Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

DE GEA AKALIA KUTI KAVU KISA MAGOLI YA UZEMBE




Maisha ya David De Gea ndani ya Manchester United yako shakani na huenda akapoteza namba katika kikosi cha kwanza.
Baada ya kufanya makosa ya mara kwa mara, Man United ipo njiani kufanya mazungumzo ya kumsajili kwa mkopo kipa Dean Henderson akitokea Sheffield United.
De Gea ameigharimu Man United mabao saba ambayo yametia doa ubora wake tangu alipojiunga na klabu hiyo mwaka 2011 akitokea Atletico.
Kosa la kutoa zawadi ya bao kwa mchezaji wa Everton Dominic Dominic Calvert-Lewin limemuweka katika mazingira magumu De Gea.
Ingawa kocha Ole Gunnar Solskjaer anamtaja De Gea ni kipa bora duniani licha ya kufanya makosa ambayo yameigharimu Man United katika baadhi ya mechi.
Henderson (21) anatajwa ni mmoja wa makipa bora katika Ligi Kuu England. Pia kipa huyo ni mchezaji wa timu ya taifa ya vijana England.
Man United inatarajiwa kuzungumza na wawakilishi wa kipa huyo mapema mwezi huu. Henderson alisajiliwa na Man United mwaka 2015 kabla ya kutolewa kwa mkopo Sheffield.
Kipa namba mbili Sergio Romero anatarajiwa kucheza mechi ya Kombe la FA dhidi ya Derby.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hili gazeti umeandika wewe au mlevi gani??(Joke)

Dean Henderson ni mchezaji wetu,hakuna haja ya kumsajili ni kumrudisha tu
 
Tahit Chong ni right wing pekee pale united kwa sasa japokuwa huwa anacheza na left wing pia.

Angel Gomez ni central attacking midfielder ambaye kwenye kikosi cha sasa kwenye pecking order huenda ni wa sita baada ya Bruno Fernandez, Juan Mata, Andre's Pereira na Jesse Lingard sometimes Paul Pogba sasa unaweza ukaona ugumu anaokabiliana nao kuwaondoa hao viumbe hapo juu.

Tahit Chong ukimuondoa Daniel James labda na Rashford hakuna watu wengine wakicheza hizo nafasi ndiyo maana anapewa nafasi kubwa ili apate uzoefu kama atafanya vizuri united wasiingie sokoni kutafuta winger mwingine.

Kingine Tahit Chong huwa anafanya vizuri sana kwenye kile kikosi cha under 23.
Sijajua kwanini Ole anamprefer zaidi chong kuliko Gomez ,mimi naona chong bado sana hajatulia na anapapara sana bora Gomez anaonyesha ana kitu fulani natamani kumuona benchi zaidi kuliko huko under 23.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, nakubaliana na hoja zako ulizoweka humu lakini ngoja nizungumzie suala la uzoefu wa Ole.

Ni ukweli usio na shaka kwamba Ole anazidiwa kwa mbali sana katika management na hao walimu uliowataja hii inatokana na uzoefu wao na kufanya kazi katika vilabu tofauti tofauti kwa muda mrefu kuliko Ole.

Jambo linalonipa Faraja juu yake ni kuwa amekutana na hawa walimu pamoja na ubora wa vikosi vyao ukilinganisha na united amegoma kuwa mnyonge mbele yao.hivyo kama atakamilisha rebuild yake na kufanya assessment nzuri juu ya mapungufu yake msimu ujao huenda tukawa na timu yenye ushindani mkubwa sana.

Ni ukweli usiopingika pia Ole ameonyesha kuwa anaweza kumanage wachezaji wake vizuri pamoja na mapungufu ya hapa na pale lakini performance appraisal kwenye eneo hili wamefanya vizuri.

