Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ighalo over Josh King!

Sent using Jamii Forums mobile app
Asee yawezekana ighalo akatusaidia ila naamini Josh alikuwa sahihi sana hasa ikizingatiwa ametoka ktk youth set up yetu. Wapuuzi sana bodi ya hii timu,yaani wwlivyoona ofa ya kwanza imekataliwa wakaahirisha hapohapo na king mwenyewe alikuwa yupo tayari na kocha wake alishakubali matokeo kwa kuamini mchezaji anataka kwenda Man U. Mi niliamini nikiamka ningekutana na habari za King kusajiliwa Man U.
 
Mara zote pogba ameingia kikosi bora cha uingereza unasemaje hayupo top 5? Hichi ni kikosi bora cha ligi ya uingereza msimu uliopita


Na kwenye 3 man midfield yupo.
huu mjadala kama unaendelea ni bora uendelee kuwa wa amani kimaneno..... kuna nyakati hapo jana presha ilipanda sana kwa pande zote mbili.

ujio wa ighalo una tafsiri gani kwako hususani kipindi hiki ambacho marcus rashford ni majeruhi?
  • anthony martial atarudi upande wa kushoto huku eneo la mshambuliaji akisimama ighalo?
 
Cha ajabu unaleta stats za msimu uliopita kuwa Pogba ni bora, ambaye hajacheza mechi hata 10, hana goli hata moja

Haya ni madhara makubwa ya kukariri

Msimu huu amekuwa bora kupata majeraha na kukalikiti nywele na sio uwanjani

Msimu wa mwaka jana wenyewe amefunga goli 13/14 (hichi ndio kigezo kikubwa kilichotumika kumuweka) , goli 7 kati ya hizo ni penati, kati ya penati 12 alizopiga, kakosa 5

Huyu hata Pep alimkataa hawezi kuwa top 5 ya midfielders UK, hata akina Moutinho wanaweza kumuweka benchi

Hawezi kuwa juu ya KDB, Kante (akichezeshwa juu), Grealish, Madison wala Silva
Msimu huu unaitwa 2019/20 msimu ujao ndio 20/21

Waandikie email ligi ya uingereza kuwa wamekosea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asee yawezekana ighalo akatusaidia ila naamini Josh alikuwa sahihi sana hasa ikizingatiwa ametoka ktk youth set up yetu. Wapuuzi sana bodi ya hii timu,yaani wwlivyoona ofa ya kwanza imekataliwa wakaahirisha hapohapo na king mwenyewe alikuwa yupo tayari na kocha wake alishakubali matokeo kwa kuamini mchezaji anataka kwenda Man U. Mi niliamini nikiamka ningekutana na habari za King kusajiliwa Man U.
Upatikanaji wa Josh ni mpaka Bournemouth wapate mbadala kwanza na kwa muda uliobakia ilikuwa ni ngumu.
 
huu mjadala kama unaendelea ni bora uendelee kuwa wa amani kimaneno..... kuna nyakati hapo jana presha ilipanda sana kwa pande zote mbili.

ujio wa ighalo una tafsiri gani kwako hususani kipindi hiki ambacho marcus rashford ni majeruhi?
  • anthony martial atarudi upande wa kushoto huku eneo la mshambuliaji akisimama ighalo?

Japo Ighalo ni panic buy ila angalau kuna positive kwenye usajili wetu, bruno miaka na miaka anaipenda man U na ighalo vile vile anaipenda sana man u na amekua hali ya kuwa akiishabikia, tumemuacha yule striker wa kibrazil ambaye Sociedad wamemu offer man Utd.

Mimi namuona Ighalo kama plan B, akianza Greenwood, Ighalo atakuwa bench na tutacheza na james kushoto, martial kati na greenwood kulia, na kwenye mfumo kama tuliocheza na City Ighalo atakuwa lone striker na martial ataenda kushoto, kifupi atatupa dimension ambayo mwanzo tulikuwa hatuna. Na kama Ole ataswitch 4-3-3 sababu ya bruno wote Greenwood, martial na Ighalo wanaweza kuanza, uzuri ni kwamba kuna break ya kimataifa ambayo pengine ikiisha Mc tominay na Pogba watakuwa wamerudi.
 
