Kocha awe mkali kidogo.
Nakumbuka Arsenal aliteta alipochukua kazi na mwenendo wa timu. Seniors players ndio walikua tatizo, malazys hawapambani kisa Mshahara unaingia.
Alipoopt madogo wenye njaa ya kushine, smith rowe, Tierney, Saka, Martinel, Sambi Lokonga, Tominayasu.
Naona timu inaeleweka.
Man U, kocha asiyeangalia jina ndio dawa. Piga wote benchi awe Ronaldo au nani vile, chukua dogo wa academy changanya na seniors walio tayari kujitolea, kina Cavani, Bruno.
Mbona mimi naona Amadi na Elanga wako vizuri upande wa Rashford muhimu kuwapa motisha kuwa wakifanya vizuri Rashford anaoza benchi.
Tofauti na sasa madogo wanaamini ni wa kutumika mechi za kindondo Carabao, huko.
Naaamini huenda tukawa na mwanga, maana hata seniors watajua hawajui, kuwa now hakuna kuchekeana.
Pia naamini hivi;
TIMU YOYOTE INAYOWEZA KUSHINDA MAKOMBE MENGI NA KUWA NA CONSISTENCY NI ILE INAYOTENGENEZA MASTAA na sio INAYONUNUA MASTAA WALIO NA ATTITUDE TAYARI. Cheki man u ya Babu Fergie, ilikua ya kuzalisha mastaa wa kuletea mafanikio akiona unaanza attitude anakupiga bei haijalishi uko on form.
Liverpool icheki, inang'aa kwa kutengeneza mastaa hawasajili mastaa.
Ndio inafanya mishahara midogo output kubwa.
Njoo kwetu, Rashford attitude, Pogba Attitude, Ronaldo Attitude, Bruno huyo attitude, Mason Greenwood (dogo naona akipotea ashajaa upepo toka aanze kuchora tattoo attitude imezidi) bishoo martial attitude, Ukiangalia wachezaji wenye attitude ndio ambao hatuna Sub za kueleweka inakera na ndio wanafanya mambo magumu.
Cheki Donny yuko positive ( hadi huruma)
Amadi yuko positive ( hana attitude si mliona aliomba msamaha kwa kukosa chances, Rashford na Martial walituomba lini).
Ifike muda Tupige bei wote wenye attitude tuwe tunaleta chipukizi wenye njaa waliotayari kufia nembo.
Bruno naona kakata tamaa na attitude nyingi kaona liwalo na liwe.