Kama timu inacheza hovyo namna ile lakini tupo top six mwalimu akirekebisha hata 10% ya makosa ya mapungufu ya timu si tunatwaa ubingwa.??
Trust the process
Akipatikana CB & CDM itakuwa mwanzo wa kutatua matatizo ya muda mrefu ya United.
Ila bado kuna hizi nafasi LW, RW, ST, CM & RB siyo za muhimu sana kuziangalia msimu huu ila zinahitaji maboresho.
LW: Rashford siyo wa kumtegemea kufanya maajabu kila msimu. Niliona tetesi za PSG kurudi tena kusaka saini yake, tukiwa na watu makini wala wasisite kuchukua pesa hiyo.
RW: Antony, Sancho hawajaonyesha kwanini wapo United. Pellistri na Amad naona kama ni suala la muda tu watauzwa.
ST: Martial ataondoka mwisho wa msimu, Højlund ndiyo tegemeo pekee kwenye nafasi hiyo ukimtoa Rashford ambaye siyo mzuri kama vile anavyotokea pembeni. Hili eneo ni tata sana maana kupata striker mdogo ili aje kugawana dk na Højlund ni ngumu sana ila kama inawezekana Sesko atafaa sana. Wakina Osimhen au Toney huwezi kuwasajili bila kuwahakikishia dk za kutosha kwenye msimu.
CM: McTominay, Eriksen, Casemiro huenda wakaondoka msimu huu. Usajili wa DM na CM utakuwa wa lazima.
RB: Kuna uwezekano wa Wan-Bissaka kupata offers mwisho wa msimu huu maana Dalot tayari ana mkataba mpya na ndiyo chaguo la kocha. Huenda EtH akamrudia tena Frimpong ambaye amekuwa na msimu mzuri sna B. Leverkusen akitumika kama RWB.
CB & CDM: Haya ndiyo maeneo ya msingi, ni muda wa Maguire sasa kuonyeshwa mlango wa kutokea kupisha wengine. De Jong na Barca inawezekana ukawa ndiyo mwisho wao, EtH akipewa nafasi ya kumsajili FDJ nahisi hataiacha impite: STATEMENT SIGNING.
Usajili wa Mount msimu ujao ndiyo utakuwa na faida maana baada ya Eriksen na McSause kusepa itapunguza gharama za kusajili viungo wengine wawili.
Ila rungu la FFP linavizia, hivyo biashara za msimu huu zitategemea pesa za mauzo ya wachezaji.
Kuhusu kutwaa ubingwa bado naona ni ngumu sana maana timu haina structure kwahiyo hata wachezaji wapya wakija watakuta bado ni kikosi kinachoundwa na muda wa kucheza pamoja utakuwa ni chini ya mechi 10 msimu mpya unaanza.
Ku-challenge EPL naona msimu wa 2025/26 ikiwezekana 100% kabisa.