Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

𝐃𝐀𝐑𝐀𝐒𝐀 𝐇𝐔𝐑𝐔 π”π‹πˆπŒπ–π„ππ†π”ππˆ

β€’Kwanini vilabu vikubwa vimekuwa vikisuasua??

Manchester United and Chelsea hivi vilabu havina tena mvuto wa kuangaliwa na mashabiki zao kama zamani (miaka 25 iliyopita) kwa miaka 5 iliyopita Chelsea imekuwa na changamoto kwenye kusogea nafasi ya kwanza katika Premier League, huku Mashetani wekundu (Manchester United) tangu mwaka 2013 kipindi cha utawala wa Sir Alex Ferguson klabu imekuwa na changamoto ya kumpata kocha ambaye anaendana na Falsafa za klabu hiyo.

Kwa wakati flani kocha JosΓ© Mourinho aliipa heshima klabu hiyo mwaka 2017 lakini hakufanikiwa kubeba Epl.

Kwa miaka 7 sasa Utawala wa Manchester City umekithiri huku vilabu vidogo vidogo kama Tottenham Hotspur, Aston Villa na Newcastle United vikijitutumua kuchukua nafasi ya Manchester United na Chelsea huku klabu kongwe Liverpool ikiwa kwenye mizani (kupanda/kushuka)





Arsenal msimu uliopita alitawala soka la England hata msimu huu pia mwendo ni uleule vijana ni wengi na wanauchu na ubingwa lakini kuna timu imekuja na nguvu mpya Tottenham ambao msimu uliopita walikuwa tofauti na msimu huu...Nini cha kufanya?

Pochettino na Ten Hag wanatakiwa kufaham ligi ya Uingereza siyo mchezo ingawa Pochettino anafaham utawala wa vilabu mbalimbali vya Uingereza vinaugum lakini sasa kashindwa kupenya kwa kila ngome matokeo yake anaweza kufutwa kazi kwa wakati flani

Ten Hag naye msimu uliopita alifiti zaidi katika Premier League kwa wakati huo na akiwa kocha mpya lakini mazowea Epl amekuwa kama kocha mpya vilabu vido anapata pointi kwa shida zaidi.

NOTE

Ni kocha mmoja tu aliyekuja England akakaa mwaka mmoja bila kombe lakini mwaka uliofuatia akabeba Epl tena misimu miwili mfululizo.

Erik ten Hag hatakiwi kuwa na hasra mana wachezaji ni kama watoto wadogo wanatakiwa kuelekezwa pa sipo na hasra hapo watajirekebisha wao pasipo na kupelekeshwa.

Erik ten Hag kibarua kinaweza kuota nyasi siku za usoni endapo mwenendo wake utakuwa hivi.

Pochettino na Chelsea yake ni vichekesho kabisa wachezaji wapo na wenye viwango bora lakini mfumo wa kocha umekuwa shida kwao kila mchezaji amekuwa wa kawaida sana.

Pochettino anaweza kuungana na kocha wa Manchester United Erik ten Hag kwa kupoteza vibarua vyao huko kwenye vilabu vyao.

Β°Falsafa za vilabu hivi vimeisha imebaki tu kama Kumbukumbu kwamba vimewahi kutawala ligi ya EPL kwa miaka mingi iliyopita hasa Manchester United.

Β°Tottenham Hotspur, Newcastle United, Aston Villa hivi ni vilabu ambavyo vinaweza kuja na tishio kwa misimu kadhaa mbeleni kwa sasa bado vinaendelea kujenga timu zao.

Kwa habari za michezo zaidi follow Benjamin Bruce Sport's

Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app
Wengine muwe mnaenda kulima njegere tuu
 
Team imekuwa ya kijinga sana hii, sikui ETH anafundisha nini tu. Hatueleweki tunacheza mfumo gani, hatuwezi kupiga pasi 5 bila kupoteza mpira, huko mbele watu wanapishana kama wanaenda sokoni(hakuna ubunifu wowote).

Kama tunapigiwa mpira mwingi hivi na kateam ka Denmark, EPL tutamaliza nafasi ya ngapi..?
Na katika hali kama hii...kinachofuata ni kukaziwa adi na watoto wadogo yaani apa kina palace na wolves wale....maana wanaamin wakikomaa kwako wanachukua points vizur tu kwakuwa wanajua hivi sasa Man Utd ni papatu papatu na hamshindi kwa uwezo wa timu kama timu.

