Jamani Bayern pale mbele na katikati wapo moto sana ila wakicheza na timu inayoshambulia sana na wapo makini, nawaona kama Bayern wana defence mbovu ni kwa sababu so far bado defence yao haijapata serious test. Mabeki wao wa kati (David & Jerome) sio wazuri sana wana makosa sana ni vile wamecheza na watu walio-flop kwa sasa.
Nimeona kuna mtu anasema kwa nini tusichokonoe kwa Alphonso Davies, kwenye timu yetu huyu jamaa hawezi kutufaa ni mzuri sana offensively but not defensively unless tuwe tayari na timu inayoweza kukaa na mpira zaidi. Kwa uchezaji wetu hawezi kutufaa maana huwa mara nyingi hatukai na mpira sana, sisi tunahitaji aina ya wachezaji ambao wapo comfortable hata tunapokuwa hatuna mpira kwa muda mrefu.
Luke Shaw hofu yangu kwake ni injury prone tu ila anaweza kui-prove zaidi akijengwa vizuri. Bissaka anahitaji kupewa training chache tu za kushambulia ila namuona amekamilika sana akijua tu kuucheza mpira hasa hasa akivuka mstari wakati ni bonge la fullback, mapungufu yake ana mchango mdogo muda tukiwa na mpira hasa tunapovuka mstari wa wakati timu ikiwa inashambulia kutokea upande wake.
Binafsi naamini tunahitaji wachezaji watatu tu kwa sasa, Beki wa kati wa maana ambaye anapaswa kuiongoza ile safu yetu ya ulinzi acheze na Harry, kiungo wa chini wakucheza nyuma ya Bruno na Paul ile nafasi ya Nemanja. Mwisho ila sio lazima sana tunahitaji mshambuliaji wa kuja kuongeza nguvu pale mbele. Mimi kwa sasa ningependa hata tupate mkongwe mmoja kwa muda wakati tunaji-fix kupata longterm target kwa sasa tumchukue mtu kama Edin Dzeko. Deal la Sancho linapoteza focus ya kujenga timu, kuna wachezaji wazuri sana kama tukiamua kufuata other options sio lazima tumkomalie yeye tu.