licha ya kwamba msimu huu wamefanya vizuri kiupande fulani kitaarifa lakini bado haiondoi ukweli wa kwamba muppetiers si chanzo cha kuaminika kwa taarifa za manchester united.
juzi niliweka taarifa kutoka chanzo hicho cha muppetiers kwa njia ya utani utani (wengi hawakunielewa)
mupptiers wanasema hivi:
- masoun mount na hojlund ndio wachezaji pekee waliosajiliwa msimu huu kwa mapendekezo ya recruitment team (kwa maana hapa erik hakuwa na nguvu kubwa)
- onana na amrabat (mkopo) ni wachezaji waliosajiliwa kwa mkono wa erik ten hag
- muppetiers wakaenda mbele .....wanasema casemiro haonekani kuwa ni mchezaji aliye kwenye mipango ya muda mrefu wa klabu na ulikuwa usajili wa dharura......recruitment team kwa sasa inatafuta mbadala wake na mchezaji anayelengwa ni palacios wa bayer leverkusen (injury prone)
usajili wa manchester united
- kocha anakuwa na target zake
- recruitment team wanakuwa na target zao
baadae wanafanya decisions, usajili pale man utd unafanywa hivi kwa mujibu wa waandishi wa habari niliosoma taarifa zao kwa nyakati tofauti.
mfano:
- mourinho hakumtaka fred
- huwezi kuniambia usajili wa matic ni wa recuitment team, bali ni usajili wa mourinho na alipoondoka matic hakuwa na career nzuri (mwisho matic kamfuata mourinho)
tatizo la manchester united bado hawana IDENTITY.
tunachezaje, tunatakaje, tunamhitaji nani kwa lengo gani........
usishangae anaondoka ten hag, baadae unaletewa conte