Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ningelikuwa nipo ndani ya bodi ya klabu ningelipendekeza ralf rangnick apewe kandarasi ya miaka miwili akiwa kama kocha mkuu na si mshauri wa klabu kama mkataba wa sasa unavyozungumza, na hii ni kwa sababu bado siamini ya kwamba nafasi yake ya ushauri itampa nguvu sawa ya kumsimamia na kuhoji maamuzi ya kocha mkuu ajaye kiundani na uwazi zaidi.

mungu wa mpira ametuletea nabii wa mpira ndani ya timu atakayeweza kutuongoza kuelekea njia sahihi baada ya kupotea kwa muda mrefu bila ya kujua ni ipi njia sahihi tunayopaswa kuifuata hivyo tusije kuipoteza fursa hii na kuendelea kuichagua njia ile ile iliokwisha tukwamisha.

pia mashabiki, legends na viongozi waandamizi wa klabu wanapaswa wavisafishe vichwa vyao ambavyo bado vimebeba fikra za kizamani zinazowafanya wajione bado tuna timu bora, bado tuna timu yenye uwezo wa kuleta ushindani dhidi ya wengine na vile vile bado tuna timu yenye wachezaji bora kama wengineo (kama vile man city, liverpool, bayern munich, real madrid na chelsea) na kuziendeleza fikra hizo zinazobebwa zaidi na historia yetu ni kuendelea kujidanganya na kuifuata njia ya motoni ambayo tumeshaanza kuifuata.

Hatua walioamua kuianza Arsenal na hata Barcelona ndio tunapaswa na sisi tuifuate bila ya kujali ni kipi kinazungumzwa au kufanywa na majirani zetu (man city, liverpool, chelsea) kwa sababu wao tayari wameshatutangulia na kutuacha kwa hatua kubwa. Laiti kama ingelikuwa kanuni ya time travelling inafanya kazi halafu ukawauliza viongozi wa arsenal baada ya kusafiri na muda kwa kurudi nyuma hadi 2018.

" hivi tumsajili pepe kwa paundi millioni 80 au tumsubirie bukayo saka huyu mwenye miaka 17, bila ya shaka jawabu litakalotoka vinywani mwao ni la kumsubiria bukayo saka kwa sababu tayari wameshamuona anachokifanya mwaka 2021 ni bora zaidi kuliko kitakachofanywa na pepe"

ralf rangnick aliwahi kusema : ni bora usisajili kabisa kuliko kusajili mchezaji ambaye si sahihi.
liverpool wamekuwa wakiitumia kanuni hii licha ya kwamba klopp baadhi ya nyakati anabanwa na kikwazo cha bajeti ya kutimiza mahitaji yake hatimaye hujifichia hapo.

Arsenal nao wameanza kuitumia kanunii hii na wanakwenda vizuri huku wakisafisha takataka zinazobeba mishahara mizuri huku work rate ikiwa ni ndogo na hata Barcelona nao wanaelekea kuitumia njia hii.

Rangnick ndiye mwanadamu pekee aliyebaki kwenye ulimwengu wa soka mwenye uwezo wa kutusafishia hawa wahuni na washenzi waliotamalaki ndani ya kikosi cha manchester united na kuleta wachezaji watakaoendana na falsafa zake, si guardiola, klopp wala arteta anayepatikana sokoni kama tutaweza kumchukua msimu ujao.

Nimemtaja Arteta si kwa sababu ya ubora wake bali ni ule ukakamavu wake wa kusimama kama bosi ndani ya klabu na ni suala la muda tu kabla hajamuonyesha mlango wa kutokea pierre aubameyang ili kuwaonyesha wachezaji wengineo ukuu wake kwa mara nyengine (alishafanya hivyo kwa mesut ozil, amemweka benchi kipa namba 1 kwa nusu msimu).

Rangnick ni mjeuri na muelewa wa mpira wa kileo kuliko mourinho, ni suala la muda tu kabla hatujashuhudia vita vya mwanaume na vijanadume vinavyokula mshahara wa paundi laki 2 huku wakiingia uwanjani wanapoteza possession mara 120 kwa dakika 90.

mara hii itakuwa ni kazi ya bodi ya klabu kuchagua upande
 
Quite worrying that siku chache chini ya Ralf amekuwa akirejea kuzungumzia jinsi tulivyo wa ovyo mentally and physically. This will be a long old season.

kwa hali hii tutaweza kucheza mechi mbili dhidi ya atletico madrid.
Ole alikuwa anafundisha nini.
 
kipindi kile mourinho anataka kumuondoa anthony martial na kumleta kizee ivan perisic wengi wetu hatukumuelewa.
leo mjinga yule bado anaendelea kututafuna, eti martial analipwa paundi laki 2.
kuna mwengine anaitwa pogba anataka kulipwa paundi laki 5.
Rangnick tuondolee hawa wahuni
 
✓Bruno Fernandes hajali anymore..

✓Maguire afadhali Jones*

✓McFred..Poor midfield combo in the history of our team as far as i can rembember.

✓Rashford==Trashford
nakuhakikishia chini ya ralf hao wahuni watachagua njia sahihi, atawafyekelea mbali pindi wasipobadilika.
ralf apewe kandarasi ya miaka 2
 
Ralph Rangnick tuondolee wahuni
  1. anthony martial
  2. nemanja matic
  3. juan mata
  4. wan bissaka
  5. edison cavani - injury prone
  6. bruno fernandez - karipio kali ili abadilike
  7. eric bailly
  8. scott na fred - wawe wachezaji wa hakiba
  9. jesse lingard
  10. dean henderson -
Mkuu kwenye hii orodha ongeza mtu anaitwa Rashford. Huyu jamaa alichojaaliwa ni spidi tu ila akili ya end product ni zero kabisa. Cavani ni injury prone sawa lakini anakupa vitu vingi sana kwenye hizo mechi chache atakazokuwa timamu kuliko Rashford ambaye hajui aufanyie nini mpira ukifika miguuni mwake.
 
