Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Aise tuna shida aise eriksen injury na kaonekana jana anatembea na magongo kabisa na hapo kumbuka na DVB naye out hadi mwisho wa msimu.

Tunaitaji kiungo mwingine haraka iwezekanavyo maana hapo kiungo aliyebaki ni fred tu na tuna wimbi la mechi nyingi kweli na hatuna backup ya viungo wa kutosha.

na hatuwezi tena kupata mchezaji mwingine wa mkopo maana mwisho ni wawili tu na tayari tunao.

Tuna wakati mgumu kweli tuombe asiwe amepata majeraha ya muda mrefu maana ratiba yetu ya February tutacheza mechi nyingi kweli hafu wachezaji wameanza kupata injury.

View attachment 2499116
Na mechi zinavyokuja kwa wingi ,mkifika March mtakuwa mnanena kwa lugha
 
Ndani ya miaka miwili thamani ya kijana huyu imefikia paundi millioni 70.

Je kama united ingelimsajili miaka miwili iliopita angeliweza kufikia ubora huu alionao kwa sasa?

Tulikuwa na mazingira bora ya kuweza kukilea kipaji chake?
Ndilo swali ninalojiuliza,
Screenshot_20230129-204811_Chrome.jpg
 
FA
Carabao
EPL
EUROPA

Tuna mechi nyingi mbeleni, tutaweza kuziafford ?

Tayari Ericksen injury,,,,
Inavyoonekana hakuna usajili wowote unaotegemewa hii January,,,,

ikitokea suprise ni bonus kwetu !!

#GGMU
Target msimu huu ni top 4. Kombe lolote hasa hasa Carabao tutakuwa sawa tu. Kikosi kilichopo tunaweza kufikia hayo malengo as long as Casemiro atakuwa fit kwa 100%.

So far, ten Hag ameni-surprise sana sikutarajia kama tungefika hapa. Binafsi sioni haja ya kuingia sokoni tusubiri majira ya kiangazi na ndio muda sahihi kupata wachezaji wazuri. Seasonal projects za timu mbali mbali zinakuwa zimekamilika na inakuwa rahisi wao kuachia wachezaji.

Hapo juu nimemtaja Casemiro kwa ssb ndiye mchezaji pekee ambaye kwa United hatuna mchezaji hata mmoja anaweza ku-cover nafasi yake hata kwa 5% tu. Hao wengine tunaweza kucheza bila wao na timu ika-balance bila shida japo tuta-struggle kidogo.
 
Hivi bayern munich hawawezi kutupa gravenberch kwa njia ya mkopo akaungana na erik ten hag?
View attachment 2500415
Haitakuwa rahisi kwa sasa huyu ni squad player kumbuka Bayern wana UEFA, DFB-Pokal na Bundesliga.

Majira ya kiangazi ndio itakuwa rahisi kumpata maana tayari Bayern wamemalizana na Konrad Laimer kutoka Leipzig.
 
Baada tu ya kusikia kuwa Chelsea na Benefica wamefikia makubaliano ya uuzwaji wa Enzo kwenda Chelsea kwa Euro mil 130, cheki mashabiki wa Arsenal na Man u wanavyoteseka

 
Back
Top Bottom