D A E M U S H I N
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 22,633
- 121,022
chief, hapo kwenye udhaifu wa vikosi umeegemea kwenye eneo la matumizi ya kifedha au viwango vya wachezaji husika aliowafundisha?mara zote mbili mou alizochukua UEFA kabeba na timu zenye vikosi dhaifu (porto na Inter), na amefeli na Man u, chelsea na Madrid, hivyo hela sio kigezo sana kwake kama mnavyofikiri bali aina ya wachezaji.
hii ndio list ya wachezaji wa Inter milan waliocheza takribani mechi 20 za msimu wa 2009/2010.
wenye wino mwekundu wamesajiliwa na jose mourinho
julio cesar, ivan cordoba, zanetti, matterazzi, walter samuel, lucio, maicon, chivu, stancovic, sneijder, muntari, stankovic, cambiasso, vieira patrick, etoo, millito, pandev, ballotelli na thiago motta.
kumradhi kwa mfano nitakao utoa:
laiti kama hao wachezaji wangelikuwa wanajishughulisha na sanaa ya maigizo ya pornography huku jinsia zao zingelikuwa na za upande wa kike bila ya shaka wangeliitwa Milfs, kwa maana ya kwamba ni jamii ya watu wenye uzoefu mkubwa sana na kazi wazifanyazo kwa muda mrefu kwenye hiyo tasnia bila ya kusahau wastani wa umri wao unaakisi sifa hiyo (wengi wao walivuka miaka 27).
kwa mtazamo wangu Jose hakukutana na kundi la wachezaji dhaifu bali alikutana na kundi la wachezaji waelewa, waliokubali kwa pamoja kumuelewa jose kwa kile anachofundisha na anachokisimamia, pia naye jose alikubali kuzielewa hisia na firka za wachezaji wake anaowasimamia na bahati njema zaidi wengi wao waliendana kwa urahisi na mfumo wa ufundishaji wa jose (kama angelikuwa guardiola na system yake naamini angelishindwa kwa kundi hilo).
hao jamaa tayari walishakuwa na sura, fikra na mioyo ya mapambano takribani wote ila walikosa mtu sahihi wa kulainisha mashine za viungo vyao na ndio maana wakaonekana dhaifu, alipoondoka jose ule ugonjwa ukawarudia tena.
Pale real madrid alishindwa kuchukua champions league ni kwa sababu ya kudra tu za maulana (hususani ule msimu aliovunja rekodi kibao pale la liga yeye na timu yake) na si kwa sababu ya ufinyu wa kikosi au ulegevu wa wachezaji wake.