Mangula na Kinana mmejidhalilisha

Mangula na Kinana mmejidhalilisha



Lakini WanaCCM; Msitegemee CHADEMA ikianguka Mtakavyo atakyekuja atakuwa lelemama Dhaifu kama CCJ; Ndio hivyo Calculas za CCM - CUF ilipokuwa kali ya kukinyima USINGIZI na VITAMBI... ilitumia muundo wa karibu tule wote; Huko sio Kumeifanya ZNZ kimya sasa kumeleta MKALI zaidi ya CUF - UAMSHO; Sasa pia kuna wanaodiriki kuwafyatulia risasi viongozi wa DINI ambazo sio kuu huko...

Sasa, Kama watataka kukifuatilia CHADEMA ambacho kinaonekana kikubwa zaidi ya CUF kwa IDADI ya Umma unayokisupport; then, Sijui kama CCM pekee itakuwa na NGUVU hizo za kukifuta; Kwanza ukiangalia Mataifa ya Magharibi Mfano USA sasa inakitambua CHADEMA kama chama pinzani nchini... Katika historia ya VYAMA HURU vya KISIASA hadi huko PAKISTANI ambako mara nyingi JESHI huwa linapindua serikali ya Rais HURU; Hawajawahi hata siku moja kuvivunja Vyama vyao vya kisiasa...

KENYA... Kanu ilianguka kwa kushindwa kuendelea kuwa na Wafuasi; lakini bado GORDON MOI na UHURU KENYATTA wanaweka KANU kama affiliate party...

Kwahiyo; Hauwezi kuelewa CCM ni nani hadi sasa anaiweka HAI hadi leo; Sidhani ni Wananchi; Ni viongozi wanaotawala kwa NGUVU za kidicteta

Kwahiyo Kama Mmechoka na MADARAKA Jaribuni kutafuta nja nyingine za kuendelea kushika HATAMU za UONGOZI; kuliko kujaribu kuwaingilia WAPINZANI kudhani ndio hapo utakapojisitiri na kuendelea KUONGOZA

CHUNGA sana... Human kindness has never weakened the stamina or softened the fiber of a free people. A nation does not have to be cruel to be tough.


 
kipesa ndio wasaau kabisaaaa.kwani tayari kuna mikakati ya makamanda walio nje na ndani kuchangia kwa nguvu kuliko siku za nyuma.kama tulikuwa tunacngia 2 sasa itakuwa 4.Waweke kesi hata mia nane.pesa ipo .
 
Chama kinaongozwa na wanajeshi, what do you expect from them. wengine tushapitia huko. it is about muscles and not about intelligence. sasa ukichanganya na wale wa first class za uchumi na siasa za maji taka, Chama kimekuwa kama meli iliyokosa nahodha, kinaongozwa with no clear direction.

Main Objective ya chama sasa ni kupambana na Chadema huku wakisahau jukumu lao la msingi la kutekeleza ilani ya chama chao ili angalau kurudisha imani kwa wananchi.

Watakapo realize kwamba Chadema ni imara na haiwezi kufa kirahisi hivyo ndiyo wakati pia wata realize kwamba muda wa kutekeleza ilani ya chama chao hautoshi.

Wanayaogopa mabadiliko wakati nafsi zao zinakiri kwamba mabadiliko ni lazima na ni kitu cha kawaida na zaidi sana kwamba hayaepukiki.
 
Wawe makini maana waweza kuwa ndio mpango wa mwisho kuimalizia CCM. Wanaweza kuwa ndo wanakamilisha kaburi la mazishi yao wenyewe.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Hivi karibuni tumeona vijana wawili walioandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo, baadaye wakafukuzwa kwa utovu wa nidhamu, wakionekana kuwa mtaji MKUUUUUUUUUUUUUUUUUBWA kabisa wa kisiasa wa Chama cha Mapinduzi.

Vijana hawa, kwa sasa hivi kwenye majukwaa ya siasa ya CCM wamechukua hata nafasi za wazee, akina Mangula na Kinana.

Wengine wanaweza kusema mie mzushi au napiga propaganda. Jamani tuwe wakweli. Changamoto gani kubwa iliyokuwa ikiikabili CCM kuliko kujaribu kurudisha jiji la Arusa mikononi mwao kwa kushinda viti ya Udiwani? Hii ndio sehemu ambayo unatumia silaha zako bora kabisa. Tena Katibu Mkuu hapo ni nyumbani kabisa, na mcheza kwao hutuzwa, lakini hakuonekana kabisa. Mzee Mangula Makamu wa Mwenyekiti, huenda alikuwa na kazi nyingi ofisini mwake, tunamsamehe.

