Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hii timu haifai kucheza epl ni bora ishuke daraja tu.
20220813_075205.jpeg
 
Kama ni project mpya niko tayari kabisa wacheze wale vijana wa pre season kila mechi nitavumilia misimu mitatu kuliko hawa wapuuzi.

Ni bora kina savage wacheze tu wapate experience hata tufungwe kila mechi niko tayari kuisubiri hiyo project ila hawa jamaa ni wameshindwa kufanya chochote

wachezaji ambao makocha zaidi ya wa4 wameshindwa kuwacoach unawategemea wa nini.
 
Glazers ni moja ya matatizo ya United. Pesa yote unayoona inanunua wachezaji ni pesa inayotokana na mapato ya timu. On top of that Glazers waliinunua United baada ya kuchukua mkopo na deni lake wakalihamishia kwenye timu. Bado wakaona haitoshi wakaiweka Manchester United kwenye soko la hisa la NYSE, miezi michache nyuma walichukua gawio lao wakaweka mfukoni.

Budget inayowekwa kusajili wachezaji ni pesa timu inayotengeneza na siyo uwekezaji wa Glazers hata senti 5. Wao ndiyo wameweka structure za kusajili wachezaji wenye majina au ushawishi mkubwa ili timu ipate mapato zaidi bila kujali timu inafanya nini uwanjani.

Glazers ni tatizo kubwa sana kwa United walinunua timu ikiwa haina deni hata la sh 1. Sasa hivi wameibebesha mzigo wa madeni na bado wanachukua pesa kutoka kwenye timu, bado pia hawataki kununua wachezaji kwa wakati wanapohitajika pamoja na pesa yote timu inayotengeneza timu ni kwasababu mapato mengi wanachukua wao.

Wanavyoiendesha timu hao Glazers tajiri yoyote anaweza kufanya, Manchester United inajiendesha lakini inahitaji mtu mwenye mapenzi na timu, biashara ni sehemu ya football lakini wanachofanya Glazers ni kuitumia United kwa faida zao binafsi.

Maneno ya Mourinho, van Gaal na Rangnick yataishi milele.
Kwa hiyo mnafungwa kwa sababu timu Ina madeni aliyekwambia kwamba hizo timu nyingine hazina madeni ni nan?

Kuhusu mfumo Siyo nyie mlisema kuwa yule directing manager wenu aondoke na akaondoka kwa kujiuzulu yaan kila kitu mtakachotaka mashabik mnafanyiwa iwe kuondoa mtu au kuleta mtu


Tangopori la Neville umelichukua zimazima bila kulifikiria
 
Huyo cocha sijui atamfunga nani hapo epl kwa mpira wanaocheza Man U,yaani hapo itakuwa kipigo mpaka wamfukuze hapo sijaona mechi ya kushinda huyo hapo epl,

Anauwezo mdogo sana,watu walimpamba tu lakini uwezo hana kabisa huyo epl haiwezi.

Mimi kwa mtazamo Wangu huyo kwa nanmna timu inavyocheza hawezi kushinda mechi yoyote hapo epl narudia tena hawezi kushinda mechi yoyote pale epl .
 
Hivi ni kweli glazer ndo tatizo pale united??

Mbona kama ni hela wamemwaga sana.
Wote hawa tumenunua kwa bei za kutisha.

Maguire

Pogba

Sancho

Shaw

Martinez

Mbona kama ni hela maboss wame mwaga sana pale united maana kazi ya maboss ni kumwaga hela kwa kumwaga hela sisi ni wa pili pale EPL nyuma ya city.

Mimi sioni kama maboss wana tatizo kwenye swala la kumwaga mpunga wametoa hela nyingi sana mpaka tulivunja record ya dunia kwa pogba lakini amna kinacho change.

Tatizo la United linaweza kuwa kubwa kuliko tunavyoona.

Kwaiyo tujiandae tu ndugu zangu ushabiki ni kupenda kitu hata na kwenye shida sio raha tu.

