 mtakuwa sawa na Mbuyu. na wewe unashabikia humiliation mliyopata Arusha na kusema bado mnawahitaji Kinana na Mangula.

Je wakijiuzulu nini kitatokea? Nipe mtazamo wako
 
wapo wapi tena hawa watu au ndio wanaompa mwigulu hii mikakakati..?
 
teh teh...mwnglu anawapeleka puta...wanasita kufanya siasa maji taka....hapa ndipo aliposema kolimba kuwa chama kimekosa mwelekeo.
 
ha ha ha haaa....eti mtaji wa magamba million 10? na bado bukoba acha wajichetue tu safari hii ni bao 8:0
 
Back
Top Bottom