Dah!...hii timu yenu ni bora ingeuzwa tu, mie sio shabiki wa united lakini na Stick na hoja ya G.Neville...kuwa shida ipo kuanzia hierach adi kwa wamiliki wa timu.

Yani...Carragher anasema wachezaji ndo wenye shida lakini NACHOKIONA NI KUWA WACHEZAJI WENU HAWAWEZI KUFANYA ZAIDI YA PALE TULIPOONA...tukiaanzia mechi zote na mahasinu wenu mlizopigwa 6-3 kwa city, ile ya 7-0 kwa liver(tena ilikuwa ni liver ile mbovu) na ata jana 0-3 kwa city pale OT. Na adi kufikia timu kubwa kama united kuwa na wachezaji wasioendana na hadhi ya timu...inatokana na POOR SCOUTING NA RECRUITMENT DEPARTMENT YA TIMU YENU(Ambapo ndio apa alipomaanisha NEVILLE...YAANI TATIZO LA KIUONGOZI)...Hapa naenda mabali zaidi kwa kusema Either MNASAJILI WACHEZAJI WA KAWAIDA WASIOOENDANA NA PROJECT YA CLUB au WANAOSAJILIWA HAWAJAKIDHI MAHITAJI YA FALSAFA(STYLE YA UCHEZAJI) YA MAKOCHA WENU....MAANA UKIANGALIA KATIKA MECHI ZOTE HIZO ZA 6-3, 7-0, ile ya madogo Copenhagen ushindi wa papatu papatu na ata ile jana kupigwa na City OT 0-3....WAEZA UKAONA KABISA UNITED HAIELEWEKI INATUMIA FALSAFA/STYLE GANI YA KIUCHEZAJI...NA KOCHA KAMA TEN HAG NI KOCHA MKUBWA NA AMBAYE KAPITA KWENYE TIMU KADHAA ULAYA IKIWEMO BAYERN NA AJAX....TOKEA ALIVYOKUWA BENCHI LA UFUNDI BAYERN....HIVYO HUWEZ SEMA ETI HANA FALSAFA YAKE SIO KWELI, ISIPOKUWA HAPO WACHEZAJI WAMESHINDWA KUENDANA NA FALSAFA YAKE YA KIUCHEZAJI NAHISI.
 
Maisha yanitese na Man U initese pia.??.

Nimeamua kurudi nyuma kidogo..mechi zetu hata hazina mzuka tena
Mkuu sio mzuka tu KIUKWELI MANCHESTER DERBY...haivutii tena maana ni ONE SiDED FOOTBALL mshindi anafahamika....na sio ilo tu Man united wanashindwa ata kuonyesha kandanda safi dhidi ya wapinzani wao Man City...

Hivyo DERBY YA MANCHESTER IMEPOTEZA MVUTO KULINGANISHA NA DERBY NYINGINE PALE ENGLAND KAMA NORTH LONDON DERBY...Na tatizo ni nyie Hampo tena katika Level ya kiushindan mliyokuwaga nayo pale EPL.

Wee ona pamoja na chelsea kuwa vibaya lakini atleast kampa arsenal Game nzuri ile juzi...Derby yao ilivutia kiukwel.

Kiukwel naona atakayempa city mchezo wa kiushindani msimu huu ni LIVERPOOL na mchezo utakuwa mkali maana LIver nao wamerud kwenye viwango vyao kulinganisha na msimu uliopita...kwa arsenal sidhani washukuru walishinda ile mechi ya pale kwao Emirates ila Etihad watapata tabu wale pia....ukizingatia KDB atakuwa kesharudi
 

Tena uyo dogo wenu PELLISTRI Ndo aliongea pumba kabla ya mechi ya jana....kuwa "Akitokaga na girlfrend wake kuzunguka pale jijini manchester haonagi mtu ata mmoja akiwa amevaa jezi ya City"....Pep alivyoulizwa ilo swali na pundit nae akajibu kisiasa kuwa " Atajaribu kuwauliza Puma kwanini jezi za Man City zimeisha madukani pale manchester".