Tukubali tu saizi tumekuwa kama Everton tu tunashiriki ligi ili tufuzu Uefa tu.
Umeongea kwa masikitiko makubwa sana. United kwa sasa mnapitia njia walizopita Liverpool na kina Milan. Mnahitaji muda kujenga timu itakayoweza kushinda na vilabu vikubwa barani ulaya. Na hii inahitaji muda. Lakini ile tabia ya kusainisha makocha afu muda mfupi mnawafukuza hamtaweza kuijenga timu yenu. Kwa mfano, huyu ETH tayari kaja na mfumo wake toka pale ajax. Na anaamini kwa % nyingi mchezaji aliyepitia pale ajax anaweza kumtumia na kupata mafanikio. Ndio maana anawajaza pale.
Mnapaswa kuendelea kumwamini hata kama timu inafanya vibaya, yaani mumpe muda. Angalao miaka 4, kama mafanikio yasipoonekana basi aonyeshwe mlango wa kutokea.

Liverpool wakati wanampa Klopp timu alikuta benteke ndio main striker, Kolo Toure na Momo Sakho ndio mabeki wa kati. Akawaambia kabisa. Makombe yataanza kupatikana ndani ya miaka mi4. Akaanza kuijenga timu. Kawaleta kina Mane, Salah, Alison Beker, Rob, vvd, Fab, kisha akampandisha TAA nk. Akaondoa magarasa kibao. Sakho, benteke, na wengine. Mpaka sasa mchezaji aliyebaki pale klopp aliyemkuta ni captain Heddo na msaidizi babu Milner. Waliobakia ni yeye kawaleta.
Kina Glazer wao wanaangali mkwanja tu. Watulie wamwamini ETH na wampe muda wa kutengeneza timu. Tofauti na hapo mtaendelea kupigwa tu.
 
1660469974483.png

Hawa viparangoto waliofanana kama matofali, akili zao pia zimefanana. Ila united mnajua kuchafua cv za makocha kweli. Conte ndio mtu aliyekuwa anawafaa. Mourinho mlimtimua, akaja Olesendeka mkamtimua. Akaja juke mjerumani akaonyeshwa mlango. Toka 2014 baada ya kustaafu mzee wa brown evelope mmeshaajiri makocha zaidi ya wa5
 
Kwa hiyo mnafungwa kwa sababu timu Ina madeni aliyekwambia kwamba hizo timu nyingine hazina madeni ni nan?

Kuhusu mfumo Siyo nyie mlisema kuwa yule directing manager wenu aondoke na akaondoka kwa kujiuzulu yaan kila kitu mtakachotaka mashabik mnafanyiwa iwe kuondoa mtu au kuleta mtu


Tangopori la Neville umelichukua zimazima bila kulifikiria
Mwanzo kabisa nimeanza kwa kuandika "Glazers ni moja ya matatizo ya United."
 
Glazers ni moja ya matatizo ya United. Pesa yote unayoona inanunua wachezaji ni pesa inayotokana na mapato ya timu. On top of that Glazers waliinunua United baada ya kuchukua mkopo na deni lake wakalihamishia kwenye timu. Bado wakaona haitoshi wakaiweka Manchester United kwenye soko la hisa la NYSE, miezi michache nyuma walichukua gawio lao wakaweka mfukoni.

Budget inayowekwa kusajili wachezaji ni pesa timu inayotengeneza na siyo uwekezaji wa Glazers hata senti 5. Wao ndiyo wameweka structure za kusajili wachezaji wenye majina au ushawishi mkubwa ili timu ipate mapato zaidi bila kujali timu inafanya nini uwanjani.

Glazers ni tatizo kubwa sana kwa United walinunua timu ikiwa haina deni hata la sh 1. Sasa hivi wameibebesha mzigo wa madeni na bado wanachukua pesa kutoka kwenye timu, bado pia hawataki kununua wachezaji kwa wakati wanapohitajika pamoja na pesa yote timu inayotengeneza timu ni kwasababu mapato mengi wanachukua wao.

Wanavyoiendesha timu hao Glazers tajiri yoyote anaweza kufanya, Manchester United inajiendesha lakini inahitaji mtu mwenye mapenzi na timu, biashara ni sehemu ya football lakini wanachofanya Glazers ni kuitumia United kwa faida zao binafsi.

Maneno ya Mourinho, van Gaal na Rangnick yataishi milele.
Mpeni team Yusuph bakharesa
 
Back
Top Bottom