Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Fan wa man utd tuwe wawazi,kadri siku zinavyoenda tunaimprove kwakweli,tusiwe watu wa kupooonda, chelsea sio timu ndogo,leo angalau tunaonesha mwelekeo.
Tunahitaj game kama hizi ili kutujaza confidence,pale katikati leo palikua poa sana,tunahitaj tu ubunifu wa kupeleka mipira mbele
 
Wanaosema mechi ilikuwa boring sijui wanatumia vigezo gani. Mechi ilikuwa nzuri na tume-outshine Chelsea. Timu hii imekamilika to be frank, tunahitaji mbinu za kuwa tnashinda mechi na kocha kuinua viwango vya baadhi ya players pamoja na kuongeza morali ya players.

Man of the match, ni Mendy.

Sent from my SM-J530F using JamiiForums mobile app
 
Baada ya kuingia pogba na Cavani Chelsea ilibidi warudi nyuma kudadadeki.
 
Ole haya majaribio yako na Dani James sasa iwe mwisho..the boy is championship quality.

VdB (£40m) anasugua benchi huku James akirukaruka tu..Poor game management..na hakuna namna leo chelsea wangetuacha tupige tu counter,kwahiyo kumuazisha ilikuwa ni ujinga tu..


Chelsea hawakufanya lolote kuonyesha wanataka kushinda..
 
TUANZEBE hanyongi mtu bana.

Maguire kila siku vituko, tushukuru Shaw alikuwa mbali
 
Tuna point saba na tuna game moja,hao wanaoitwa wakali wa epl,man city na liva hali zao hohe hahe,sasa sijui huwa tunafananishsa nan?au everton na leeds?
So far tupo vizuri,naiman katikat ya mwezi november tutakua even better.
By z way liva kashapigwa anatafuta mpira kwa tochi,naona klop kamfata referee analalamika eti kazima taa uwanjani,mpira hauonekani
 
Hahahahahah haya bwana
 

Tuone mwisho wa mechi itakuaje na msimamo wa League unasemaje
 
OGS leo angemuanzisha Telles badala ya Shaw naimani tungeshinda,hasa baada ya kuingia cavan
Changamoto kubwa ya luke shaw,anapoteza sana mipira
 
Rudia tena kusoma uone kama kuna sehemu nimeandika mechi kumi.......
Ndani ya mechi moja anakukera mara kumi anakufurahisha mara moja

Sent from my itel S31 using JamiiForums mobile app
 
Inatakiwa kila mtu ashinde mechi zake, ukijilinganisha na timu nyingine ni makosa, wakati nyingn zinafanya vibaya wew fanya vizuri ili uwe na point nyingi mana nia ni unatakata ubingwa.

Siyo ajabu nae Ole anafikiria kama ulivyofikiria wewe! Kua hata timu nyingn kubwa zimekabwa, wakat kuna nyingine zinazidi kumwacha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…