Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hii timu mara ya mwisho kutufunga 2008.

Miaka kumi na tano iliyopita.

Mna haki kushangilia draw ya jana.
 
Hii timu mara ya mwisho kutufunga 2008.

Miaka kumi na tano iliyopita.

Mna haki kushangilia draw ya jana.
United kufungwa na Barca siyo kitu cha ajabu lakini kiti anachokaa Barcelona basi pembeni yake yupo United.

Barca ya miaka hiyo unafungwa unakubali kabisa tumezidiwa, mara ya mwisho kabla ya jana tumekuja Camp Nou na kikosi kibovu huku ile Barca yenyewe ikiwa ndiyo inaishia. Hii Barca ya sasa ya kawaida tu kama ilivyo United mpaka tunakutana Europa.

Timu kama Madrid ilikuwa level moja na Barca na United lakini uongozi wa hizi timu mbili ukazipoteza na sasa tunarejea.

Kufungwa na timu bora si ajabu lakini siyo Barcelona hii 😁 njooni Old Trafford tuwape tiketi ya kurudi Spain mpambane na mbio za ubingwa.

Halafu, nani jana kaitafuta droo? 😂
 
Barcelona wameruhusu magoli 7 tu kwenye La liga mpaka sasa..

Tuimprove sana kwa kweli

EtH mwezi wa sita asafishe watu wasiokuwa na umuhimu na azibe magap na watu watakaotufanya tuwe bora zaidi ya hapa.

Martial,Maguire,VdB,Jones,Williams,Tuanzebe,Bailly,McTominay,Elanga,Telles..hawa wote inabidi waondoke klabuni.
 
Kwa timu hipi ya kunifunga?

Una timu mbovu sana.

Wachezaji wazito na wavivu kama wamebebeshwa dunia mgongoni.

Mkipata mpira hata kukaa nao kwa sekunde tano ni mtihani.

Ni utoto tu wa Barca ila ulikua unakufa nyingi.

Timu yenu still inategemea miujiza kushinda na sio uwezo.
 
Sasa mkuu, unaposema "ni utoto tu wa Barca.." si ndio madhaifu yenyewe hayo ambayo hufanya timu zifungwe na watu wabebe makombe? Mpira ni mchezo wa makosa.

Hata MUFC ya Ole ilikuwa timu nzuri ila "ni utoto tu wa akina Pogba na ubishoo ila tulikuwa tubebe makombe."

Hakuna muujiza kwenye mpira, unafanya makosa na unaadhibiwa watu wanabeba makombe. Acha tantalila nyingi, wewe kwa sasa hauna timu ya kutisha. Kunywa maji utulie.

Kumbuka umeitafuta sare kwenye uwanja wako wa nyumbani na hapo ulikuwa unacheza na MUFC ambayo haina Martinez wala Sabitzer.
 
Hongereni kwa ushindi jana nyie manure maan sishani kama kuna team kutoka EPL imeshawi kuondoka na ushindi pale camp nou .Kupata sare ni ushindi mkubwa sana kwenu.
 
Gemu kama ya leo piga nikupigie mara ya mwisho kuiona ilikuwa Fainali mwaka jana Qatar France Vs Argentina ..
Kweli kabisa mm mara ya mwisho kuona mechi kali kama ya jana ilikuwa ni

Wazee fc vs mwandiga fc

Ilikuwa ni fainali ya kombe la Ng'ombe mechi ilitoka sare ya 8:8

Penati hakuna aliyefunga hata moja wakarudia kesho yake mechi ikaisha 11 : 11

Zikapigwa penati kila mtu akakosa ikabidi Ng'ombe ichinjwe wagawane nyama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…