Ukitizama apo...unaona kabisa yule dogo aliropoka...kuridhisha media lakini sio kweli kwamba uzunguke jiji lote la Manchester eti usione raia aliyevaa jezi ya City....No tena BIG NO....Maana kiasili hizi timu zina mahali zilipoanzishwa MFANO ATA PALE MERYSEYSIDE...INAFAHAMIKA KUWA LIVER NDIO MWENYE MAFANIKIO MAKUBWA NA MAKOMBE MENGI LAKINI BADO EVERTON WANA MASHABIKI/WAZAWA WAO JAPO SIO WENGI kulinganisha na LIVERPOOL...Sasa how Come useme Hakuna shabiki wa City katika jiji la manchester??....Na wale wanaoingiaga Match Days za kila weekend pale etihad wanatokaga wapi??...

KWANZA JIJI LA MANCHESTER LINA VITONGOJI VIKUBWA VIWILI...ACHILIA VENGINE VIDOGO VIDOGO KAMA SALFORD...NAVYO NI STRETFORD...AMBAPO HAPO NDO MAN UNITED ANA NGOME NA WAZAWA WENGI WA HAPO NI UNITED LIA LIA....PIA STOCKPORT ALIPOZALIWA FODEN...AMBAPO WAZAWA WENGI WA HAPO NI CITY

Pia yule mtoto anataka kutuaminisha haoni jezi za City Jijini Manchester...Na hawa watu wote hapo chini wanaishi wapi labda??...au sio MANCHESTER HII HAPO PICHANI...NA KAMA HAPO NI MANCHEATER SASA INAWEZEKANA VIPI USIONE JEZI YA CITY KATIKA JIJI LA MANCHESTER KAMA ALIVYOJINASIBU PELLISTRI.

Screenshot_20230612-231530.jpg

Screenshot_20230612-224222.jpg
 
Ten hag kutimuliwa amepewa odds 10 πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…
 

Attachments

  • Screenshot_20231030_102718_1xBet.jpg
    Screenshot_20231030_102718_1xBet.jpg
    65.4 KB · Views: 8
Team imekuwa ya kijinga sana hii, sikui ETH anafundisha nini tu. Hatueleweki tunacheza mfumo gani, hatuwezi kupiga pasi 5 bila kupoteza mpira, huko mbele watu wanapishana kama wanaenda sokoni(hakuna ubunifu wowote).

Kama tunapigiwa mpira mwingi hivi na kateam ka Denmark, EPL tutamaliza nafasi ya ngapi..?
Tuliwaambia mpira wa janja janja ni mbio za sakafuni

Mkasema 7Hag nomaaa
Wazee wa gengeni
 
ETG kipara feki

Ni tapeli, jasusi au profile zote hizi anazo?
Mgunda yupo vizuri kuliko huyu muhuni
 
Kutoka kwa Privadinho

Leo kiukweli Ten Haag ameniudhi. Kwanza amenifanya niwe na wasiwasi mkubwa na capabilities zake as coach

Mimi sina uwezo mkubwa kiukufunzi kuliko yeye lakini naweza kufanya tathamini ya kile ambacho ameleta mezani

Leo amesema John Evans ameanza mbele ya Varane kwa sababu za kimbinu, akamweka Regulion bench ambaye ni Natural left back huku akianza Lindelof upande huo.

How dare against Man City? Ina fact kuna kiburi kipo nyuma yake. Nahisi kuna sura ua Ferguson anataka kuivaa.

For me its too early kwa Ten Haag hata kuvaa soksi chafu za Fergie achilia mbali viatu vyake.

Ukitazama mentality ya wachezaji wa Man United wapo so stressed. Mtazame Anthony alivyoingia? Ni kama aliingia na jazba? Why? Tazama drama za Sancho?

Haya rudia tena Interview za Ronaldo na Dressing room ya Ten Haag. Kuna kaubabe au niseme kajeuri ambako Ten Haag anajipa.

Kitendo cha management kumwamini na kumpa mamlaka Ten Haag sidhan kama kina afya kwa Ten Haag

Naelewa why Management ya United ilimpa mamlaka Ten Haag, ni kwa sababu kulikuwa na presha kubwa kwa Ex coaches wa United walilalamika kuwa hawasikilizwi.

For its bad timing, wamefanya jambo sahihi, ila they are having average coach.

Tazama sajili zake, angalia game plan zake. Hata kwenye sub binafsi zinaambatana na ubabaishaji au ubahatishaji.

For me Ten Haag is not right man for the Job. Anatumia leseni ya babu yake kuendesha gari.

Atatuua kwa stress huyu baba. Hana character wala personality ya kubeba image ya United kwenye tough moment. We need strong and gaffer with amazing exposure.

Credit: Privaldinho
 
Back
Top Bottom