Bila shaka nguvu ya vijana ilihitajika. Chama hiki kikongwe kuliko vyote barani Afrika kimekuwa na utamaduni wa muda mrefu wa kutayarisha vijana. Wengine hata wanapata mafunzo ya kutumia silaha kwa ajili ya kukihami chama na kwa kidhungu wanawaita Greenguards. Wazee wa chama waliangalia huku na kule hawakupata watu wa kuwaamini. Hawakuamini malezi yao. Waliona maandalizi yao yana kasoro. HAKUNA MWANA UVCCM orijino aliyefuzu kupewa majukumu!

Wazee waliposhindwa kupata mavuno mazuri toka mashamba yao, wakaambiwa kuna bidhaa ready made. Unahitaji tu kulipa. Vijana walioandaliwa na chama kidogo kinachokera sana. Vijana ambao wana gubu la kufukuzwa kutoka uongozi wa umoja wa vijana wa chama hicho kwa utovu wa nidhamu.

Wazee wakawaona kuwa hao ndio wenyewe, kwa kuwa CCM sasa inahitaji kampeni zinazoweza kufanywa na watu wasio na adabu, wasio na haya, wasio na nidhamu. Kampeni za kusema watu. Kampeni za majitaka. Wakapewa boss ambaye ana sifa zote hizo.

Hawa ndio wakaenda Arusha, kujaribu kurudisha madiwani wa CCM kwenye manispaa ya Arusha. Wakaenda wakiahidi kutumia vipaji vyao vyote, kuhakikisha CCM inashinda. Walitoa kashfa nyingi kwa maisha binafsi ya Dr. Slaa, walitoa yale waliyoyaona ni mapungufu makubwa ya uongozi wa Dr. Slaa, walikosoa muundo wa uongozi wa chama n.k.

Bahati mbaya ajali zilianza kutokea katika kikosi hiki kilichoaminiwa na chama Tawala. Mtela Mwampamba alihukumiwa kifungo cha mwezi mmoja kutokana na kuwa MUONGO, na UONGO wake ukathibitishwa pasipo kiwingu cha mashaka. Wakati bado timu ya kampeni ya CCM ikiuguza majeraha ya majeruhi Mtela, ajali nyingine ikatokea. Mheshimiwa Mbunge, na Naibu Katibu Mkuu akajikuta ameshindwa kujizuia kuonesha kipaji chake kikubwa, ufundi wa KUTUKANA MATUSI ya NGUONI. Akadhihirisha kipaji chake hadharani na kwa bahati mbaya ikawa hapa JF. Naye akahukumiwa kifungo cha mwezi mmoja.

Mpiga kampeni aliyebaki akawa Juliana Shonza. Naye siku ya Jumapili akaianza kwa majigambo akituletea uzi CCM kuibuka kidedea uchaguzi Arusha.

Aliendelea kuwepo hadi vituo vilipotangaza matokeo. Mpaka sasa hajajitokeza tena.

Maswali yangu:

Je CCM mlijua ni uwanja wa siasa au wa mipasho? Mbona basi mllituletea watu waliokubuhu kwa mipasho badala ya sera? Mbona mlituletea waongo? Mbona mlituletea watukanaji? Mlitegemea kuvuna zabibu kwenye shamba la miiba?

Poleni sana.

NAWASHAURI MUENDELEE KUWATUMIA HAO MAKADA WENU KWENYE MAJUKWAA YA SIASA!!

.
992814_508888975850421_972006896_n.jpg


KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Sifahamu wenzangu wa ccem wanatumia vigezo gan kuchagua watu wa kusimamia kampeni, lakini uzoefu unaonyesha kwamba popote walipotumwa hao wanachadema wawili wakiongozwa na Mwigulu lazima ccem iangukie pua!
Sisi wengine hatupendi ccm ipotee kwenye ramani ya nchi, lakini kwa mwenendo wa kuwatumia hao vijana kuna hatari kubwa kwa chama hiki cha Nyerere!
Ni Ushauri tu, hutaki unaacha!
 
Njaa zinawasumbua vijana,walivyovalia hiyo miguo yao ya kijani hata hawapendezi,naamini mioyoni mwao wanaiwaza CDM na gwanda.ila acha wagange njaa,muda si mrefu watatupwa pembeni hizo mia mbili mia mbili wanazopata hawazipata tena kutoka CCM,hizo simu zao wanazopigiana na kina Mwigulu mwisho wa siku hawatapokeleana tena na ikibidi wataziweka kwenye rejected list.wakuu nawa-promise muda si mwingi yatawakuta haya,na ndipo watajuta hadharani.hiyo ni CCM bwana.yuko wapi Tambwe ?
 
Politics is not for the faint hearted. Kumeza matamshi magumu kama wanayotoa haea watoto ni ngumu sana. Poleni, vaeni ujasiri tu mvumilie manake sasa labda mhamie tlp!
 
Lakini CCM wajiulize kuwaweka mbele vijana hawa kunawakatisha tamaa sna vijana origino,hasa ikizingatiwa hawaitetei CCM
 
Huwezi kumdhalilisha mgonjwa kwa malazi yake ili wananchi akuchague, hiyo ni ngumu sana kwa atafakarie mambo.
Pia mfumo mbovu wa utawala ndo huleta kampeni chafu na zenye matusi ambazo magamba wanazo.
Shindaneni kwa hoja zenye maana ili wananchi wanufaike na nchi yao.
 
mwigulu akitoka ban atakana kwamba kuna mtu ali hack password yake akaweka matusi ili kumchafua, kama kule facebook
 
Hii ni Arusha, wasiofahamu siasa za hapa huwezi kuja na kuingia kichwa kichwa kama hao madogo, . Hapa kuanzia mwanafunzi, mama muuza mchicha mpaka daraja la kwanza ni wanasiasa. Ukija hapa na siasa zako tunakusikiliza na kupima then we decides.
 
Hii ni Arusha, wasiofahamu siasa za hapa huwezi kuja na kuingia kichwa kichwa kama hao madogo, . Hapa kuanzia mwanafunzi, mama muuza mchicha mpaka daraja la kwanza ni wanasiasa. Ukija hapa na siasa zako tunakusikiliza na kupima then we decides.

Arushaone mnaroho mbaya sana nyie watu,pamoja na kununua kadi za wapiga kura,kukamata vijana na kuwanyan'ganya vitambulisho vya kupigia kura,kupiga mabomu lakini bado mmetufanyia haya????kweli CDM haiwezi kufa hata kwa mtutu wa bunduki!!!!!
 
Hayo ni marudio tu baada ya kufeli,

Political strategic wa ccm ni msaliti, anawaingiza mjini kila kukicha!

Chadema songeni mbele, Red Brigade kazi mtindo mmoja, linda chadema na malizi zake!
mwanafunzi anayerudiarudia darasa au mitihani huwa si mwerevu bali anakariri.
 
Wana jf

CCM chini ya Mzee wa pembe za ndovu imepanga mipango mikali sana jamaa wa ndani sana amenitonya kama ifuatavyo:
1. Wanasema kuwa lazima CHADEMA ife kabla ya zoezi la kuteu wagombea wa uraisi na ubunge kutoka vyama kwa uchaguzi 2015 halijafika wala kukaribia, kwa kuwa eti ikifikiwa wakati huo na CDM kikiwa na nguvu iliyonayo sasa hivi, eti
CCM itasambaratika yenyewe na ndio itakuwa mwisho wake.Hii wanasema ni kutokana na mgawanyiko uliopo sasa hivi,Kwa mtazamo huo jamaa kaniambia wamekuja na plan A na B. Plan A ni kuwabambika kesi viongozi wote wa CHADEMA ili wawe wanahangaika na kesi na fedha zote ziishie kwenye kesi wakose muda wa kufanya mikutano ya kushawishi wananchi,kuongea na wamiliki wa vyombo vya habari kupunguza kabisa kuandika habari ya CDM na kuanzisha vipindi kwenye redio wakati wa asubuhi na jioni vyenye lengo ya kuzunguzia amani kwa lengo la mlango wa nyuma wa kuiponda CHADEMA. Kuwatumia baadhi ya viongozi wa upinzani kuiponda chadema hasa class mate wangu pale UDSM Mbatia. Jamaa akaniambia kama plan A itashindikana plan B watadili na Dr Slaa moja kwa moja watadili naye vipi hakunitonya. Tafakari chukua hatua.
msichangae ccm ikajiunga na TLP na NCCR, hawatasimamisha mgombea wa urais bali watam-support yule wa CCM kuipunguza makali CDM. this is plac C.
 
Back
Top Bottom