Kwangu hii ndio mechi ambayo timu ilikuwa mbovu kuliko siku zote,Olympiakos ni timu kibonde ukilinganisha na nyingine zote zilizoingia kwenye hii stage but kwa kiwango cha jana Moyes ana kazi nzito sana,timu nzima ilikuwa imechoka kuanzia mpira unaanza.Rio,Vidic,Carick,Cleverley,Rooney,Smalling,Valencia,Young walikuwa kama wamelazimishwa kucheza.Inaonekana wachezaji hawamkubali kabisa Moyes hata ukiangalia body language wanaonekana kama kila mtu anacheza kivyake.Sioni hata half time au kwenye mechi akitoa maagizo kama kuna mchezaji wanamsikiliza na kumfatisha
Kuna haja ya kuwarudisha wasaidizi wa SAF (Carlos Quirez au Rene) waje kumsaidia Moyes otherwise sioni dalili kama Moyes anaweza kuibadilisha hii timu.Management ilikosea sana kumpa contract ya miaka 6 nafikiri wangempa miaka 2 then akiibadilisha timu ndio wamuongezee