Mkuu huo wosia wa mama uliuandika ukiwa wapi hasa?
Maana nataka nione ukiwa harusini wanapotoa wosia mtu anapata muda wa kuchukua notebook na kuandika eti wosia?!!!It is really beyond me!
Nachojua harusi zetu hizi za kiswahili,siku ya sherehe pale mbele,no one has that time ya kuchukua notes!
Nina wasiwasi na authenticity ya hiyo note-taking activity to begin with!
Sikufanya harusi mkuu, nilifanya ndoa tu kawaida.
Binafsi sikutaka kabisa harusi huo ni mmoja katika msimamo wangu niliouandika katika kitabu changu cha kumbukumbu.japo ingelazimu ningefanya harusi. Ila nilimwambia wife usishangae nkakuacha peke yako kati kati ya shughuli. sijui ni kama ni sababu ya umasikini au ushamba wangu ndio maana naliogopa kufanya harusi, sijui!
sikuwa napenda mambo ya harusi kabisa mkuu.hata nikiona watu wanafanya harusi nilikua nawaza Sana, hivi namimi kuna siku itakua hivi. Nafsi yangu ilikataa!
japo nilijua itakua hivyo ila wife naye nilimpanga ikiwezekana kikombe hiki kituepuke. nilimpanga naye akaniunga mkono.
na hata mama kabla sijaoa nilikua namwambiaga,sipendi kufanya harusi.
Mzee yeye hakua na shida kabisa,hanaga maneno.
Nilikua nawaza wazazi wa wife, na watu waliolikwa kwenye vikao vyao watakubali???
Kama utani tukatoa Kama wazo au ombi kwa mshenga.sikutegemea Kama tungeeleweka,sijui mpaka leo aliwafikishiaje na walijadiliana vipi. Lakini Mungu mkubwa,haiwi Haiwi ikawa. tukakubaliwa.
Hakukua na kwenda ukumbini wala kukodi Magari.na mwisho wa shughuli kila mtu alichukua njia yake, kabla hatujawaaga wazazi wetu wote kwa mara ya mwisho ili kila mtu akalale kwa mwenzie official kwa mara ya kwanza ndio mama akaniita na kuniambia hayo maneno.
Japo watu walioalikwa changanya na wapita njia walikua wengi wengi lakini haikuwa ile ya kuuzishana sura kiviiile! Jambo ambalo nilikua silipendi.
Sidhani Kama ilikua harusi ile. Me huwa naona ni ndoa nikifananisha na wanaofanya harusi.
Maneno hayo ya wosia niliyaandika nikiwa home siku chache baada ya ndoa.sababu ni kawaida yangu kuandika vitu tangu niko shule sec,ndio nilikorithi hiyo tabia.
Baada ya ndoa nilichukua kitabu changu nikaanza kujikumbusha na kuandika yaliyotokea siku ile na niliyoambiwa siku ile.
Kifupi mi napenda kuandika. Chochote kitakachonitokea kikanigusa lazima niandike.
Sijui Kama nimekujibu kidogo mkuu?