Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Leicester anaweza poteza kwa spurs na asernal...pia tutakutananae.

Naiona kama uchochoro wetu
 
Mkuu umeongea vyema sana, kiukweli kuna wachezaji huwa ni very promising katika soka la vijana lakini wanapokwenda kwenye soka la wakubwa wanaishia njiani

Man Utd ndio timu ambayo imetoa vijana wengi na wakacheza premier league kwa wingi kuliko klabu nyingine yoyote uingereza (duniani) lakini wengi wao wakichezea vilabu vingine

Umeongea mambo mengi, ila umenigusa sana ulivyotaja Ravel Morrison, huyu bwana mdogo ana kipaji kweli kweli lakini kipaji chake ndio hivyo kinapotea, kwa sasa nadhani yupo Sheffield. Huyu bwana mdogo kwa nyakati tofauti Ferdinand na Rooney wamewahi kusema kwenye kizazi chao pale United alikuwa bora kuliko Pogba na Lingard lakini angalia kwa sasa anavyotangatanga, hata Lingard amemzidi
. Kwa wasiomjua huyu dogo anacheza na vitu akina Hazard, ni mtundu mtundu kama Wabrazili hivi. Nadhani huwa kuna shida ya attitude ya wachezaji hawa vijana, angalia hata Chelsea kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa ikitawala soka la vijana Uingereza lakini hao vijana wako wapi kwenye timu ya wakubwa?

Kwa sasa tunawatazama akina Levit na Garner kama viungo wa kati watarajiwa kwa miaka inayoanzia hivi karibuni, pia yupo Traore na Mejibri. Lakini ili wafikie uwezo wao halisia ni kuwa na right mentality. Wengine pia umewataja.

Kiukweli kwa sasa sioni kama kuna tija ya kuweka hawa watoto katika mechi tunazocheza (labda kwa uangalifu sana), maana mechi zote ni kama fainali, zote ni must win games iwe Europa, iwe FA na ligi ndio kabisa. I hope msimu ujao kutakuwa na fursa za kutosha kwao kuonesha vipaji vyao.
 
SteveMollel mbona umetukaushia kutupa story za movies kwenye jukwaa letu
 
Leicester ana fixture ngumu sana, atatupisha pale juu lazima, pia tuna game nae mkononi
 
Manchesta bhana, kubalini zamanzenu zimepita. Mnashinda dhidi za timu bottom half mnaona mmerudi...
 
The problem is mnapigia hesabu wengine kupoteza. Je nyie mtashinda game zote wakati hao wengine wanapoteza? Huu ni mpira
Inaonekana hesabu za probability zilikutesa sana kijana.
Huhitaji kuwa na elimu ya juu kuona kwamba leicester ana ratiba ngumu sana ukilinganisha na sisi ofcourse anything can happen but ni ngumu kuamini atachukua 3 points kwa utd,asernal na spurs.
 
Inaonekana hesabu za probability zilikutesa sana kijana.
Huhitaji kuwa na elimu ya juu kuona kwamba leicester ana ratiba ngumu sana ukilinganisha na sisi ofcourse anything can happen but ni ngumu kuamini atachukua 3 points kwa utd,asernal na spurs.
Mkuu sawa. Ngoja tusubiri
 
Sisi tunapigania nafasi ya tatu nyie endeleenii kubaki hapo mlipo sisi hatuwezi kukaa uswahilini.
 
Pre season na mwishoni mwa ligi Manchester United utawapenda .
Ngoja ligi ianze upya

Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
Msimu uliopita mwishoni mwa Ligi, walipoteza mechi karibia zote.

Msimu 2017/18, matokeo mchanganyiko

Hata 2016/17, napo ililuwa hivyo, Mou aliamishia nguvu zote kwenye Europa league.

Sa sijajua hicho kitu ulikiona wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…