36, no kids, unafanya kazi, ila bado unasubiri akuletee mke mwenzio ndani ndio uondoke sio? au ngoma kabisa.
36 bado marketable bana, ama?
Ingekuwa tukio la mara moja, ningekushauri ushirikishe wazazi ila kwa jinsi ulivyoelezea na kama ni kweli, hama hapo haraka utafute ustaarabu wako.
Omba kabisa talaka muachane, huyo hakupendi na hakutaki kabisa na sijui kwanini hakupi talaka? Au anakutegemea? Achana na huyo mbwa, tafuta life yako, wewe bado binti mdogo, hutakosa wa kukuoa na swala la watoto lisikuumize kichwa, utajua la kufanya baada ya kutoka hapo.
Tena usije ukasikiliza ushauri wa eti mkalishwe chini msuluhishwe, hiyo ni kitu mbaya sana, huwezi ukakubali kuishi na mtu aliekubali kukuheshimu baada ya kusuluhishwa na ndugu, hutakaa kwa amani kwa sababu atakuwa na masimango yasiyoisha kama anavyotumia kauli kuwa alikuoa kwa huruma. Achana na huyo mpuuzi. Medical solutions za tatizo lako zipo? Madaktari wanasemaje? Angalia mbele, achana na jitu jinga hilo.
Kuna vitu vya kumuomba Mungu. Hili la huyu Nacherewa Mungu alishalijibu zamani kwani ameweza kumuonyesha tabia kamili ya mume wake na lililobaki hapo ni kuchukuwa hatua. Tunatakiwa kuwa na maarifa Mungu ametupa akili... hakuna sababu ya kung'ang'ana na mume mzinzi. Wanawake wengi wamekuwa wanyonge kwa kunyanyasika na kuendelea kuvumilia mateso hata pale penye uwezo wa kutoka na kuishi kwa furaha na ndio maana makanisa yanajaa wanawake wanaolia kila siku kwa mambo ambayo hawakupaswa kuyalilia na matokeo yake huambulia kufa kwa magonjwa ya kuambukizwa na hao wanaume waliokuwa wakiwalilia usiku kucha. Wengine huwa wanafikia hatua ya kuwaombea hao wanaume wafe ili wawaache wajane! Wanawake zindukeniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii looool
Asante kwa ushauri, ninatibiwa kwa specialist , daktari anasema hili tatizo linatibika na ninaendelea kutumia dawa za hospital, ila na yeye anatakiwa atumia dawa na vyakula vya kuongeza sperm. Ila kwa stress hizi ni ngumu kupata mtoto na tendo lenyewe la ndoa ni mara chache mtoto atapatikana vipi.
yaani ukitakata kujua kwa nini wanawake wamejaa makanisani soma Zaburi 3:14-16, ni mwanamke kutambui adui yake ni nani.. yani inshort unamuambia indirectly aende for divorce, hata katika sheria ya nchi resort ya kwanza sio petition ya divorce lazima kuwe na usuluhishi..all in all, mtu atafanya atakalo, haya Mungu kamuonyesha tabia ya mume wake, the next move is hers, either stand in prayers or get a divorce, zote ni solution na zote zina majibu yake
Asante nitakitafutaKama utapata Muda soma kitabu kinachoitwa "BIKIRA YANGU" mwandishi ni Privatus Karugendo. Kingine ni UMEVAA MIWANI GANI & MAJI YAKIMWAGIKA YANAZOLEKA mwandishi ni Faustin M. Kamugisha.