Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tunataka cleansheet.

Ila kadri muda unavyokaribia pressure inanijia, maana last time nilikuja na matokeo yangu OT, dah noma sana.
ole at the wheel.... sijui nimeandika sentensi sahihi?

lazima presha iwe kubwa kwa sababu munahitaji alama 33 ili muondokane na laana ya kukosa ubingwa kwa miongo mitatu.

cool down brother...
 
ole at the wheel.... sijui nimeandika sentensi sahihi?

lazima presha iwe kubwa kwa sababu munahitaji alama 33 ili muondokane na laana ya kukosa ubingwa kwa miongo mitatu.

cool down brother...

Ubingwa uko around, shida ni pride ya kwamba tumemfunga Man Utd.

Maana sasa hivi ni nyie tu mnaotupigia kelele kwamba hatuwawezi.
 
Ubingwa uko around, shida ni pride ya kwamba tumemfunga Man Utd.

Maana sasa hivi ni nyie tu mnaotupigia kelele kwamba hatuwawezi.
teh teh
ukimkuta mshabiki wa man utd anajisifia kuwa bora mbele ya liverpool kwa kigezo cha head to head msimu huu basi mpuuzie..

ni sawa sawa na mtu anayesifia kuongezeka kwa pato la taifa lisiloleta satisfaction yeyote kwa raia wa kawaida.

uchumi umepanda kwa asilimia 10
 
teh teh
ukimkuta mshabiki wa man utd anajisifia kuwa bora mbele ya liverpool kwa kigezo cha head to head msimu huu basi mpuuzie..

ni sawa sawa na mtu anayesifia kuongezeka kwa pato la taifa lisiloleta satisfaction yeyote kwa raia wa kawaida.

uchumi umepanda kwa asilimia 10

Nimekuelewa mzee mwenzangu, ila washabiki huwa tunatambiana kwa vitu vidogo vidogo kama hivyo.

Sasa leo inabidi hizo doubts zifutike.
 
kwa mara ya kwanza nimeangalia highlight za bundesliga msimu huu kwa sababu ya huyo haaland.....
pale borussia amezungukwa na thorgan hazard, fundi jadon sancho na marco reus.

kwa hii style ya uchezaji wa haaland kama atakuja manchester united hii ya nyakati hizi tungelikuja kumtukana bure ed woodward, ole na haaland mwenyewe.

utofauti mkubwa uliopo kati ya greenwood na haaland ni kwamba mmoja wao kila timu anayokwenda anakutana na wachezaji wanaojua kumhudumia mshambuliaji.

niliwahi kuandika humu ndani ya kwamba mason greenwood amezungukwa na wachezaji vilaza ndio maana tunaogopa kumuingiza moja kwa moja kwenye kikosi cha kwanza...

greenwood kiufungaji anamzidi hata yule dogo wa barcelona mwenye thamani ya paundi millioni 40...
utofauti wao unabaki pale pale kwenye kupewa huduma stahiki (mwenzake amezungukwa na messi, griezmann, suarez, de jong n.k)

man utd hii inahitaji mshambuliaji anayejitafutia huduma mwenyewe mfano wa kylian mbappe, sergio aguero, carlos tevez, wayne rooney, luis suarez na karim benzema.

greenwood anajua kujiweka kwenye maeneo ya hatari kuliko mshambuliaji yeyote tuliyenaye.
imagine huduma zile anazozipata yesu wa manchester city aliyezungukwa na debruyne, sterling, mahrez, silva brother zimgeukie mason greenwood.

licha ya kuwa na uhaba wa washambuliaji ila kuikosa huduma ya haaland hakujanichukiza.
Ubonafsi mwingi sana aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom