Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

KUNA kitu Bruno Fernandes ameongeza Manchester United tangu atue Old Trafford akitokea Sporting Lisbon wakati wa usajili wa Januari - nacho si kingine, bali ni ubunifu na hamu ya kushinda mechi.
Lakini, wakati Fernandes akiendele kuifanya Man United kuwa bora, bado mashabiki wa timu hiyo wanajiuliza swali hili, je, itakuwaje siku Paul Pogba akirudi uwanjani baada ya kupona majeraha ya enka yaliyokuwa yanamsumbua? Balaa.
Maana kurudi kwa Pogba kutamaanisha kuwa safu ya kiungo ya Man United itakuwa na mafundi wawili kwa wakati mmoja, kitu kitakachozidisha ufundi katikati ya uwanja kwenye kikosi cha Ole Gunnar Solskjaer.
Ila kama unajiuliza wote wawili watatumikaje kwa wakati mmoja, basi jibu lako liko kwenye mifumo hii inayotoa picha ya jinsi gani Pogba na Fernandes watakichafua pamoja.




Mfumo wa 4-3-3
Golini kama kawaida anaanza David De Gea, ukuta utakuwa na Aaron Wan-Bissaka, Victor Lindelof, Harry Maguire na Luke Shaw kama majeraha hayatasumbua, kisha mbele yao kutakuwa na viungo watatu.
Katika mfumo huu wa 4-3-3 ni wazi kuwa Fred ataanza huku Scott McTominay na Nemanja Matic wakisugua benchi katika nafasi ya kiungo wa kati, kisha upande wake wa kushoto atasimama Fernandes na kulia atasimama Pogba.
Kama Frank Lampard alivyowatumia Ross Barkley na Mason Mount dhidi ya Everton, inawezekana kucheza na viungo washambuliaji wawili katika hizo nafasi mbili, lakini kikubwa waridhie kushuka chini kukaba.



Mfumo wa 4-2-3-1
Solskjaer anaweza kuamua kutumia viungo wawili wa chini katika mfumo wa 4-2-3-1, hivyo eneo hilo anaweza kumtumia McTominay na Pogba.
Hii itamruhusu Pogba kuchezesha timu kutokea chini wakati Fernandes atapewa ruhusa ya kutembea juu na kucheza huru huku akiwa na jukumu la kutengeneza nafasi akitokea shimoni.
Kulia na kushoto kwa Fernandes katika mfumo huu wanaweza kutumiwa kina Daniel James na Anthony Martial, huku kinda Mason Greenwood akisimama mbele peke yake kuongoza mashambulizi.




4-1-2-1-2
Katika mfumo huu, Solskjaer anaweza kutumia mfumo wa Diamond katika eneo la kiungo. Mfumo huu tayari Man United imeshautumia katika siku za karibuni na kuleta matokeo chanya.
Fred atacheza kama kiungo wa chini, kisha mbele yake kulia na kushoto watakuwa McTominay na Pogba mbele yao atasimama Fernandes ambaye atakuwa nyuma ya washambuliaji wawili akiwa na jukumu la kuwalisha.
Mbele kabisa Martial anaweza kuanza sambamba na mmoja kati ya Greenwood, Daniel James au hata Odion Ighalo.



Mfumo wa 3-4-2-1
Man United ya Solskjaer imekuwa na utamaduni wa kubadilikabadilika katika mifumo ambayo inatumia hasa kutokana na aina ya wapinzani. Kuna wakati wamekuwa wakitumia mabeki watatu au watano kama ambavyo walifanya katika mechi dhidi ya Manchester City.
Lindelof, Maguire na Shaw watacheza kama mabeki watatu wa kati katika mfumo huu, kisha Wan-Bissaka na Brandon Williams watacheza kama ‘mawing-backs’ wa kulia na kushoto.
Fred na McTominay wanaweza kucheza kama viungo wa chini huku Pogba na Fernandes wakisogea juu kidogo na kutanua uwanja kulia na kushoto ambapo Martial ataongoza mashambulizi.



Mfumo wa 5-3-2
Mwisho kabisa utatu wa eneo la kiungo wa Fernandes, Fred na Pogba utajaziliziwa pembeni na Wan-Bissaka na Williams, huku mbele kukiwa na watu wawili ambao ni Martial atakayecheza na Greenwood, James au Ighalo.
Katika mfumo huu mabeki wa kati wataziba nafasi ambazo zitaachwa na Pogba na Fernandes pindi wakiwa wamepanda mbele kushambulia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KUNA kitu Bruno Fernandes ameongeza Manchester United tangu atue Old Trafford akitokea Sporting Lisbon wakati wa usajili wa Januari - nacho si kingine, bali ni ubunifu na hamu ya kushinda mechi.
Lakini, wakati Fernandes akiendele kuifanya Man United kuwa bora, bado mashabiki wa timu hiyo wanajiuliza swali hili, je, itakuwaje siku Paul Pogba akirudi uwanjani baada ya kupona majeraha ya enka yaliyokuwa yanamsumbua? Balaa.
Maana kurudi kwa Pogba kutamaanisha kuwa safu ya kiungo ya Man United itakuwa na mafundi wawili kwa wakati mmoja, kitu kitakachozidisha ufundi katikati ya uwanja kwenye kikosi cha Ole Gunnar Solskjaer.
Ila kama unajiuliza wote wawili watatumikaje kwa wakati mmoja, basi jibu lako liko kwenye mifumo hii inayotoa picha ya jinsi gani Pogba na Fernandes watakichafua pamoja.




