Manchester United (Red Devils) | Special Thread

mara zote mbili mou alizochukua UEFA kabeba na timu zenye vikosi dhaifu (porto na Inter), na amefeli na Man u, chelsea na Madrid, hivyo hela sio kigezo sana kwake kama mnavyofikiri bali aina ya wachezaji.
chief, hapo kwenye udhaifu wa vikosi umeegemea kwenye eneo la matumizi ya kifedha au viwango vya wachezaji husika aliowafundisha?
hii ndio list ya wachezaji wa Inter milan waliocheza takribani mechi 20 za msimu wa 2009/2010.
wenye wino mwekundu wamesajiliwa na jose mourinho

julio cesar, ivan cordoba, zanetti, matterazzi, walter samuel, lucio, maicon, chivu, stancovic, sneijder, muntari, stankovic, cambiasso, vieira patrick, etoo, millito, pandev, ballotelli na thiago motta.

kumradhi kwa mfano nitakao utoa:
laiti kama hao wachezaji wangelikuwa wanajishughulisha na sanaa ya maigizo ya pornography huku jinsia zao zingelikuwa na za upande wa kike bila ya shaka wangeliitwa Milfs, kwa maana ya kwamba ni jamii ya watu wenye uzoefu mkubwa sana na kazi wazifanyazo kwa muda mrefu kwenye hiyo tasnia bila ya kusahau wastani wa umri wao unaakisi sifa hiyo (wengi wao walivuka miaka 27).

kwa mtazamo wangu Jose hakukutana na kundi la wachezaji dhaifu bali alikutana na kundi la wachezaji waelewa, waliokubali kwa pamoja kumuelewa jose kwa kile anachofundisha na anachokisimamia, pia naye jose alikubali kuzielewa hisia na firka za wachezaji wake anaowasimamia na bahati njema zaidi wengi wao waliendana kwa urahisi na mfumo wa ufundishaji wa jose (kama angelikuwa guardiola na system yake naamini angelishindwa kwa kundi hilo).

hao jamaa tayari walishakuwa na sura, fikra na mioyo ya mapambano takribani wote ila walikosa mtu sahihi wa kulainisha mashine za viungo vyao na ndio maana wakaonekana dhaifu, alipoondoka jose ule ugonjwa ukawarudia tena.

Pale real madrid alishindwa kuchukua champions league ni kwa sababu ya kudra tu za maulana (hususani ule msimu aliovunja rekodi kibao pale la liga yeye na timu yake) na si kwa sababu ya ufinyu wa kikosi au ulegevu wa wachezaji wake.
 
hii Man city ya sasa hivi ilivyo moto, halafu unasikia mtu anakwambia Ole hana mbinu, mumemuona kocha wenu Pochetino? wamepigwa na 0 short on target. pengine na ligi wasibebe.
  1. mechi ya guardiola dhidi ya Ole usiweke suluhu kwenye mkeka wako
  2. zikiwa mechi mbili kila mmoja ana uwezo wa kumfunga mwenzake au Guardiola kuambulia suluhu mechi moja
  3. ikiwa ni mechi moja ni rahisi kwa Ole kupoteza
ndio niliojifunza kwa miaka hii miwili
 
Guardiola anatufunga carabao tu, kwenye league mechi zote anakaa kajitahidi msimu huu kapata draw 0-0 kwenye misimu hii miwili ole kama Kocha permanent wa utd, mechi 4 tumemfunga 3 katoa draw 1 hajatufunga.


Na mimi comment yangu haikulenga matokeo, Bali tulivyo nullify mfumo wake.

Mpaka February 2021 Cancelo alikuwa ni Contender wa mchezaji bora Epl msimu huu, sehemu nyingi akimwagiwa Sifa kedekede kama Full back anae occupy nafasi mbili kiungo na Fullback muda wote,

Mechi yetu ya juzi ole na Shaw waka onyesha udhaifu mkubwa wa mfumo wa Pep, Yule Cancelo shaw anakaa nae karibu pale pale kwenye chaki ya katikati ya uwanja, Henderson aliporusha mpira kwa shaw na shaw akamt0ka Cancelo, moja kwa moja uwanja ukawa mweupeee, hakuna mtu akaenda moja kwa moja move ile ikatupa Goli la pili.

Mechi iliofuatia Cancelo akakalishwa benchi, mechi inayofuatia tena na leeds wakaiga mfumo wetu ule ule kaangalie magoli ya leeds yote yalitoka upande wa Cancelo, toka hapo mechi kubwa Cancelo benchi linamhusu.

Kama umeangalia jana VS psg zichenko alikuwa ni Key, Pochettino hakufanya Homework yake kivipi Ole aliwazuia City, am florenzi alijiamini sana sijui, lakini kifupi walishindwa kuzuia full back inayo cheza kama Midfield jana na ku concede goli mapema tu.
 
Of course matumizi ya kifedhi ndani ya miaka 2 alitumia 140M ambayo ni average 70m kwa msimu, hiki kiasi Roma wanakimudu japo soko la sasa hivi ni kubwa.

Wachezaji wengi aliosajili walikuwa ni reject ama Ambao wapo timu ndogo.

Mfano Millito Katoka Genoa, Muntari ports mouth, Motta Genoa etc, na wengine Reject kina Lucio, Etoo na Sneidjer etc.
-Millito hakuwahi kuwa 20 goal striker kumbukumbu zangu kama zipo sahihi ila misimu miwili kafunga zaidi ya 20 goal
-Sneidjer Hajawahi kuwa na kiwango kama cha Inter

Hivyo mkuu MOU Ana uwezo wa kuwa fanya wawe competitive wakiwa Serious.
 
Liverpool’s Premier League fixture with Manchester United at Old Trafford has been rescheduled for Thursday May 13.


The game will kick off at 8.15pm BST and be broadcast live on Sky Sports.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…