Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Achaneni na mpira wa kujigongagonga njooni kule the blue side of manchester muone mpira wa kikubwa.
 
Hakua mchoyo sana.

Mnaombeza Weigehorst jua mawinga wenyewe hawampi mpira.

Yeye akipata mpira anatoa pasi.

Michezaji ya kuforce kufunga na uchoyo naichukia.

Gemu za ushindi ndio wanatuangusha
Mimi bado nakazia kocha inabidi anunue straika wake mwenyewe awa walipo watamuangusha maana wanataka wafunge wao tu siku wakiwa out of form tumeliwa. Tunahitaji timu icheze kwa ushirika kuanzia nyuma hadi mbele sasa leo dakika zote straika Weighorst hapewi mpira na hili ni tatizo mechi karibu zote.
 
Mie tokea Ile gemu ya mrudiano ya arsenal tuliopoteza, ilikua ni uzembe wa ten hag kushindwa kufanya sub mapema alinikera sana, ijapokua nakubali kuwa kwa Sasa tumebahatika kupata kocha mzuri.

Hii gemu ya Leo asingefanya sub mapema tusingepata ushindi huenda tungefungwa kabisa na hawa Leeds.
Kuna game EtH ametunyima points kwa kutofanya Sub mapema au na kuanza na watu ambao hawana mchango wowote.
 
Back
Top Bottom