Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Shaw anapandisha timu lakini akifika maeneo ya hatari hata AWB ana afadhali..Poor poor deliveries..Mipira yote inablockiwa..Telles majalo zake nzuri sana,zote anazishusha ndani ya boksi
Shaw hatulii siku hizi
 
Shaw anapandisha timu lakini akifika maeneo ya hatari hata AWB ana afadhali..Poor poor deliveries..Mipira yote inablockiwa..Telles majalo zake nzuri sana,zote anazishusha ndani ya boksi
Mechi ijayo tunakuanzisha wewe ukapandishe mashambulizi
 
Jana insta kulikua na kumfananisha Bruno na Kimmich.

Katika game 48 Bruno ana assisst 16. Katika hizo game 48 Kimmich ana assisst 21. Bruno ni kiungo mshambuliaji na Kimmich ni kiungo mkabaji.

So kwenye karatasi inatakiwa imaanishe Kimmich anaweza kazi ya kuwalisha washambuliaji kuliko Bruno ila katika uhalisia inakuja hivi Kimmich anampa pasi Lewandoski, Muller au Gnabry wote hawa ni clinical finishers halafu Fernandes anampa pasi Rashford, Martial, Greenwood au Ighalo.

Bruno angekua Bayern angekua na assisst zaidi ya Kimmich simply kwakua ukimpa Lewandowski pasi 5 anaweza akakosa moja au mbili. Rashford ukimpa pasi tano anaweza akakosa zote.

Same ilikua kwa Ronaldo msimu uliopita wakasema ni mbovu kwa assisst na yeye ilikua hivi hivi, ukicheki game unaona anatoa pasi ila watu wa kufunga ndiyo hakuna.

Ile post ilimkosea heshima Bruno.
mkuu huyu Joshua Kimmich hawajakosea hata kidogo kumfananisha na fundi Bruno mi naona wote ni wachezaji bora isipokuwa kila mmoja kuna anachomzidi mwenzake,kwangu mimi kiungo bora kwasasa ni Bruno ila ukiwa na Kimmich anakupa zaidi ya kile unachohitaji coz anaweza kucheza nafasi nyingi kwa ufanisi zaidi ya mchezaji yeyote duniani.
 
Back
Top Bottom