Mfumo wa 4-3-3
Golini kama kawaida anaanza David De Gea, ukuta utakuwa na Aaron Wan-Bissaka, Victor Lindelof, Harry Maguire na Luke Shaw kama majeraha hayatasumbua, kisha mbele yao kutakuwa na viungo watatu.
Katika mfumo huu wa 4-3-3 ni wazi kuwa Fred ataanza huku Scott McTominay na Nemanja Matic wakisugua benchi katika nafasi ya kiungo wa kati, kisha upande wake wa kushoto atasimama Fernandes na kulia atasimama Pogba.
Kama Frank Lampard alivyowatumia Ross Barkley na Mason Mount dhidi ya Everton, inawezekana kucheza na viungo washambuliaji wawili katika hizo nafasi mbili, lakini kikubwa waridhie kushuka chini kukaba.



Mfumo wa 4-2-3-1
Solskjaer anaweza kuamua kutumia viungo wawili wa chini katika mfumo wa 4-2-3-1, hivyo eneo hilo anaweza kumtumia McTominay na Pogba.
Hii itamruhusu Pogba kuchezesha timu kutokea chini wakati Fernandes atapewa ruhusa ya kutembea juu na kucheza huru huku akiwa na jukumu la kutengeneza nafasi akitokea shimoni.
Kulia na kushoto kwa Fernandes katika mfumo huu wanaweza kutumiwa kina Daniel James na Anthony Martial, huku kinda Mason Greenwood akisimama mbele peke yake kuongoza mashambulizi.




4-1-2-1-2
Katika mfumo huu, Solskjaer anaweza kutumia mfumo wa Diamond katika eneo la kiungo. Mfumo huu tayari Man United imeshautumia katika siku za karibuni na kuleta matokeo chanya.
Fred atacheza kama kiungo wa chini, kisha mbele yake kulia na kushoto watakuwa McTominay na Pogba mbele yao atasimama Fernandes ambaye atakuwa nyuma ya washambuliaji wawili akiwa na jukumu la kuwalisha.
Mbele kabisa Martial anaweza kuanza sambamba na mmoja kati ya Greenwood, Daniel James au hata Odion Ighalo.



Mfumo wa 3-4-2-1
Man United ya Solskjaer imekuwa na utamaduni wa kubadilikabadilika katika mifumo ambayo inatumia hasa kutokana na aina ya wapinzani. Kuna wakati wamekuwa wakitumia mabeki watatu au watano kama ambavyo walifanya katika mechi dhidi ya Manchester City.
Lindelof, Maguire na Shaw watacheza kama mabeki watatu wa kati katika mfumo huu, kisha Wan-Bissaka na Brandon Williams watacheza kama ‘mawing-backs’ wa kulia na kushoto.
Fred na McTominay wanaweza kucheza kama viungo wa chini huku Pogba na Fernandes wakisogea juu kidogo na kutanua uwanja kulia na kushoto ambapo Martial ataongoza mashambulizi.



Mfumo wa 5-3-2
Mwisho kabisa utatu wa eneo la kiungo wa Fernandes, Fred na Pogba utajaziliziwa pembeni na Wan-Bissaka na Williams, huku mbele kukiwa na watu wawili ambao ni Martial atakayecheza na Greenwood, James au Ighalo.
Katika mfumo huu mabeki wa kati wataziba nafasi ambazo zitaachwa na Pogba na Fernandes pindi wakiwa wamepanda mbele kushambulia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ktk mifumo yote hapo ujamuweka Rashfod, na kijana anakua mzuri akitokea kushoto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hilo jopo la Makocha ndiyo litaifikisha Manchester United mbali, bahati mbaya kuna mashabiki kazi yao kumuona Ole, hafai
 

Attachments

  • IMG-20200315-WA0000.jpg
    IMG-20200315-WA0000.jpg
    57.5 KB · Views: 4
Naamini muda huu Mourinho angekuwa ameshachakaa vibaya mno pale Totenham stadium,London
 
MAAMUZI MAGUMU!
HATMA YA UBINGWA WA LIVERPOOL KUPITIA MBINU HIZI.



