Huu mfano wa Simba tupo sawa kabisa mkuu mpaka darasa ....kipindi hicho cha darasa la tano kila wakati wa mapumziko chandimu kilikuwa kinapigwa kati ya Simba na Yanga Kwa wale wa darasa letu Tu....
nilikua napenda Sana mpira lakini kutokana na Wana Yanga kua wengi Sana nikawa sipati namba (kipindi sina upenzi wowote hapo ila mi shida yangu nicheze mpira) sasa hawa Wana simba walikua wanapelea pelea kwahiyo nikawa napata namba sana Simba.... ushindani,ubishi, na kutokubali kushindwa iwe uwanjani ama class nikajikuta ni mtetezi wa simba kweli kweli

baadae nkawa mtazamaji wa Simba na Yanga huku nikiwa na marafiki wale wale ambao wengi wakawa tukifungwa wakati mechi inaendelea wananizomea mno ....na mimi nikawa sikubali ...goli likisawazishwa namimi nakinukisha ....baadae nikajikuta automatically mwana Simba...
huku Kwa Manchester sina historia kiivyo sababu za kimazingira tu (hasa marafiki zangu kipindi nakua almost 80% walikua ni manutd fans) zilinifanya niwe naangalia manutd pia na kwakua napenda amsha amsha za kimpira nikajikuta tu niliwepo mahali watajua tu hapa manutd fan yupo....
japo utoton nlikua napenda sana kuwaangalia Chelsea akina drogba, kalou, malouda, cech, bosingwa, Alex,lampard, anelka, Terry, Torres , shevishenko etc ndo timu ya Kwanza kua naifuatilia sema kutokana na utopolo walokua wanacheza sometimes wakantia hasira nkaacha kuwaangalia (kuchungulia maana nlikua sina pesa kipindi hicho) nkaja jikuta ni AIG ,AON ...Kwa kina CR7, Rooney, Luis Nani na wengineo.