Well deserved
Screenshot_20200201-150250~2.jpeg
 
MANCHESTER United imekamilisha usajili wake matata kabisa kwenye dirisha la Januari kwa kumnasa Bruno Fernandes.
Kuwasili kwa kiungo huyo wa Kireno huko Old Trafford, kuna watu itakula kwao. Katika kukamilisha dili hilo, Man United imelipa Pauni 46.6 milioni na Pauni 21.2 milioni nyingine italipa baadaye kutokana na maendeleo ya mchezaji huyo ndani ya uwanja, ikiwamo kama atawasaidia Man United kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu.
Kocha Ole Gunnar Solskjaer msimu huu amekuwa akipendelea zaidi fomesheni mbili 4-3-3 na ile ya 3-4-1-2, ambayo amekuwa akiitumia kwa siku za karibuni. Kwenye mchezo wa Kombe la Ligi nusu fainali ya pili dhidi ya Manchester City, Solskjaer alitumia zaidi fomesheni ya kushambulia 4-3-3, ambayo wakati mwingine uwanjani ilikuwa ikionekana 4-2-4.
Ujio wa Fernandes unampa nafasi zaidi Solskjaer kujimwambafai. Kwa sababu kiungo huyo wa Kireno anaweza kucheza kiungo wa kati, kiungo mshambuliaji (namba 10) na kiungo wa pembeni.
Haionekani kama Solskjaer atamchezesha Fernandes kwenye kiungo ya pembeni, nafasi ambayo mara kadhaa kwenye timu ya taifa ya Ureno. Kwenye kikosi cha Man United, viungo wa pembeni hawana shida, shida ipo kwenye viungo wa kati.
Kwa maana hiyo, Fernandes anatua Man United kwenda kushindana kuwania nafasi kwenye kiungo ya kati na hapo kuna wachezaji watatu wapo kwenye hatari ya kupoteza nafasi kwenye kikosi cha kwanza: Scott McTominay, Jesse Lingard na Andreas Pereira.
McTominay alikuwa mchezaji muhimu kwenye kikosi cha kwanza cha Man United hadi hapo alipopata maumivu ya goti, ambayo yamemweka nje ya uwanja hadi baadaye mwezi huu. Hivyo, huenda akajiikuta kwenye wakati mgumu sana atakaporejea uwanjani kwa sababu itamlazimu kupigania nafasi.
Lingard ndiye aliye kwenye hatari zaidi ya kupoteza nafasi, hasa kutokana na mara nyingi kupangwa kwenye namba 10 kwenye fomesheni za 4-3-3 na 3-4-1-2. Sasa mwenye ufundi wake kwenye namba 10, Fernandes amewasili, Lingard ataponaje?
Kwenye eneo hilo bila ya shaka, Solskjaer atamtupa benchi Lingard na kumtumia zaidi Fernandes kutokana na uwezo wake wa kufunga mabao na kutengeneza nafasi kwa wachezaji wenzake.
Pereira naye yupo kwenye hatari ya kupoteza nafasi yake kwenye kiungo ya kati, bila ya shaka Solskjaer atamtumia Fernandes kwenye nafasi hiyo baada ya staa huyo wa Kibrazili kuwa na kiwango kisichoeleweka, kinapanda na kushuka kama homa za vipindi.
Fred, kwa upande wake ameonekana kuwa kwenye kiwango bora sana kwa sasa, hivyo atakuwa na nafasi katika kiungo ya kati, lakini ushindani utakuwa kwa Nemanja Matic na ushindani utakuwa mkali wakati Paul Pogba atakapopona na kurudi uwanjani. Fernandes akitumika kama namba 10, hapo Lingard, Juan Mata na Pereira watalazimika kuanzia kwenye benchi. Fernandes akitumika kama kiungo wa kati, shughuli itakuwa kwa Matic, McTominay, Fred na Pereira na kama akitumika kwenye kiungo ya pembeni, basi Daniel James, Anthony Martial na pengine Mason Greenwood watalazimika kusubiri kwenye benchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAMA kuna usajili ulisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa Manchester United basi ni huu wa Bruno Fernandes aliyetua Old Trafford juzi akitokea Sporting Lisbon, kulekule walikowachukua Luis Nani na Cristiano Ronaldo enzi zile za Sir Alex Ferguson.
Baada ya kumkosa wakati wa usajili wa kiangazi, Man United imetumia sehemu kubwa ya dirisha dogo la usajili kupambana kunasa saini ya kiungo huyo na hatimaye siku chache kabla usajili kufungwa alitua Trafford.
Kwa nini watu wengi wanaamini Fernandes atakuwa suluhisho katika safu ya kiungo ya Man United? Ametoka wapi? Ni ipi historia yake? Na kipi ataongeza? Ni baadhi ya maswali ambayo yatajibiwa na makala haya;-




Ni nani?
Jina lake kamili ni Bruno Miguel Borges Fernandes, alizaliwa Septemba 8, 1994, katika kitongoji Maia, Porto, nchini Ureno, alianzia kucheza soka katika klabu ya Novara inayoshiriki Ligi Daraja la Pili nchini Italia, kabla ya kutua Udinese, kisha Sampdoria zote za Serie A.
Mwaka 2017, alijiunga na Sporting Lisbon ambako alijenga jina lake na kuibuka kuwa mmoja kati ya wachezaji tishio zaidi wa kiungo barani Ulaya, akishinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Ureno katika misimu ya 2017–18 na 2018–19. Januari 2020, Man United ilimnasa kwa dau la awali la Pauni 47 milioni.



Frank Lampard wa Kireno
Fernandes, 25, anajulikana kama Lampard wa Kireno kutokana na aina yake ya uchezaji ambayo imetawaliwa na kufunga mabao mengi akitokea kwenye eneo la kiungo.
Kama ilivyokuwa kwa Lampard ambaye enzi zake uwanjani alisifika kwa kuwa kiungo mwenye mabao mengi, huku akifunga sana kwa mashuti makali ya mbali na Fernandes pia ni hatari sana akiwa katikati ya Uwanja.
Wakati Lampard akifunga mabao 27 kutokea katikati ya Uwanja katika msimu wa 2009-10, Fernandes aliweka rekodi ya kuwa kiungo mwenye mabao mengi zaidi msimu uliopita kutokana na kufunga mabao 32 katika mechi 50.
Mbali na kufunga Fernandes pia anajua sana kupiga pasi za mwisho, katika mechi 134 alizocheza akiwa na kikosi cha Sporting Lisbon amefunga mabao 63 na kupiga pasi za mabao 42 hii inanyesha jinsi gani staa huyu anakuja na mabao Old Trafford.



Fundi mwenye jicho la tatu
Huyu jamaa anajulikana kwa jina la Fundi Mwenye Jicho la Tatu au ‘The Three-Eyed Maestro’ kama ambavyo amekuwa akiitwa huko kwao kutokana na aina yake ya uchezaji.
Pale timu yake inapopoteza mpira hukabia juu akiwa na straika ili kuwapa wakati mgumu mabeki wa kati wa timu pinzani, wapinzani wakifanikiwa kuondoa mpira katika eneo lao la hatari na yeye hushuka chini kabisa kucheza kama kiungo wa chini.
Timu yake ikiwa inashambulia hupenda kupandisha timu juu au kucheza pembeni ya mshambuliaji na kusubiri kugongeana naye haraka na kuwazuru wapinzani. Mashabiki wake pale Sporting walikuwa wanamuita ‘Three-Eyed Maestro’ wakimaanisha kiungo fundi mwenye jicho la tatu jina hili lilikuja kutokana na uwezo wake mkubwa sana wa kupiga pasi kwa wenzake hata katika mazingira magumu.
Fernandes ana uwezo wa kupiga chenga, kukokota mpira na miguu yote miwili, mzuri kwenye mipira ya kichwa anajua kupiga mipira iliyokufa ana mashuti makali sana na ni aina ya kiungo ambaye hukaa nje ya boksi kusubiri mipira ianguke na kumuadhibu mpinzani.


Jezi namba 10
Fernandes anajiamini sana akiwa na miaka 21 alienda Sampdoria akitokea Udinese na baada ya kufika pale akadai kuwa anaitaka jezi namba 10 ya timu hiyo, jezi ambayo inaheshimika sana ndani ya klabu hiyo kutokana na kuvaliwa na magwiji kama Roberto Mancini, hii iliwashangaza wengi, lakini huyo ndiye Bruno ambaye haogopi presha ya mashabiki.


Soka la kimataifa
Wakati akiwa Italia hakuwahi kuitwa kwenye timu ya taifa ya Ureno, kwa mara ya kwanza Fernandes alichaguliwa kujiunga na timu yake ya taifa Agosti 28, 2017 akichukua nafasi ya Pizzi ambaye aliumia kuelekea mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Visiwa vya Faroe, lakini hakucheza mechi hiyo.
Fernandes alichezea timu ya taifa ya Ureno chini ya miaka 23 katika michuano ya Olimpiki mwaka 2016, na kwa mara ya kwanza alichezea timu ya taifa ya wakubwa Novemba 10, 2017 akiingia kuchukua nafasi ya Manuel Fernandes katika mechi ya kirafiki ambayo timu yake ilishinda 3-0 dhidi ya Saudi Arabia.
Alifunga bao lake la kwanza akiwa na kikosi cha Ureno, Juni 7 mwaka 2018 katika mechi ya mwisho ya kujiandaa na fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Algeria ambayo timu yake ilishinda kwa mabao 3-0.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom