Kuna wadau wanasema timu yetu inacheza kwa uoga against big teams hasa ukizingatia matokeo yetu dhidi ya timu hizo siyo ya kuridhisha kabisa.
Binafsi nina maoni tofauti kidogo juu ya hilo.
Ukiangalia timu yetu msimu huu karibu mechi zote tunatumia mfumo wa 4 2 3 1 au 4 4 2 diamond dhidi ya timu zote kubwa na ndogo.
Msimu uliopita tulicheza 4 2 3 1 dhidi ya timu ndogo na 3 4 2 1 dhidi ya timu kubwa ukiondoa mechi ya Liverpool pale Anfield tuliyocheza karibu mifumo yote uwanjani katika vipindi tofauti tofauti.
Kwanini tumeshindwa kuzifunga timu kubwa tukiwa na timu bora kuliko msimu uliopita ?
Binafsi naona kuna sababu kadhaa.
1. Safu yetu ya ushambuliaji kutokuwa clinical sana msimu huu kuliko msimu uliopita msimu huu tumetengeneza chances nyingi za kufunga magoli lakini tunatumia chache sana kupata magoli ilihali msimu uliopita washambuliaji wetu walitumia nafasi chache sana kutupa matokeo kwa sababu wote walikuwa form pamoja na kukabiliwa na majeraha.
2. Msimu huu timu nyingi kubwa zinacheza kwa tahadhari kubwa sana against United kiasi cha kutokushambulia carelessly kama msimu uliopita unaweza kuona mechi zetu zote against top teams tumepata goalless draw isipokuwa mechi na Arsenal OT na mechi dhidi ya Tottenham OT zingine zote ni goalless draw.
3. Counter attacking football ya Ole kushindwa kufanya kazi hasa ukizingatia sababu zangu mbili hapo juu ambayo ndiyo iliyomuua Guardiola mechi tatu mfululizo, unaweza kuona Man city waliamua kucheza 4 2 3 1 against United OT, Arsenal walicheza mfumo ule ule, na hawakushambulia kwa kujiachia ili wadhibiti mikimbio ya washambuliaji wetu.
Je Ole anacheza kiuoga dhidi ya timu kubwa ?
Jibu ni hapana msimu huu Ole anacheza na timu kubwa kwa kujiamini zaidi kuliko msimu uliopita.
Unaweza kuona katika mechi zote kubwa Ole katumia 4 2 3 1 au 4 4 2 diamond tofauti na msimu uliopita ambao alitumia 3 4 2 1 au 4 3 2 1mifumo ambayo ni completely defensive ukilinganisha na 4 2 3 1 au 4 4 2.
Ukiangalia possession ya Ole katika big games msimu huu na uliopita inaonyesha wazi msimu huu umiliki wa mpira umeongezeka tofauti na msimu uliopita against big teams.
Hata ukiangalia attempts on goal au chances created against big teams msimu huu zimeongezeka kuliko msimu uliopita.
Tumeshindwa kuzifunga timu kubwa siyo kwa sababu ya uoga wa Ole bali kwa sababu ya kushuka kiwango kwa safu yetu ya ushambuliaji na sababu zingine nilizoorodhesha pale juu.
Nawasubiri Southampton .