Mzee Mangula na Kinana,
Mlifanya siasa za mkakati mkashinda chaguzi nyingi na chama chenu kikawa imara na kujipatia sifa za kutosha.
CCM ilianza kupoteza mvuto mlionekana nyie ndio tegemeo kubwa na mna uzoefu wa kutosha kuokoa jahazi lisizame.
Mkaombwa kurudi kwenye usukani wa chama mkakubali mkajiwekea mikakati ya namna ya kuendesha chama. Mkaomba mpewe timu ya ushindi mmepewa.
Swali je timu yenu ya ushindi imeshinwa kazi? Mmepokonywa kata 5, mmepata kura chache kuliko upinzani pamoja na kushinda kata nyingi.
Hii tafsiri yake chama kinazidi kuporomoka na hata vitongoji na vijiji vilivyofanya uchaguzi vingi vimeangukia upinzani.
Je hamuoni huu ni muda muafaka wa kuachia ngazi kabla mambo hayajawa mabaya zaidi?
Mnaweza kusema bado mnaweza kubadilisha hii trend kwa kufanya mabadiliko kwa kupindi kilichobakia. Kama mmeshindwa walau kunyakua hata kata moja ya CHADEMA au hata kijiji leo hii ni kitu gani kinakupa nguvu kwamba utaweza mwaka mmoja ujao?
Kumbukeni kwamba nguvu zenu(physical strength) zinapungua kila kukicha sababu ya uzee na dunia inabadilika kwa kasi sana kutokana na technologia. Na kwa umri wenu technolijia inawaacha. Je huu si muda muafaka mkawapa watu wengine wapange timu ya ushindi kuanzia sasa?
Kama mnadhani bado kuna uwezekano wa ushindi hapo mbeleni, je timu ya Mwigulu, Nape et al, unadhani itawafikisheni kwenye malengo.
Kulinda heshima yenu jiuzuluni muwape vijana ama wazee wengine waoneshe umahiri wao nyie mmbakie kuwa washauri.
Usione aibu kujiuzulu sasa maana aibu inayofuata ni kubwa kuliko ungejiuzulu sasa.