tatizo kuu linalotukabili hatujui muda sahihi wa kufanya maamuzi yenye maslahi mapana kwa klabu.
mfano:
chini ya ralf rangnick tulishuhudia kupewa muda mwingi wa kucheza anthony elanga, kwa klabu ilio makini ingelihakikisha inamuweka sokoni dirisha lililopita na tungelipata fedha nzuri.
mimi ninayeishi huku unguja upembani nilishamuona anthony elanga hana future njema hapo klabuni, ina maana uongozi wa manchester united wao hawakuliona hilo?
leo hii tunamweka elanga kwa thamani ya paundi millioni 10
liverpool wamemuuza neco williams kwa paundi millioni 17 kwenda nottingham forest.
liverpool wamemuuza harry wilson kwa paundi millioni 14 kwenda Fulham.
liverpool wamemuuza solanke kwa paundi millioni 19 kwenda bournermouth
hawakusita kuwaweka sokoni kwa sababu walishaona hawana mpango nao wa muda mrefu licha uchanga wa umri wao.
walichokifanya wao ni kuwabrand wachezaji wao.
full stop
manchester city walimuuza bazunu kwenda southampton, yaani city wamepata paundi millioni 13 kwa golikipa anayecheza Kikosi B.
MAN CITY hao hao wamemuuza lavia kwenda southampton kwa paundi millioni 15 huku wakiweka kipengele cha kumnunua tena kwa paundi millioni 40, huyu lavia naye alicheza team B.
sisi mpaka leo tunaumiza kichwa juu ya dean henderson, yaani kimasihara masihara tunazikalia paundi millioni 25 hadi 35 kwenye makalio ya carrington.
Team ilio serious haiwezi kumfikiria scott mctominay kwa zaidi ya mara mbili, newcastle united walishaonyesha nia ya kumhitaji lakini klabu inasita kupokea paundi millioni 25 hadi 35 kwa mpuuzi kama yule.
unajiuliza hii klabu ya manchester united inakhofia kitu gani kwa kumpoteza mctominay?
uza mctominay baadae mnunue mathew nunez wa wolves,
umepoteza nini?
tuna safari ndefu sana