IKIWA MANCHESTER UNITED WATAMPATA ANDRE ONANA,ITAKUA NI DIRA BORA KWA ERIC TEN HAG.
Hali ilivyosasa..
Ni wazi fika Man united kwasasa inakumbwa na hali ya kutokua na kiwango kizuri cha fungo la usajili,kuna baadhi ya taarifa zinasema kiwango alichopewa Ten Hag ni £120 mil.
Licha ya kuwa taarifa hizi sio rasmi lakini bado haifichi ukweli ya kuwa United kwasasa wapo kwenye ugumu katika fungo la pesa za usajili. Pia bado eneo la utawala bado halijakaa sawa, Hakuna kinachoeleweka moja kwa moja. klabu inauzwa ama la.!!.
TIMU LAZIMA IENDELEE.
Ten Hag analijua hili, kazi yake ni moja tu,kuhakikisha timu inafanya vizuri pasina kujali kile kinachoelendelea juu,ukiwa kama Meneja mkuu kazi yako kubwa ni kudhibiti kitaaluma kitengo ulichokabidhiwa.
Kitalamu Erick anavyo vipaumbele kuhusu timu yake kuelekea msimu ujao,na niwazi anahitaji kuingia ndani ya pre-seoson akiwa na ukamilifu wa baadhi katika orodha yake, Tayari anaye Mason Mount, kisha anamuhitaji Onana.
KWANINI ANDRE ONANA,AU KWANI GOLIKIPA MPYA.
Kwanza ni katika kuhakikisha timu inacheza kama anavyotaka. Msimu ulioisha Ten Hag alibezi zaidi kwenye mkakati kuliko falsafa. mkakati ni kuhakikisha timu inapata matokeo pasina kujali ni mtindo upi mama utatumika kuhakikisha unapata matokeo .
Falsafa ni mtindo unaoeleweka wa uchezaji katika kuhakikisha timu inapata matokeo.falsafa ya Hag ni kuifanya timu yake inadhibiti(umiliki ) wa mchezo,pasi na nafasi .
United ya Hag haikucheza hivyo, hii ilitokana na yeye kutokua na ufahamu mzuri wa kiufundi kuhusu wachezaji wake kiutendaji .
KUSUKA MTINDO WA UCHEZAJI.
Falsafa za kudhibiti mchezo zinahitaji uwe na mlinda mlango mwenye uwezo mkubwa wa kudaka na mwenye umahili miguuni, ili kufanikisha adhma yake anahitaji kwanza golikipa wa namna hiyo(hapa ataenda kutengeneza style of play) kisha baadae itabakia kwa mchezaji mmoja mmoja kutekeleza majumu kiufundi.
KATI YA MSHAMBULIAJI NA GOLIKIPA NANI MUHIMU KUMPATA KABLA.
Ten Hag anaenda kuitengeneza United kifalsafa, na hii itatokana kama atampata mapema mlinda mlango anayemuhitaji. Dira ya uchezaji inatengenezwa kuanzia kwa golikipa,kisha mbinu za kiujumla zitatengenezwa kutokana na aina ya wachezaji alionao.
kutokana na bajeti iliopo ikisema usajili mshambuliaji mahili inamaana hautampata golikipa unayemuhitaji, itakulazim utoke nje ya falsafa, kitu ambacho sio sera ya makocha waliokulika kwenye misingi ya sera hiyo.
Jibu mlinda mlango ni muhimu zaidi katika falfasafa kuliko mshambuliaji,Ukimpata Onana umeipata falfasafa,kisha mambo mengine yatafuta baada ya kuipata cream ya timu .
JE TIMU INAWEZA KUFANYA VIZURI PASINA MSHAMBULIAJI WA KATI.
Ndio, bila shaka... ikiwa kama utakua na ugumu katika kuzuia na kucheza soka safi utakua na nafasi kubwa ya kushinda mchezo.
mfano Man city ya msimu wa 2021/2022 iliweza kuchukua taji pasina kuwa na mshambuliaji mahili wa kati, Muda mwingi gabriel Jesus aliwekwa bench. hata Arsenal hatari ya msimu ulioisha bado haikua na strike mahili lakini ni mingoni mwa timu zilizofunga mabao mengi,.
Wachezaji wake wengi wa mbele waligawana mabao. United inawachezaji wengi mahili nafasi ya mbele, unaweza kuwatumia hawa wote kuhakikisha wanakupa mabao, una Sancho, Antony,Rashford ,Martial,Bruno fernandez,Mason Mount na Mason Greenwood, hawa wote wanauwezo wa kufunga na kuasist..
KUUZA SIO RAHISI KWASASA.
Utaanzaje kuuza wachezaji ukiwa hauna uhakika wa kununua wengine. haiwezekani kabisa. Malengo makubwa ya Ten Hag ni kuhakikisha anatumia nyenzo alizonazo kutengeneza anachokihitaji, kama kutakua na mbadiliko yeyote basi anaweza kuyafanya baadae ila kwasasa tusitegemee kuona United inauza baadhi ya wachezaji wake wa kikosi cha kwanza.
WASHABIKI WAMSAPOTI TEN HAG.
Bila kuficha kwasasa United ndio timu ambayo haieleweki nini inakifanya, inawachezaji wengi ambao ni mizigo, haina pesa, haina uongozi imara. kwa ufupi United ni kama dume la ng'ombe ambalo halina faida.
Usitegemee kuiona Unitd inashindana na timu kama Man city,Arsenal na Real Madrid. Ondoa matarajio kuhusu Manchester united.Jiandae kwa chochote . Nakuhusia play katika sehemu unayoiyona itakufaa kama shabiki,napo ni kumsapoti Ten Hag.
Wasallam..
Kalamu ya Nasri kulemba
follow instagram Nasrikulemba.