Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Man u ina matatizo na watu hawataki kuambiwa ukweli
Mwisho wa cku CR7 kasema ukweli ili timu ipone matokeo yake watu wanamshambulia CR 7
Cjui vichwan mwa watu kuna nn? Mtu anajifanya kuijua man u kuliko CR7 mwenyewe
Amesema sawa ni vizuri: Kwanini anasema muda huu ambao yeye mwenyewe hafanyi vizuri kwa nafasi yake?

Ameonesha tabia mbaya zisizofaa kwa wachezaji wenzake hususani kumsema namna ile mwalimu wa timu.
 
Amesema sawa ni vizuri: Kwanini anasema muda huu ambao yeye mwenyewe hafanyi vizuri kwa nafasi yake?

Ameonesha tabia mbaya zisizofaa kwa wachezaji wenzake hususani kumsema namna ile mwalimu wa timu.
Unadhan kuna mtu anaweza kutoboa jipu kama alivyofanya yeye??? Hana cha kupoteza na mwalimu amuheshim C7 mwalimu wa daraja la chini
 
Arsenal waliacha kukumbatia wachezaji wenye Ego na wagomvi kama kina Aubameyang matokeo yake timu inacheza vizuri now na wapo top of the League.

Matatizo ya United yanafahamika lakini sio chanzo asilimia 100 ya sisi kutokufanikiwa..
 
Nilitaka kwenda Man City lakini Sir Alex Ferguson alinipigia na kuniambia sipaswi kwenda City nami sikutaka kumkatalia, nikaufuata moyo wangu na nikarejea Old Trafford.

Nilidhani nitaona vitu tofauti ndani ya United lakini nimeshangaa mambo mengi ni yale yale tangu nilipokuwa nina miaka 20,21,22 teknolojia imebadilika ila United tupo pale pale.

Nahisi kusalitiwa na Man United, kuna baadhi ya watu hawataki niwepo hapa na sio msimu huu tu ni tangu msimu uliopita wanataka niondoke, mimi naiheshimu sana klabu hii na Mashabiki wake.

Sina heshima yoyote kwa Erik Ten Haag kwakuwa yeye haniheshimu, kama wanataka kufanya mabadiliko ikiwemo kuniondosha ni sawa ila wanapaswa kubadili vitu vingi sana ndani ya United.

Sijui kwanini Wayne Rooney ananikosoa sana, pengine kwakuwa bado nacheza muda mrefu tena kwenye ushindani mkubwa kuliko yeye, hilo sifahamu.

- Sehemu ya Interview ya Ronaldo na Piers Morgan ambayo itaanza kuruka Jumanne na Jumatano.
Ronaldo yupo sahihi, toka alipoondoka Ferguson timu haileweki inataka nini, walishayasema Van gaal na Mourinho alichofanya CR7 ni kukazia tu. Timu inahitaji mabadiliko makubwa sana.
 
Nyie watu mnalalama tu bila sababu mmeshindwa jiuliza ni kwanini CR7 amefanya hiyo Interview hasa kipindi hichi tunaelekea kwenye michuano ya kombe la dunia, pia kuna dirisha la usajili hapo Januari. Ni wazi kuwa CR7 yuko tayari kwa lolote lile na inaonekana kaisha pata timu ya kwenda.
 
Cristiano Ronaldo: "Hatuna kocha mi nawambia, siku moja ametukalisha chini na kuanza kutuambia kuwa hana marinda"
 
Cristiano Ronaldo: "Huyo kocha inapaswa aelewe kuwa mimi ni mkubwa kuliko yeye hivyo aniheshimu sana, ndio maana leo hii madogo wengi wako upande wangu maana kila wakifunga wanapiga ile staili yangu mpya ya ushangiliaji"
 
Mtu analipwa £500k p/w..summer hii pia meneja wake alikuwa anapiga simu kwa kila sporting director anayemjua ili amtoe Ronaldo United..Yet Ronaldo anasema anahisi kusalitiwa ..

Achilia mbali drama nyingine alizotufanyia..

I hope ameshapata timu ya kwenda January hii.
Sidhani kama kuna timu yo yote itakayokuwa kumchukua mtu anayejiona wa maana kuliko wenzake wote, na hata kuliko kocha.

Labda Sporting Lisbon alikoanzia!
 
Cristiano Ronaldo: "Kuna siku nimevamiwa na wauaji ila Mwenyezi Mungu akasaidia hawakufanya chochote baada ya kuwabana wale wauaji wakasema wametumwa na kocha eti waje waniue"
 
Ni kwel kwenye uongozi kuna shida , hakuna asiejua,,,,

Ronaldo kaongea upupu Sana eti hamueshimu mwalimu,,,,

Alafu amevizia hakuna match hivi karibuni watu wanaenda world cup ndo akaongea ,,,,

Kingine anataka kutafuta huruma na support kwa Mashabiki waone kwamba ameonewa, mchezaji mkubwa wa caliber yake anakuwaje na vituko Namna hii,,, watoto/vijana Kama kina Alejandro/Anthony wanajifunza Nini toka kwake ?

Ni muendawazimu pekee ndiye atakaekuwa upande wake na kumtetea ,,,

Alianzia ujinga wake pre season, akaja Kuna match moja sikumbuki alitoka kabla muda , akaja ya Spurs, juzi aaambiwa match na Fulham hatoanza lakini atakuwa sehemu ya kikosi, yeye akadanganya anajisikia vibaya kwa hio hakusafiri na wenzie kwenda London,,,

Umri umemtupa, hawezi kufanya alichokuwa anafanya akiwa 20's ama early 30's ,!

