Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 21,178
- 37,475
Mkuu mimi nina mtazamo tofauti kidogo.Tunamaliza ligi huku tukiwa tumeshindwa kufikia standard ya manchester city kimpira japo kwa asilimia 60.
Hii ina maana ya kwamba msimu ujao tutaendelea na maisha ya kubana korodani kwa kila mechi tutakayoiangalia.
Huo ni utabiri wangu
Unapotaka kupambana na manchester city, hatua ya kwanza ni kufikia level yake ya kiuchezaji, Arsenal wameikaribia hatua hii.
Tunafanya makosa mengi, mengi, mengi sana tukiwa ndani ya uwanja.
Naamini tumepiga hatua ingawa si nyingi kama tulivyotarajia.
Mzunguko wa pili tulikuwa tunaongelea habari ya ubingwa.Mambo yalianza kwenda ndivyo sivyo baada ya red card ya Casemiro na kuumia kwa Lisandro,Varane & Martial.
Tuna hitaji wachezaji 4 au 5 tu ili tuweze kukimbizana na City.Mlinzi wa kati,Kiungo na mshambuliaji wa kati.Tunaweza kuongeza mlinzi upande wa kulia na mshambuliaji kulia.
Team kwa mara ya kwanza imejitahidi ingawa bado kidogo.Tuna hitaji kuondoa magarasha yote na nafasi zao kuzibwa na wachezaji sahihi.
Tumpatie Mwl muda na zaidi ya yote tushukuru Mungu top four ipo ndani ya uwezo wetu.