hii hoja ya kusajili wachezaji kwa kuangalia zaidi upande wa kibiashara kuliko uwanjani wengi wetu hatuna uthibitisho wa dai hilo(tumekuwa tukizungumza tu ili kusongesha siku), kwa mtazamo wangu changamoto kubwa zinazotukabili mara kwa mara lifikapo dirisha la usajili ni:-
- kusajili mchezaji ambaye si hitaji kuu la mwalimu, tumeona wakati wa utawala wa mourinho alihitaji kwanza mlinzi wa kati lakini akaletewa kiungo (Fred) ambaye hawezi kutimiza majukumu yake ipasavyo bila ya kuwa na safu bora ya ulinzi.
- kushindwa kusajili target lengwa za makocha, kwa mfano hili litokezea wakati wa utawala wa van gaal na hata david moyes (kocha anataka mchezaji A lakini analetewa mchezaji wa kundi C)
- kurukia rukia wachezaji bila ya kuangalia direction yetu ya kiuchezaji, mfano rejea usajili wa juan mata na aina yake ya uchezaji jinsi isivyoendana na style ya kocha aliemsajili
- kudelay kufanya maamuzi (ukisikia stori za nyuma ya pazia jinsi tulivyowakosa baadhi ya wachezaji utashangaa)
- baadhi ya wachezaji tunauziwa ghali kwa sababu ya kukosa mipango bora ya kushawishi target nyenginezo.
mpaka bodi imefikia hatua ya kukubaliana na matakwa yake bila ya shaka hatutashuhudia upishanaji wa kauli kwenye suala zima la usimamiaji wa klabu ndani ya uwanja, kama kutatokezea sintofahamu kati yao namuona Rangnick akiondoka klabuni (jamaa ni mtu wa misimamo na kwa hilo waulize chelsea wali[omtaka msimu uliopita aliwajibu nini)
Ralf rangnick hajawahi kufanya kazi katika timu yenye budget kubwa mfano wa manchester united, kwa mukhtadha huo haitokuwa rahisi kuweza kumuhukumu. Imani yangu atayafanikisha zaidi ya yale aliyoyafanya akiwa kwenye timu zenye bajeti ndogo kwa kusajili na kushauri aina ya wachezaji wanaoendana na hicho anachotaka kukijenga.
kwa mfano leo nimeona tetesi za kiungo anayeitwa
amadou haidara kutoka leipzig, release clause yake ni paundi millioni 33 hivyo klabu imeamua kumfuatilia mwishoni mwa wiki hii.
sidhani kama aliwahi kusajili mchezaji mwenye gharama kubwa mfano wa hiyo, kama atafiti philosophy yake sidhani kama ni tatizo kwetu na kwake.
kwa ufupi rangnick amepewa nafasi adhimu ya kuuonyesha ulimwengu wa wapenda soka yeye ni mwanadamu wa aina gani, Je ni mtu special kama anavyosifiwa na wanafunzi wake na nchi nzima ya ujerumani au ni mbabaishaji anayejificha nyuma ya mafanikio ya wanafunzi wake?