LICHA ya kusimamisha Ligi Kuu England kwa wiki tatu hadi Aprili 3 mwaka huu, vichwa vinawauma mabosi wa bodi ya EPL, kutokana na kutakiwa kuja na majibu ya nini kitafanyika iwapo virusi vya Corona vitaendelea kuitesa nchi hiyo.
Hadi sasa hakuna jibu la moja kwa moja linalotolewa na mabosi hao ambao wanatarajiwa kufanya kikao cha dharura wiki hii, kuhusiana na nini kitafanyika ikiwa tatizo la Corona litadumu kwa muda mrefu maana Ligi Kuu England haina kanuni inayoeleza hatua gani zitachukuliwa iwapo ligi itavunjika.

Lakini, wachambuzi wa soka la England wamekuja na aina nne za uamuzi mgumu ambazo vigogo hao wanaweza kuchagua moja.



UAMUZI WA KWANZA:
Kuvunja Ligi
Huu ni uamuzi unaowakera zaidi mashabiki wa Liverpool waliokuwa wanaamini huu ni mwaka wao na baada ya mechi 29 msimu huu wanaongoza ligi kwa tofauti ya pointi 25 mbele ya Manchester City inayoshika nafasi ya pili na wanahitaji mechi mbili tu kutwaa ubingwa wao wa kwanza baada ya miaka 30.
Lakini, kwa mujibu wa uamuzi huu uliowekwa mezani na Makamu Mwenyekiti wa West Ham, Karren Brady, kwa upande wake anashauri ligi ivunjwe na kila kitu kianze upya kuwe hakuna bingwa wala timu ya kushuka daraja, hii ni nzuri kwa timu yake inayoshika nafasi ya 16 ikiwa na pointi 27 na wastani mzuri wa mabao kulinganisha na timu zilizo chini ya mstari wa kushuka daraja.
Uamuzi huu unaiathiri zaidi Liverpool inayokaribia kutwaa taji la Ligi Kuu kwa mara ya kwanza baada ya miaka 30, lakini pia uamuzi huu utaiathiri Leicester City ambayo ipo kwenye nafasi nzuri ya kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.


UAMUZI WA PILI:
Kumalizia MECHI
Huu ndiyo uamuzi ambao mabosi wa EPL, wanaona hauna utata kila timu na itapata inachostahili, kupitia uamuzi huu wanataka kusubiri na kumaliza ligi kivyovyote na hata kama tatizo la virusi vya Corona litachukua muda mrefu kiasi gani, lakini vikiisha tu ligi imaliziwe ndipo msimu mpya uanze.
Lakini, ili hili litokee lazima michuano ya Euro 2020 isifanyike ili kutoa nafasi kwa klabu kucheza mechi za ligi wakati wa kiangazi, maana kama michuano hiyo ikiwapo wachezaji watajiunga na timu zao za taifa na hawatapata nafasi ya kucheza soka katika ngazi ya klabu.


UAMUZI WA TATU:
Ligi kuisha hapa
Kama tatizo la Corona lisipomalizwa mapema basi mashabiki wengi wa Liverpool wanataka uamuzi huu ambao ni kumaliza ligi katika hatua hii na kuwapa ubingwa huku. Norwich City, Aston Villa and Bournemouth zikishushwa daraja.
Uamuzi huu unainufaisha zaidi Liverpool ambayo itapata ubingwa ambao inastahili, lakini unaziumiza timu nyingi, kuanzia zile zitakazoshushwa daraja wakati zikiwa na nafasi bado ya kupamba na kubaki Ligi Kuu hasa kutoka na ukweli kuwa tofauti kati ya timu ya 18 na ya 17 na 16 ni mabao tu.
Lakini pia timu ambazo zinapambana kutafuta nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya, Manchester United, Wolves na Sheffield United zitaathiriwa na uamuzi huu kwa sababu bado zina nafasi ya kuingia nne bora kama ligi ikiendelea, lakini ikimalizwa hapa basi hawatashiriki michuano hiyo mwakani.


UAMUZI WA NNE:
Kuongeza idadi ya timu
Ili kuepusha kelele ya timu zitakazoshuka daraja na pia kuiwezesha Liverpool kutwaa ubingwa ambao imeupigania sana msimu huu, basi Bodi ya Ligi inaweza kuamua hakuna kushusha timu daraja na kuipa ubingwa Liverpool.
Na ili kuzipa haki zile timu ambazo zimekuwa na msimu bora Ligi Daraja la Kwanza, timu za Leeds na West Brom zipewe nafasi ya kupanda daraja, hii itamaanisha kuwa msimu ujao utakuwa na timu 22 badala ya 20, huku kila timu ikifurahi, japokuwa zile za timu zinazowania nafasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa zitalia lia tu.


Ndugu mwanamichezo nini maoni yako?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom