Castr binafsi niliwahi kutoa hoja humu kuwa sajili nyingi za united ukiziangalia kwa jicho la ndani zinalenga kufanya biashara zaidi kuliko mafanikio ndani ya uwanja. Na uongozi kwa kulitambua hilo wakawa wanaweka malengo ya kucheza champions league badala ya kubeba makombe msimu baada ya msimu. Hii imesababisha wachezaji kuona ni wa thamani sana kibiashara kuliko wanachokitoa uwanjani.
Wachezaji waingereza; Huu mjadala pia umewahi kujadiliwa sana hapa na majukwaa la liverpool na arsenal. Kuna upendeleo mkubwa sana wanafanyiwa hao watoto wa malkia kuanzia gharama za usajili,mishahara yao na nafasi kwenye kikosi cha kwanza kwenye timu. Wakishuka viwango hawaguswi,na pundits wao wanakuwa mstari wa mbele kuwatetea kwa hoja dhaifu sana.
Moyes alishindwa kuwafanya wajitoe kiuchezaji,Ole pia aliwaogopa wachezaji wa aina hii. Van gaal na Mou walikuwa wametambua tatizo la msingi la timu ni attitude ndio maana wakaondolewa kwa zengwe ili hawa wachezaji wapumue. Kinyume na wengine,Ralf anaonyesha ana guts za kulisemea,kukemea na kuwatoa kafara wachezaji wa aina hii ili waliobaki wajue thamani ya timu.
Fikiria kwa nini dakika za mwanzo tunacheza mpira mzuri kwa kufuata maelekezo ya mwalimu lakini baada ya daki 30 tunakuwa vimeo kama vile ni timu mbili tofauti?