buffalo44
JF-Expert Member
- May 8, 2016
- 5,126
- 13,106
Bila Kuwasahau Newcastle jitu kama Joelinton, Wilson, Dany Burn yaani mijitu ya kuforce kona inaingia, Brighton kuna Wellbeck akiwa kwetu alikua mwembamba kuna Dunk,Timu za wenzetu wanafanya mazoezi gani, Wolves unakuta mijemba imepanda kweli kweli ina nguvu, Fulham kuna mijitu vile vile ile dk ya 90 Adama alipepea weee mpaka golini jitu kweli kweli, Njoo Nottingham mbele kuna Jitu Awoniyi, Bolly, Worall, asee. Yaani timu yetu tu ndio unaona kama hawali vile wala hawa nguvu.
Shida nini? Alafu mijitu inalipwa pesa neefu?
Aston Villa kuna vijitu ila vimekomaa na majitu kweli kweli Watkins, Mings, Khonsa, House. Namkubali Watkin dogo mkatili ana nguvu mpaka ya shuti sifa za strikers.
Njoo Tottenham aliyetuadhibu ni Sarr ni dogo ila amepanda intensity kila sehemu
Arsenal ndio wako kama sisi ila kidogo wanatuzidi intensity.
Palace nayo ina mijitu Schlupp, Guehi, Edouard.
Litimu langu, Unaona kabisa kama hawali vile mwangalie Varane, Martinez, Dalot, Wan Bissaka, Mount, Ericksen, Mbele Martial, Bruno, Gernacho unajiuliza wananyanyua nondo kweli.