Mwisho wa siku hakuna mchezaji aliemkubwa kuliko club never,,,, ! Watakuja wengi na wataondoka, that's all

Timu ipo Salama na kwenye right direction chini ya ETH, apewe muda aweke ideas zake pia apate players anaowahitaji, sio kitu Cha siku moja ,,,msimu huu hatuna Cha kupigania tushinde,,, sana sana tunahitaji kushiriki UEFA mwakani

Chief-Mkwawa Anahesabika Kama legend ? Kwangu Ni Big No, kaiexpose Sana club na dharau kwa mwalimu
Mkuu shida ya United ipo ndani wewe ukimuangalia Ronaldo huhisi kwamba anareact kutokana na anavyotreatiwa United?
 
Time to let him go
20221114_114733.jpg
 
Cristiano Ronaldo: "Mimi sina shida na mashabiki, shida yangu iko kwa kocha maana kuna siku nimemkuta kwa mganga akiniroga"
 
CR7 ni binadamu mbinafsi aliyewahi kutokea ulimwenguni

Kwake kila kitu ni kuhusu yeye, hajali klabu, hajali wachezaji wenzake

Anaamini yeye ni mkubwa kuliko klabu, anaamini anaweza kuishurutisha klabu

Alilazimisha kuondoka kwenye dirisha lililopita, leo anakuja na stori klabuni hawamtaki

Kwa kauli zake anaonesha hakumuheshimu Ragnick, na sasa ana mu undermine Ten Hag kocha anayeijenga timu

Cr7, ni adui namba wa United kwa sasa
 
Man u ina matatizo na watu hawataki kuambiwa ukweli
Mwisho wa cku CR7 kasema ukweli ili timu ipone matokeo yake watu wanamshambulia CR 7
Cjui vichwan mwa watu kuna nn? Mtu anajifanya kuijua man u kuliko CR7 mwenyewe
Hata kama aliyo yaongea ni sawa ila alichoboronga ni hapo kwenye kumlalamikia kocha wake kua hamuheshimu na yeye pia hawezi kumheshimu.
Ngoja tusubirie hio full Interview, maana kipindi cha pre-season aliwalalamikia waandishi wa habari wa Uingereza kua wanamzulia uongo.
 
ETH Anapongezwa kwa sasa ila najua muda si mrefu utamgeuka.umeshaambiwa tatizo la united sio Ronaldo wala ETH tatizo ni viongozi wa hii club hawataki kuwajibu kwa ajili ya future ya club tangu aondoke sir Alex Ferguson mpk leo hakina transformation ndo maana timu inafanya vibaya wamekuja akina pogba, van gal, mourinho,lukaku wote wameondoka wanasema uongozi wa club ni tatizo ndo maana timu haiendi top level leo ameongea Ronaldo tena bado mnabisha mtaendelea kusindikiza watu wanabeba mataji miaka na miaka ndo maana mnaitwa united fans hili swala mlibebe msiweke chuki tu dhidi ya Ronaldo ameongea ukweli hata kama hakutakiwa kuongea
Nimempongeza EtH kwa kuhakikisha nidhamu inakuwepo kwenye timu na timu inakuwa moja bila kujali ukubwa wa mchezaji. Ronaldo alitaka awe mkubwa kuliko Kocha na hilo sio sahihi.

Tatizo la uongozi wa club lipo na linajulikana lakini halihalalishi mchezaji kutokuwa na nidhamu kwa Kocha,wachezaji na timu nzima.

Ronaldo ana mkataba pale kama mchezaji, angetimiza wajibu wake kwanza ndio aanze kiherehere.

Yani kocha yupo huko anajenga nidhamu na roho ya kujituma kwa wachezaji, yeye anahaha kwenye media kumvunja kocha moyo pamoja na wachezaji wenzake? Halafu unasema tatizo la club?

Ronaldo ni mbinafsi, anaangalia Records zake binafsi, hizo ni hasira za kuwekwa bench. Yeye hata kama anajua ni mzigo kwa timu hajali, anataka apangwe tu Records zake zitimie.

Mtu analalamika hata aibu hana, amekuja Cavan anajituma kuliko yeye ila kwa heshìma akavuliwa jezi aķapewa yeye, anataka heshima gani tena?
 
Nimempongeza EtH kwa kuhakikisha nidhamu inakuwepo kwenye timu na timu inakuwa moja bila kujali ukubwa wa mchezaji. Ronaldo alitaka awe mkubwa kuliko Kocha na hilo sio sahihi.

Tatizo la uongozi wa club lipo na linajulikana lakini halihalalishi mchezaji kutokuwa na nidhamu kwa Kocha,wachezaji na timu nzima.

Ronaldo ana mkataba pale kama mchezaji, angetimiza wajibu wake kwanza ndio aanze kiherehere.

Yani kocha yupo huko anajenga nidhamu na roho ya kujituma kwa wachezaji, yeye anahaha kwenye media kumvunja kocha moyo pamoja na wachezaji wenzake? Halafu unasema tatizo la club?

Ronaldo ni mbinafsi, anaangalia Records zake binafsi, hizo ni hasira za kuwekwa bench. Yeye hata kama anajua ni mzigo kwa timu hajali, anataka apangwe tu Records zake zitimie.

Mtu analalamika hata aibu hana, amekuja Cavan anajituma kuliko yeye ila kwa heshìma akavuliwa jezi aķapewa yeye, anataka heshima gani tena?
Mpumbavu huyu, dirisha kubwa alitaka kuondoka ila management ikamkazia ndio maana ameamua kuisagia kunguni kipindi hiki ili dirisha dogo likifunguliwa tu aruhusiwe asepe.
Shida inakuja ni timu gani inayo muhitaji kwa sasa?
Hao mashabiki wanaomtetea humu wakisikia timu yao inataka kumsajili wanaanza kupiga kelele kua hawataki kirusi ndani ya timu yao.
 
Back
Top Bottom