Una Chuki na EMERY, nambie ARTETA lini kashawahi kuwa na Mfumo mmoja kwa kipindi cha Misimu 3 ya kwanza.
ARTETA ndo Huyu alikuwa anaitwa BUSTETA kwa kucheza na Mabeki 5, na alikuwa anamtumia SAKA kama Wingback na alikuwa anataka Muuza mpaka Klopp alikuwa Moja ya watu walomtaka.
Hamisi Mbona UNAONGOPA ndugu yangu?? ARSENAL ya WENGER ilikataaga Nafasi ya Mkurugenzi wa Michezo "DOF" na WENGER alipendekezewa Jina la GAZIDIS akamkataa MICHAEL ZORC, na Hamjawahi kuwa na Wachezaji hao wazuri unaosema. SVEN alikuwa ni "HEAD OF SCOUTING" Arsenal wewe unatuambia ni DIRECTOR OF FOOTBALL" Wa ARSENAL ipi Hiyo?
Yani EMERY NI POOR Kwenye TALENT ID! Naweza ingia Imani hili neno unapenda litumia lakini Labda unalielewa Tofauti. EMERY ndo Mwalimu aliemsajili SALIBA, LENO , TIERNEY, CEBALLOS, MARTINELLI, ambao alikuwa anaanza tengeneza timu. Amemtoa SAKA, SMITH ROWE academy. Nitajie Jina moja mpo nalo kwenye KIKOSI Chenu cha kwanza ARTETA amemtoa ACADEMY, Kingine nitajie Mchezaji ARTETA kamsajili hana Jina kamfanya kuwa WORLD CLASS.
Najua Wengi wenu Mliitelekeza ARSENAL, Nikwambie tu Sajili ya PEPE ni ya Bodi yenu sababu za Kibiashara ila EMERY alimtaka ZAHA. Kuuzwa kwa SAKA ilikuwa ishu ya BODI na masuala ya mkataba.
Mbona umeongea mambo mengi ya uongo
Arteta ametumia mifumo mitatu toka aje Arsenal ,3-4-3 ,4-2-3-1 na 4-3-3 mpaka Sasa
Sven misiltant alikuwa head of scouting Lakini majukumu yake mengine yalikuwa Kama Director of football
Unadanganya Arteta alitaka kumuuza Saka ,huu Ni uongo mkubwa
Uongo mwingine mkubwa ,Saliba ,Leno ,Toreira ,Ceballos , Tierney , Sio sajili za Emery , Emery alikuwa head coach tu
Ndio maana hata hizo Sajili bado alikataa kuwatumia mchezaji Kama Toreira ,Ceballos , hata Pepe baadae alianza kumpiga bench sababu chaguo lake alikuwa Zaha,
Emery hakuwa kufanya sajili yoyote hapo Arsenal,ukitaka ushahidi wa kila sajili unazodanganya hapo juu nitaweka ,Saliba, Martinelli ,Ni sajili za Fransis Cagigao ,Leno, Toreira,Auba,Guendoz ,Tierney Ni sajili za Sven misiltant
Emery hakuwahi kusajili mchezaji yeyote hapo Arsenal narudia Tena huu Ni UONGO MKUBWA.
EMERY alimtaka Zaha ,bodi ikagoma ,Emery alikuwa tayari kumtoa Saka plus £40m bodi ikazuia
Nakupa na hii Emery huyo huyo alikuwa tayari kumtoa Smith Rowe plus £25m ampate Upamecano aliyekuwa Leipzig kipindi Smith yupo Leipzig kwa mkopo
Sijui unanielewa
Emery amewatumia Saka Kama beki ,martinell Kama CF, Tena hawazidi hata mechi 5 ,
Arteta ndiye aliyekuja akawaamini na kuwapa namba 7,10 na 11
Akamtoa Saka Kama LB kwenda LW ,LW ,LCM had RW
Arteta ndiye kamfanya Saka ,martinell kuwa moja ya mawinga Bora duniani
Narudia Tena Sajili za Saliba ,Martinelli Ni za Francis Cagigao ,Emery aliwataka kina Nzonzi ,kutoka Sevilla
Nakusubiri uje na uongo mwingine ,mm na ushahidi mwingi Sana