CORONA YAISHIKA PABAYA MAN UNITED
THAMANI ya Manchester United kwenye soko la hisa la Marekani imeporomoka kwa Pauni 1 bilioni kutokana na mlipuko wa virusi vya corona unaozidi kuitikisa duniani kwa sasa.
Michuano kibao ya soka duniani, ikiwemo Ligi Kuu England na Ligi ya Mabingwa Ulaya imesimama kutokana na mlipuko wa Corona ambao hadi sasa umesababisha vifo vya watu 7,900.
Inaelezwa mlipuko huo umesababisha mtikisiko kwenye soko la hisa la Marekani na thamani ya Manchester United imeshuka kutoka Pauni 3 bilioni hadi Pauni 2 bilioni.
Mwezi mmoja uliopita miamba hiyo ya England ilikuwa na thamani ya Pauni 3 bilioni, lakini tangu mlipuko wa Corona hisa hizo zimeshuka thamani kwa kasi kubwa sana, hisa moja imeshuka hadi Pauni 9.99 kutoka 16.53 mwanzo wa mwaka huu.
Man United ilinunuliwa na family ya Glazer mwaka 2005 kwa thamani ya Pauni 790 milioni ambayo imepanda licha ya wamiliki hao kupingwa sana na mashabiki kutokana namna wanavyoendesha klabu hiyo.
Tangu mwaka jana, Mwana Mfalme wa Saudi Arabia, Mohammed bin Salman amekuwa akijaribu kuinunua timu hiyo huku wamiliki familia ya Glazer ikiweka wazi inataka Pauni 3 bilioni ndiyo iuze klabu hiyo.
Kama wakifanikiwa kuuza kwa bei hiyo watapata faida mara zaidi ya tatu ya kile ambacho baba yao Malcolm Glazer alitumia wakati akiinunua timu hiyo.
Lakini, wakati huu ambao timu hiyo imecheza mechi 11 bila kufungwa, mlipuko wa virusi vya Corona unaonekana kuharibu mambo Old Trafford.
Inaelezwa nahodha mpya wa timu hiyo, Harry Maguire ndiyo amerudisha umoja ndani ya klabu hiyo kutokana na kuanzisha vipindi vya kuzungumza usiku kila baada ya mazoezi.
Wakati huo huo; Mlipuko wa virusi vya corona unazidi kuleta majanga kwenye timu za Ligi Kuu England na sasa kuna taarifa kuwa vituo vya televisheni vya Sky Sports na BT Sport vimepanga kuvishitaki vilabu hivyo kama msimu hautaisha.
Inaelezwa kampuni hizo mbili za televisheni zitazipiga faini ya Pauni 750 milioni klabu za ligi kuu kama msimu usipoisha kwa kuvunja makubaliano ya kimkataba.
Taarifa kutoka England zinadai mkataba wa vituo hivyo na klabu za ligi kuu unaeleza wazi vituo hivyo vimenunua haki ya televisheni ya msimu mzima hivyo kama msimu ukiishia nusu ni kuvunja makubaliano ya kimkataba.
Hata hivyo, kwa jumla madai ya vituo hivyo vya televisheni yatapelekwa kwenye vyombo vya sheria ikiwa tu hiyo Aprili 4, ligi itashindwa kuendelea kama ilivyokuwa imepangwa.
Sent using
Jamii Forums mobile app