Bado naendelea kumpa benefit of doubt mpaka ligi iishe nione atatoka na nini kama atachanga karata zake vizuri.
baada ya kufanya operation safisha mji (darmian, valencia, young, sanchez, fellaini, smalling) pamoja na kuleta wachezaji wengine wanne (ambao ni wan bissaka japokuwa sifurahishwi na style yake ya kiuchezaji kwenye ulimwengu huu wa kisasa, maguire amekuwa kiongozi mzuri sana kwa wachezaji, daniel james huyu natumai kilio changu cha mwanzoni wa msimu kitafanyiwa kazi na ole msimu ujao ambapo sikupendelea huyu dogo awe mchezaji wa kikosi cha kwanza, bila ya kumsahau bruno fernandez) hao wote kwa pamoja wameweza kuleta utofauti mkubwa kwenye kikosi chetu kwa muda mfupi zaidi.

ni matumaini yangu dirisha la tatu la usajili chini ya ole gunnar (tutamaliza biashara ya rebuilding kwa kutafuta wachezaji wengine sahihi hususani eneo la winga wa kulia) ila tatizo kubwa litakalobaki ni ubora wa mwalimu mwenyewe kututhibitishia ubora wake kimbinu, kiupande wangu bado namuona ole hajapevuka kimbinu ukimlinganisha na makocha wengineo wanaofundisha timu pinzani mfano jurgen klopp, carlo ancelotti, josep guardiola isala.

kuna nyakati sir alex alikuwa na kundi bora la wachezaji na hatimaye akafanikiwa kulitawala soka la england (1999, 2008-2009 na wapinzani wake wakasema anabebwa na timu bora pamoja na bajeti), vile vile kuna nyakati sir alex alikuwa na kundi la wachezaji wenye viwango vinavyotabirika (2010.-2012) kabla ya kuingia uwanjani ila pia alifanikiwa kulitawala soka la england na cha ajabu zaidi aliweza kucheza robo fainali ya ligi ya mabingwa takribani mara tatu ndani ya miaka minne kama nitakuwa nipo sahihi.

Hivyo basi ubora wa rebuilding unaofanywa na mwalimu hautoshi kuthibitisha ubora wake katika kuongoza timu kubwa kama manchester united (ole gunnar anapaswa kupevuka zaidi kama anahitaji kudumu man utd kwa muda mrefu zaidi, mfano mdogo tumeshacheza na wolves takribani mechi sita kwa siku za karibuni lakini mpaka leo tumeshindwa kupata tiba ya kimbinu dhidi yao).

sote hatufahamu anachokiwaza ed woodward (mzee wa suprise) kwenye mtindio wa ubongo wake, tukumbuke mara nyingi amekuwa akitamka hadharani ya kwamba klabu itaendelea kufanya kazi na ole msimu ujao kwa sababu ya kuvutiwa na mipango yake ndani ya klabu, hata nyakati za louis van gaal alimpaka mafuta kwa mgongo wa chupa na mwisho wa msimu akavunja mkataba wake licha ya kubeba ubingwa wa FA dhidi ya crystal palace na sababu kubwa anayoiangalia zaidi ni tiketi ya UEFA.

kivyovyote itakavyokuwa mwalimu yeyote atakayekuwepo msimu ujao atakuwa amebakiwa na kazi ndogo sana ya kukamilisha rebuilding ya kikosi chetu ambayo imeanza kufanywa na ole gunnar solskjaer...... ni mwendawazimu pekee ndiye atakayekuja na mkakati mpya wa kujenga timu na kuutelekeza huu uliopo.

  1. david degea au dean henderson
  2. wan bissaka + ( dalot au Ethan Laird )
  3. luke shaw + brandon williams
  4. eric bailly + lindeloff + tuanzebe
  5. harry maguire
  6. scott mctominay + nemanja matic (man of the match wa mechi yetu dhidi ya everton kwa mtazamo wangu)
  7. fred + paul pogba
  8. bruno fernandez
  9. marcus rashford
  10. anthony martial
  11. daniel james + greenwood + juan mata

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumalize mechi mapema, Fernandez na Fred wapumzishwe
manchesterunited___B9XMvvtDZ9j___.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom