Arsenal siyo kwamba mna kikosi kibaya, tatizo hamtaki kukubali ukweli.
Tukipitia kila mchezaji defence yenu yote na kipa siyo wachezaji wanaopaswa kuanza kwenye timu yoyote ile inayopambana kubeba EPL au UCL.
Midfield ni Rice na Ødegaard tu unaweza kuwategemea na siyo Havertz.
Front line pale ni Saka tu, huwezi kutegemea striker kama Jesus ubebe EPL au UCL.
Labda kama nyie wenzetu mna vipaumbele tofauti na kushinda makombe.
Ndiyo maana mimi huwa sipo excited na msimu wowote wa United kwasasa kwasababu nishakubali United haiwezi kushinda EPL wala UCL msimu ujao na ikitokea yatakuwa ni maajabu ktk soka.
Mashabiki wa Arsenal tatizo lenu ni kujipa matumaini makubwa sana. Mna kikosi cha kawaida sana. Msimu ujao mkijitahidi sana ni top 4 place, UCL kule kwa hicho kikosi mnaweza kufika last 16. Makombe ambayo mnaweza kushinda kwa hiyo squad ni FA Cup na Carabao.
Kwa takwimu za msimu ujao nikipanga combined XI ya wachezaji wa United x Arsenal itakuwa hivi.
View attachment 2684958