Mkuu kwenye hii orodha ongeza mtu anaitwa Rashford. Huyu jamaa alichojaaliwa ni spidi tu ila akili ya end product ni zero kabisa. Cavani ni injury prone sawa lakini anakupa vitu vingi sana kwenye hizo mechi chache atakazokuwa timamu kuliko Rashford ambaye hajui aufanyie nini mpira ukifika miguuni mwake.
huyo mpuuzi akiendelea na performance hii mpaka february itabidi nimweke kwenye hiyo list, kwa sasa kisingizio chake kinaweza kuwa ni match fitness baada ya kufanyiwa upasuaji wa bega.

kuhusu cavani umri wake na afya yake havikubaliani tena na mradi mpya, ni bora tuwekeze kwengine
 
Hii ndio Gen Gen Dressing
tapatalk_1640700373988.jpeg
 
Victor Lindelof tested positive for COVID-19 yesterday, Rangnick tells Sky
Kabla sijasikia press ya Ralf kuhusu Lindelof nilianza kujiuliza kama kweli ni mtu sahihi pia kwa kumuacha nje Lindelof na kumuanzisha Varane aliyetoka majeruhi pamoja na Maguire asiye na ubora kwa sasa.

Lakini bado napata shida kuamini kama itatokea Maguire akampisha Lindelof pindi akiwa timamu wa afya. Kwa mtizamo wangu mimi captain wetu anatakiwa apewe muda bench ajiulize maswali magumu kuhusu uwezo wake kabla Ralf hajamuonyesha mlango wa kutokea.
 
Kabla sijasikia press ya Ralf kuhusu Lindelof nilianza kujiuliza kama kweli ni mtu sahihi pia kwa kumuacha nje Lindelof na kumuanzisha Varane aliyetoka majeruhi pamoja na Maguire asiye na ubora kwa sasa.

Lakini bado napata shida kuamini kama itatokea Maguire akampisha Lindelof pindi akiwa timamu wa afya. Kwa mtizamo wangu mimi captain wetu anatakiwa apewe muda bench ajiulize maswali magumu kuhusu uwezo wake kabla Ralf hajamuonyesha mlango wa kutokea.
hata mimi nalisubiria hilo swala, sijamuona beki mwenye uwezo wa kumweka nje lindeloff pale.
kuna nyakati jana alikuwa anadelays mpaka ikawa chukizo.
 
Kocha atalaumiwa bure, average players.
Hata Spurs alikuwa na AVG players alipokuja Conte sasa hivi sio avg player tena. 90% ya timu kufanya vizuri ni kocha, aproch ya kocha kuanzia kwenye mazoezi, dressing room, mawasiliano na timu na mchezaji mmoja mmoja na wawapo uwanjani with or wthout the ball ina matter sana
 
Ralph Rangnick tuondolee wahuni
  1. anthony martial
  2. nemanja matic
  3. juan mata
  4. wan bissaka
  5. edison cavani - injury prone
  6. bruno fernandez - karipio kali ili abadilike
  7. eric bailly
  8. scott na fred - wawe wachezaji wa hakiba
  9. jesse lingard
  10. dean henderson -
Abaki nani sasa, Degea na Maguire, Ronaldo?
 
huyo mpuuzi akiendelea na performance hii mpaka february itabidi nimweke kwenye hiyo list, kwa sasa kisingizio chake kinaweza kuwa ni match fitness baada ya kufanyiwa upasuaji wa bega.

kuhusu cavani umri wake na afya yake havikubaliani tena na mradi mpya, ni bora tuwekeze kwengine
Hapo kwa Cavan nilikuwa naongelea kwa muda na hali ya kikosi tulichonacho kwa sasa.

Tukirudi nyuma kwa jinsi United wanavyocheza,unashindwa kujua rebuild ya Ole ilipatia eneo gani hasa katika usajili,mbinu,mifumo,na falsafa zake. Kiukweli tunapata shida kujua kama alitujenga au ametubomoa kwa jinsi hali ya kikosi ilivyo chini sana hadi sasa kama vile tumerogwa!

Naunga mkono hoja tuanze upya chini ya Ralf au mwalimu mwingine yeyote yule ilimradi awe na uwezo wa kutuvusha na jinamizi hili.
 
Tukirudi nyuma kwa jinsi United wanavyocheza,unashindwa kujua rebuild ya Ole ilipatia eneo gani hasa katika usajili,mbinu,mifumo,na falsafa zake. Kiukweli tunapata shida kujua kama alitujenga au ametubomoa kwa jinsi hali ya kikosi ilivyo chini sana hadi sasa kama vile tumerogwa!
Ole aliamini zaidi watu kuliko structure, huyu wa sasa anaamini structure.
 
Kwa hii ON/OFF ya Fred,naanza kupata shida kama kweli anastahili kuwa mchezaji wa kikosi cha kwanza pale United. Jana kabla sijamuona MC,hadi nikashangaa anavyoshindwa kupiga pasi ya mita 3-4 akiwa huru kabisa!
 
Back
Top Bottom