Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

"Kilichobaki ni kula maandazi tu."

We're not serious as a club. Kuanzia wamiliki, kocha na wachezaji.

Tumewapa City treble. Mechi ya FA Cup wachezaji wetu walichoweza ni kuongea tu vitendo sifuri. Walijisifu kuwa tutazuia City kushinda treble (Rashford) lakini hakuna wanachojali kuhusu hii timu. Garnacho pekee ndiyo alionyesha kujali na kuipambania jezi ya United.

Baada ya fainali ya FA Cup, De Gea alipaswa kuonyeshwa mlango wa kutokea ila bado kocha anaruhusu aongezwe mkataba.

Mchezaji kama Sancho ana mfululizo wa misimu mibovu ila jana kaonekana tayari anawahi vacation.

Hatuwezi kuwafikia City bila kuwa na wamiliki walio na mpango kazi na wapo tayari kuwekeza kwenye mawazo ya kocha na kuwa na watu wenye viwango na ushindani ktk nyadhifa mbalimbali ndani ya club.

Hatuwezi kuwafikia City tukiwa bado tunawategemea wachezaji kama De Gea, Martial, Maguire, Fred, McTominay, Elanga, Sancho.

Hatuwezi kuwafikia City tukiwa na kocha asiyefanya maamuzi magumu. Kumpa mkataba De Gea ni kosa la kwanza. Tutalipa mishahara mikubwa kwa watu kukaa bench na hawana uwezo.

United ni lazima ikubali kumalizana na wachezaji hasa legends, huwa ni ngumu sana sisi kuwatimua wachezaji. Madrid wamemuachia Benzema ingekuwa ni sisi angebaki tutafute backup yake. Siyo kazi ngumu kujua kuwa De Gea muda wake ktk top level football unamalizikia.
Hakika msikumbatie watu.. Anzisheni upya.

Hlf mpeni team mwarabu sema tu siasa na roho mby wa wazawa pale England khs mwarabu lkn ndo wanafaa sana kuwavusha ili muweze kwenda mguu kwa mguu na sisi. Vinginevyo tena na pep akiwepo asee makombe makubwa mtayasikia tu bila investment za maana kwny team.
 
Kama sijakosea,kuna kipindi Onana alikuwa anazurula bila timu kabla Inter hawajamsajili na imewalipa.
Hawa Scouts wa Man Utd sijui huwa wanafanyia wapi kazi zao za kutafuta talents!
Kwa nilichoona onana anapass accuracy nzuri kushinda middle wetu fred na mac halafu tunataka kupambania kombe. Huu msimu ujao nisipoona angalau wachezaji 6 wamesepa itakua basi tena,tena sita wale wa first team bila hivyo tutamsindikiza pep miaka nenda rudi.
 
Kama sijakosea,kuna kipindi Onana alikuwa anazurula bila timu kabla Inter hawajamsajili na imewalipa.
Hawa Scouts wa Man Utd sijui huwa wanafanyia wapi kazi zao za kutafuta talents!
Inter milan walifikia makubaliano ya uhamisho wa Onana mwezi january, erik ten hag ametangazwa kuwa kocha ajaye wa manchester united mwezi APRIL.
 
Hata hivyo pamoja na Performance yake timu nzima ya Inter inawachezaji serious sana.

Kikosi kizima cha Inter Milan kuna wachezaji wachache sana Man U wanaweza kusogelea uwezo wa mchezaji mmoja mmoja wa Inter Milan.

Ukimwangalia Denzen Dumfries halafu umlinganishe na Diogo Dalot ni mbingu na ardhi,

Nicolo Barrela huwezi kumweka Daraja la Fred na Mictominay.

Jana Marcelo Brozovic, Acerbi na Damian walitudundisha mtu mzima anatakiwa kufanya nini anapopewa kazi.
Kuna vijana walikuwa wakifanya kazi chafu Baston, Barella, na Hakan watu wenye workrate hii kikosini kwetu ni wanne tu. Bruno, casemiro, Martinez na Bissaka.

Kundi lililobaki ni watu ambao wanatakiwa kusubiri kama mwanaume aliyechoka waende kutoa support.

United inakabiliwa na tatizo la kutofanya usajili sahihi.
 
Hadi sasa hakuna dalili yoyote toka kwa timu yetu.

Kwa madhaifu ya kikosi chetu bila sajili mpya hata 6 tena sio za mkopo na bure sioni tukimalisa hata nafasi zile 7 za juu hata 10 kabisa.

Huu ni ukweli mchungu
Man United wanahitaji Beki mwingine anayeweza kucheza angalau position ya kushoto au kulia.

Injury za Raphael Varane na upuuzi wa Maguire zinatugharimu sana.

The likes of Josko Gvardiol, Milan Skrinniar, Nikola Milinkovic Savic, itakuwa ni boost kubwa sana.

Kwenye midfield tunahitaji atleast two signings the likes of Jacob Ramsey, Mason Mount, Nicolo Barella, watakuwa boost kubwa sana.

Beki wa kulia pia, striker na goal keeper.
 
Ushauri kwa utd
Pia kuna wachezaji wako huru kibao kwa jinsi timu ilivyo wanaweza saidia sana kulinganisha na waliopo kikosini
Kundi kubwa la wachezaji wa United wanapaswa kuwa back up tu na kwa ukubwa wa timu wengi hata hiyo back up role hawastahili.

Ferguson kwenye timu yake asingekuwa nao hawa wachezaji kwenye kikosi chake cha kwanza never.

Wachezaji wazembe hawawezi kukupa makombe
 
Kundi kubwa la wachezaji wa United wanapaswa kuwa back up tu na kwa ukubwa wa timu wengi hata hiyo back up role hawastahili.

Ferguson kwenye timu yake asingekuwa nao hawa wachezaji kwenye kikosi chake cha kwanza never.

Wachezaji wazembe hawawezi kukupa makombe
Japo di maria umri umeenda sidhani kama antony anafikia hata nusu ya uwezo wake kuna kroos modric etc
 
Hata hivyo pamoja na Performance yake timu nzima ya Inter inawachezaji serious sana.

Kikosi kizima cha Inter Milan kuna wachezaji wachache sana Man U wanaweza kusogelea uwezo wa mchezaji mmoja mmoja wa Inter Milan.

Ukimwangalia Denzen Dumfries halafu umlinganishe na Diogo Dalot ni mbingu na ardhi,

Nicolo Barrela huwezi kumweka Daraja la Fred na Mictominay.

Jana Marcelo Brozovic, Acerbi na Damian walitudundisha mtu mzima anatakiwa kufanya nini anapopewa kazi.
Kuna vijana walikuwa wakifanya kazi chafu Baston, Barella, na Hakan watu wenye workrate hii kikosini kwetu ni wanne tu. Bruno, casemiro, Martinez na Bissaka.

Kundi lililobaki ni watu ambao wanatakiwa kusubiri kama mwanaume aliyechoka waende kutoa support.

United inakabiliwa na tatizo la kutofanya usajili sahihi.
Vipi Lukaku mbona haujaleta uchambuzi wake na yeye ?
 
Back
Top Bottom