Dah! Tuacheni masikhara asee, Kwamba ETH hana Uwezo wa Kung'amua Talent !! Mourinho wakati fulani alimwambia Gary Neville na Scholes kwamba Ualimu sio kama Kusimama Mbele ya Luninga kubwa na kuwasogeza wachezaji huyu angekaa hapa huyu alitakiwa kuwa hapa wakati Mpira unapigwa, kwa kusogeza tu kwenye zile Screen zao za Uchambuzi.
Pep akiichukua City sajili za awali kabisa alikuwa na Kina Nolito, Marlos Moreno, Bravo n.k wote hao hakuna walichofanikiwa kwa falsafa ya Pep {So kwa Point yenu ina maana na yeye Hana Talent ID}, ETH amekuwa na Msimu mmoja sajili 4, Cup Finals 2, 3rd Place finish, I Trophy! Kwa standard ya UTD huwezi ita haya ni mfanikio but kwa kile timu inapitia unaona Mwangaza,
Klopp mpaka anapata Rhythm ya timu yake wachezaji alowakuta ni kama 2/3. Arteta Mpaka Arsenal inacheza kwa namna anataka ni takriban msimu wake wa 3!
Moja ya Kazi Rahisi sana ni Kuchambua kilichotokea {nazungumzia tunaowaita wachambuzi wa soka}
WAPE TIMU WAWE WALIMU! ETH Akiwa anaichukua FC Utrecht timu ilikuwa ishajikatia tamaa ila kwa Ubora yupo nao kung'amua Talent alimchukua Haller kwa Mkopo toka Auxerre, Aliwachukua kina Zacharia Baykal, na Academy akatoa Chuma kadhaa ikiwamo Sofyan Amarabat. na Aliifikisha mpaka Playoff ya Mashindano ya Ulaya akapigwa na Zenit ya Mancini ilokuwa na mastaa kibao wakatolewa kwa tofauti ya Goli 1.
AJAX. ETH kaenda Ajax inasua sua, Ila mpaka anaondoka ana Debutants 23 wakiwamo hawa wa juzi juzi kina
hamis77 wanawasifia ni wachezaji haswa kina Timber. List ni ndefu mno ila ina kina Gravenberch, Neres, Kudus, Dest, K.Taylor, Licha, Alvarez n.k
Utambuzi mzuri wa Talanta unaanzia Ndani, Pep alivuka mstari akiwa La Masia, ETH kaprove na Ajax mara 2 Kwa ngazi kubwa ya Mashindano ya Klabu Ulaya! Ukitaka jua anaweza anachofanya watizame Ajax wanavyojitafuta tangu amewaacha. UTD tumekuwa na Utaratibu wa kuamini Academy yake na ndo imeleta wonders mara nyingi tu. ETH Still anamtengeneza Garnacho na unaona mwanga ni muda tu atakuwa moja ya World Beater, Kuna Mainoo taratibu ataanza eleweka, kuna Isak Hansen Aaroen na wengine wengi tu. Msimu huu kaongeza sajili 3 so timu yake ina watu 7 alowasajili
Husajili leo timu ika-click Kesho. Pep timu yake ya Treble kaanza ipata baada ya kupasuka na Palace 0-2 Etihad wakati hapo Arsenal gari lishawaka ila likaangushwa na utoto wao. ETH Kashajifunza huezi implement vitu kwa haraka kiasi hicho, Alijaribu huo Ujinga kwa Brighton na Brentford ikawa aibu ameamua tafta matokeo wakati anajenga timu yake.
Kuna wataoleta Hoja ya Kina De Zerbi, kabla hujampa Daraja Unampa Jifikirie sana kwa nini akitoka Sassuolo hakuna timu ilikuwa na Mda naye!