Manchester United (Red Devils) | Special Thread

hujakosea pamoja na bruno
 
Wewe unadhani tatizo kuu ni lipi?
Kuondoka kwa mtu kama Ferguson kwenye timu aliyoitumikia kwa zaidi ya miaka 20 na aliyeweka falsafa zake zilizoota mizizi haliwezi kuwa jambo dogo, ilikuwa ni lazima Man u iyumbe hata kocha angekuwa nani, na ndiyo maana watu wanaojua alama za nyakati kama Pep walikataa kumrithi Fergie co kwamba hawakuwa wanapenda la hasha bali walijua isingekuwa rahisi. Fergie alimpendekeza Pep na walipata kuongea wakiwa USA lkn licha ya kipindi kile Pep kutokuwa na timu lkn aligoma kwa kisingizio eti anapumzika kwanza.

Hii timu tuvumilie tu atakuja wa kutuvusha japo tutatakiwa tubadilike kabisa tuachane na falsafa za Fergie na pia kuna aina fulani ya wachezaji wapo pale inabidi wapewe mkono wa kwaheri, kocha aanze upya na wachezaji anaowataka japo tatizo lingine ninaloliona ni kila kocha anayekuja pale anakwambia ana kikosi kizuri baadaye mambo yanamuendea kombo.
 

Kwani kule si mlimfunga Liver 4 mpaka mkaomba ligi ianze
 
Man U inaweza isiwe na world class players, TRUE. Lakini still kwa hii bunch iliyopo sasa hivi sio ya kupigwa 6 na Brentford & Brighton huku yenyewe ikifunga goli moja tu.

Tuache lazyman's analysis.
Hawajafunga goli hata moja, ilikua ni own goli na brighton
 
Rangnick alivyotangaza kukubali kazi ya Austria nikasema timu inaenda chini zaidi ndiyo maana hata yeye hana imani nayo ameamua kuondoka na ile nafasi ya ushauri haitaki.

Nikajibiwa ushauri atafanya huku anakua kocha Austria. Baada ya siku kadhaa akajiuzulu huo ushauri. So mi narudia tena kusema kwamba timu bado haina project ya maana.

Mashabiki wa United Pogba alisema hawajui mpira. Ni ngumu kidogo kumpinga Pogba kwenye hili hebu kumbuka jinsi mashabiki walikua wanapiga kelele wanahitaji winga na winga ni Sancho.

Sancho amekuja. Ana magoli 3 katika mechi 30. Lakini huwasikii mashabiki wakisema kwamba wanahitaji winga yaani wanazuga kua tatizo la winga limeisha.

Wakaanza leta lawama kwamba wanahitaji DM. Mi ninavyojua Fred ni DM na Scot ni DM, ila mashabiki wanaamini Rabiot ndiyo dawa ya hii ishu. Sasa waulize hao mashabiki kama wamewahi muona Rabiot akicheza.

Rabiot alikua mzuri akiwa PSG, akaenda Juve akawa average, Juve na PSG zipo ligi mbili tofauti yawezekana alishine PSG kwakua PSG ipo farmers league. Akiwa Juve akawa hapangwi akaanza maneno yeye na mama yake wakawa wanaishambulia Juve mitandaoni.

Sasa mchezaji wa tabia hizi akija timu ambayo ipo hovyo tutarajie nini? Sasa jiulize ni kweli mashabiki walihitaji winga au walimhitaji Sancho? Na saa hii ni kweli wanahitaji DM au wanamhitaji Rabiot?

Narudia tena. Shida ya United ni kocha.
 
Mkuu unataka kuniambia hawa brentford wana wachezaji wakali kuliko hao uliowataja? Kwamba utd inahitaji iwe na de jong, Rabiot kuifunga Brentford?
Hii timu imefikia hatua haifundishiki.

Hili ndiyo lililowazi timu zinakuja zikjua kupress tu tayari tunapoteana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…