Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu Pedro Goncalves siyo level ya Rashford hata kidogo.

Tunamunderate sana Rashford katika kikosi chetu lakini Rashford ana impact kubwa kikosini sawa na Bruno.

Msimu uliopita Rashford alihusika katika nusu ya magoli tuliyofunga.
Msimu huu kukosekana kwake mwanzo wa ligi limekuwa pigo kubwa sana tumeishia kustruggle kuvizia magoli ya tap ins.

Kama huwa unaangalia uwepo wa Rashford huwa unatengeneza space kubwa sana kwa Bruno kufunga na kutengeneza chances.

Katika assist tatu alizotoa Lindelof msimu huu mbili alifunga Rashford.

Kuingia kwa Rashford game yetu na Villa Real ilikuwa advantage kubwa sana kwa Ronaldo na Sancho pembeni timu nzima ya Villa real ilihamia kushoto kupambana imminent danger ( Rashford).
 
Dah
We jamaa, kwaiyo maguire kichwa kikubwa akili kisoda, ila man utd pale tulipigwa pakubwa bora hata tungemchukua Coulibary wa Napoli
 
Huyo Pedro Goncalves ni mtu na nusu Ana njaa hatari, alafu pesa yake ya kawaida tu anachukulika
 
Hahaa umenikumbusha Mo Salah aliposajiliwa L'pool usajili wake ulipigwa vita sana kwamba ali-flop EPL iweje Klopp amrejeshe? Pedro hajawahi kucheza mechi yoyote ile ya EPL akiwa Wolves. Aliomba kuondoka mwenyewe msimu wake wa kwanza Ureno alikuwa mchezaji bora wa ligi kijana, maana yake kuna sbb za msingi zilimfanya asiwe anacheza Wolves.

Pedro kawaongoza Sporting Lisbon kubeba ubingwa wa ureno tokea mwaka 2002 zaidi ya miaka 19 akiwa top scorer wa timu na ligi nzima ya ureno. Alifunga magoli 23 kati ya magoli 65 ya Sporting Lisbon msimu uliopita. Misimu miwili mfululizo amekuwa mchezaji bora kijana wa ligi ya Ureno.

Msimu huu japokuwa alikuwa nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi miwili bado ni kinara wa ufungaji wa Sporting Lisbon ana goli 11 kati ya michezo 14 aliyocheza. UEFA ana goli 4 kati mechi 3 alizocheza, hakucheza mechi mbili za mwanzo ambazo Sporting walifungwa zote. Juzi kawaongoza Sporting kuwavuruga Dortmund alifunga goli 2.

Ukimfuatilia vizuri huyu dogo Rashford hamfikii hata nusu ya uwezo wake ni vile haimbwi na vyombo vya habari.
 
Nadhani team inahitaji marekebisho madogo.

Mosi,tunahitaji kuwaondoa wachezaji wasio na tija.
1. Jones
2. Mata
3. Matic
4. Martial
5. Pogba
6. Cavani
Pili,tunahitaji kusajili wachezaji wa kiwango cha juu katika nafasi za Mlinzi wa kati,mlinzi pembeni kulia,kiungo mlinzi na mshambuliaji kazi imeisha.
 
hujielewi, umetoka huko ulikotoka na kukutupukia hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…