Kwenye mechi ya jana
Nimeona Man Utd yetu ikicheza kwa kuchoka kwenye mechi 3 au 4 zilizopita
Kuchoka kwa timu yetu, kwa asilimia kubwa kumechagizwa na kuchoka kwa Bruno Fernandez. Kama kuja kwake kumeibadilisha sana United positively, hivyo hivyo hata kuchoka kwake kumeifanya timu icheze vibaya.
Bruno amecheza mechi zote tangu aje United, tena zote dakika 90, nadhani ni mechi si zaidi ya 2 alizotolewa sub. He is not a machine, of course hata mashine zenyewe zinachoka.
Mechi ya jana kabla ya magoli, sisi mashabiki tuliona karibu kila mchezaji wetu anacheza ovyo (labda kasoro Lindelof tu), inawezekana ni kweli hawakucheza vizuri, lakini pia inawezekana kutokana na presha tuliyokuwa nayo sisi mashabiki, tuliona kila mchezaji anakosea kwa kila anachofanya. Najaribu kuwa objective hapa.
On Bruno
Kutokana na standards za Bruno, alicheza chini ya kiwango, lakini overall Bruno alidhihirisha yeye ni key man, katika key moments. Nakumbuka mapema sana ali penetrate pasi kwa Martial na akashindwa kuitumia, hata penati iliyopatikana kisha yeye kufunga, Bruno ndiye aliyetoa pasi ya kumtafutia lawama Martial (hizi pasi huwa naziita za kumtafutia lawama striker, kwa kuwa huwa ni pasi nzuri sana na striker akimisi goli anaonekana fala).
Tunamlaumu Bruno kupoteza mipira, ni kweli alipoteza mipira mingi. Lakini mchezaji yoyote anayetoa pasi za mbele, pasi za penetration na pasi za magoli, lazima pasi zake ziwe na risk kubwa ya kupotea, assists haziwezi kupatikana bila kutoa pasi zenye risk za kupotea.
Haiwezekani unataka kula yai halafu hutaki livunjike. Nakumbuka De Bruyne mechi yake na Arsenal, alipoteza mipira mingi sana kutokana na pasi zake kutofika kwa walengwa, hiyo ndio gharama ya kutoa telling pass. Sidhani kama tutafurahia pass success rate za Bruno ziwe 100%, lakini zote ni back pass na square pass (safe pass).
Itoshe kusema kuwa jana ilikuwa ni mechi ya kutafuta matokeo. Lakini mechi 4 za mwisho zimeonesha kwa wale waliokuwa wanaamini tunajitosheleza kwamba tunahitaji kusajili.