𝐃𝐀𝐑𝐀𝐒𝐀 𝐇𝐔𝐑𝐔 𝐔𝐋𝐈𝐌𝐖𝐄𝐍𝐆𝐔𝐍𝐈

•Kwanini vilabu vikubwa vimekuwa vikisuasua??

Manchester United and Chelsea hivi vilabu havina tena mvuto wa kuangaliwa na mashabiki zao kama zamani (miaka 25 iliyopita) kwa miaka 5 iliyopita Chelsea imekuwa na changamoto kwenye kusogea nafasi ya kwanza katika Premier League, huku Mashetani wekundu (Manchester United) tangu mwaka 2013 kipindi cha utawala wa Sir Alex Ferguson klabu imekuwa na changamoto ya kumpata kocha ambaye anaendana na Falsafa za klabu hiyo.

Kwa wakati flani kocha José Mourinho aliipa heshima klabu hiyo mwaka 2017 lakini hakufanikiwa kubeba Epl.

Kwa miaka 7 sasa Utawala wa Manchester City umekithiri huku vilabu vidogo vidogo kama Tottenham Hotspur, Aston Villa na Newcastle United vikijitutumua kuchukua nafasi ya Manchester United na Chelsea huku klabu kongwe Liverpool ikiwa kwenye mizani (kupanda/kushuka)
>>>Wachezaji wa Manchester United hawajitumi wanaendelea kumuangusha kocha wao.
>>>Wamechoka mapema yale mashambulizi na kutawala mchezo umekuwa wa kawaida kila timu inapenda kukutana na Manchester United au Chelsea kuliko vilabu vingine ili kwa sababu vinajua Manchester United na Chelsea ni vilabu ambavyo havina ugumu wa kufunguka mabeki zao na viungo vyao ni vyepesi wa kufunguka.

Arsenal msimu uliopita alitawala soka la England hata msimu huu pia mwendo ni uleule vijana ni wengi na wanauchu na ubingwa lakini kuna timu imekuja na nguvu mpya Tottenham ambao msimu uliopita walikuwa tofauti na msimu huu...Nini cha kufanya?

Pochettino na Ten Hag wanatakiwa kufaham ligi ya Uingereza siyo mchezo ingawa Pochettino anafaham utawala wa vilabu mbalimbali vya Uingereza vinaugum lakini sasa kashindwa kupenya kwa kila ngome matokeo yake anaweza kufutwa kazi kwa wakati flani

Ten Hag naye msimu uliopita alifiti zaidi katika Premier League kwa wakati huo na akiwa kocha mpya lakini mazowea Epl amekuwa kama kocha mpya vilabu vido anapata pointi kwa shida zaidi.
NOTE

Ni kocha mmoja tu aliyekuja England akakaa mwaka mmoja bila kombe lakini mwaka uliofuatia akabeba Epl tena misimu miwili mfululizo.

Erik ten Hag hatakiwi kuwa na hasra mana wachezaji ni kama watoto wadogo wanatakiwa kuelekezwa pa sipo na hasra hapo watajirekebisha wao pasipo na kupelekeshwa.

Erik ten Hag kibarua kinaweza kuota nyasi siku za usoni endapo mwenendo wake utakuwa hivi.

Pochettino na Chelsea yake ni vichekesho kabisa wachezaji wapo na wenye viwango bora lakini mfumo wa kocha umekuwa shida kwao kila mchezaji amekuwa wa kawaida sana.

Pochettino anaweza kuungana na kocha wa Manchester United Erik ten Hag kwa kupoteza vibarua vyao huko kwenye vilabu vyao.
°Falsafa za vilabu hivi vimeisha imebaki tu kama Kumbukumbu kwamba vimewahi kutawala ligi ya EPL kwa miaka mingi iliyopita hasa Manchester United.
°Tottenham Hotspur, Newcastle United, Aston Villa hivi ni vilabu ambavyo vinaweza kuja na tishio kwa misimu kadhaa mbeleni kwa sasa bado vinaendelea kujenga timu zao.

Kwa habari za michezo zaidi follow Benjamin Bruce Sport's
Sent from my SM-A047F using
JamiiForums mobile app