happiness win
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 2,461
- 1,394
Mwanzo 3:14-16, matatizo hayaanzi machoni hapa au kwenye ubongo, yanaanza katika ulimwengu wa kiroho, mtu asipotambua hilo hawezi elewa na anaweza akaomba yote hayo na kwa imani akayapata kasoro ya adui yake anayemletea matatizo kugeuka kuwa rafiki
Ni kweli kabisa kila jambo sio matatizo tu linaanzia kwenye ulimwengu wa kiroho kabla ya kuzaliwa kwetu duniani. Huwa tunashiriki na kujua maisha yetu yatakuwaje duniani. Tatizo dhambi hufunika uwezo wa kutambua na kukumbuka maisha yetu yatakuwaje duniani. Hapo tulipaswa kuwa wa kiroho kwa kudumu katika maombi na yote yanayotusumbua yasingetokea maana tungeyajua kabla. Ndio maana nikasema sio kila kitu kinaombewa, kuna vingine unaviepuka tu, na ndio Maana unawezaomba na ukajiona kama hujibiwi bila kujua lile jambo lilitakiwa kuchukuwa hatua fulani na sio kukaa na kuliombea. Sana sana kama unaweza uingie huko kirohoni na kuangalia nini cha kufanya.
Hiyo mwanzao uliyoiquote... inaonyesha uadui wetu na shetani ulipoanzia na adhabu tuliyopata kwa kutotii kwa Hawa. Hapa tunazungumzia Kuondoka katika maisha ambayo si ya raha kwetu, haina maana kwa kuwa tulitenda dhambi basi tutaishi kwa kuumia duniani na kuwa watu wa kulia na kuomboleza bila sababu ... hilo Mungu alitupa neeema kwa damu wa mtoto wake. Ni somo refu sana unaweza usinielewe. Ila point yangu inabaki kwa Nacherewa kuondoka na kutafuta amani na furaha Maana Mungu wetu alituhakikishia kuishi kwa raha tukimtegemea yeye, jicho la kushoto likukosesha ling'oe. Najua bado ni ngumu kunielewa
Last edited by a moderator: