Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tuna mambo mengi ya kufanya, zaidi kuja kufukua ramli chonganishi kama hizi

Ndio maana kuna upupu mwingi tu uliandikwa humu kuhusu United kupigwa nyingi na Liver lakini hatuna muda kuufukua
Manchester United niliyoiona juzi ni mbovu kwelikweli kuliko niliyoiona msimu uliopita

Namuona Guardiola akiwapiga 4+ mwenye uwezo aje kufukua hii comment jamani siku ikifika
 
Kuna kitu nakiona kwenye miguu na moyo wa Pereira ila sikioni kichwani mwake.

Tatizo la Pereira ni kuendelea kuishi utoto wake katika utu uzima wake.
timu inaweza kuwa na mwalimu hodari kimbinu na mikakati lakini akakosa wachezaji sahihi lakini pia timu inaweza kuwa na wachezaji sahihi lakini ikakosa mwalimu mwenye mipango mizuri ya kutafuta ushindi.

ni nadra sana kuikuta timu kubwa ikikumbana na matatizo yote hayo mawili kwa wakati mmoja, bahati mbaya sana kwa muda huu man utd tunasumbuliwa na matatizo hayo mawili kwa wakati mmoja.
  • kipindi cha kwanza kocha anakuja na mikakati mizuri sana ya kupambana na liverpool na hatimaye mipango inafanya kazi kwa dakika 45, tulifanikiwa kumdhibiti kiunganishi kikuu roberto firmino, bila ya kumsahau origi, robertson na mdogo wake arnold alexander, na wakati huo huo liverpool walikuwa na mwanadamu sanamu uwanjani asiyekuwa na athari yoyote na hapa namkusudia captain henderson,
  • ushawadhibiti wachezaji watano kwa mkupuo mmoja lakini cha kusikitisha tukashindwa kuitumia nafasi hiyo adhimu kwa kukosa kwetu wachezaji sahihi. ndani ya dakika 45 tunafanya shambulizi moja tu la hatari zaidi na ndilo lililotupa goli na baada ya hapo kama kawaida yetu ni mwendo wa kulose posession kwa wachezaji wetu utafikiri timu yetu haifanyi mazoezi kila siku, sijui yule andreas perreira alifanya maamuzi mangapi ya ovyo akiwa eneo la hatari la adui.
  • kipindi cha pili timu inarudi uwanjani ikiwa na mawazo ya kujilinda, ok ni sawa unalinda kwa muda wote huku midfields yako ikiundwa na claudio makele, mikel obi, michael ballak na michael essien tena dhidi ya barcelona ya xavi au gaucho. Kibaya zaidi tulikuwa tunalinda chini zaidi (karibu ya eneo letu la kujidai na kuzidi kuikaribisha presha).
  • unamruhusu trent alexander na robertson wafanye wanachokihitaji kama wanavyofanya kila siku,unategemea kitu gani ukiachana na neno bahati ipo upande wetu, wakati kipindi cha kwanza ulikwisha wadhibiti na hawakuweza kuleta athari yoyote ile golini kwako?
  • wakati huo huo liverpool walishaingiza wachezaji wawili muhimu wenye uwezo wa kutembea na mipira kwa uhakika tofauti na wachezaji wa kwetu sisi. kivyovyote kitakachofuata ni adhabu tu na si chengine au uokolewe na neno bahati ilikuwa upande wetu.

tumepata suluhu kwa udhaifu wa timu yetu kwa ujumla na si kwa ubora wa liverpool kwa mechi ya jana.
liverpool walipocheza na barcelona waliipata nafasi kama ile tulioipata sisi jana ya kuwa pungufu kabla hatujabadilisha mfumo na kilichotokezea kila mtu anakifahamu.
 
Tuna mambo mengi ya kufanya, zaidi kuja kufukua ramli chonganishi kama hizi

Ndio maana kuna upupu mwingi tu uliandikwa humu kuhusu United kupigwa nyingi na Liver lakini hatuna muda kuufukua
Nne zinawahusu kwa Guardiola

Nitakuja kufukua mwenyewe
 
Hata mech ya liverpool ulimwengu ulitabir cha ajabu mashabik wa liverpool wakaanza kuomba kila mmoja kwa lugha yake shetan kakaba mtu koo muda wote klopp anasemelea kwa waamuzi huku VVD analamba mchanga

Arsenal pia alipewa hivyo hivyo ushindi bahat mbaya aliokolewa na boko la tuanzebe

Kifupi had muda huu hujagundua kama hii timu imeweza kumudu mech kubwa?

Mech 3 hatujapoteza tia akilini hili nakwambia


Mkuu umeamua kusemelea kwa manchester city liverpool kawa kiande?


Lampard kala 4-0
Sasa kwa ubovu huu Guardiola anawaachaje?

Hata moja la kufutia machozi sidhani kama mtapata kwa jinsi timu ilivyokuwa mbovu. Mechi ya MUNLIV niliiona kabla na niliyoyasema kuhusu hiyo mechi kafukue Post zangu prior to the match

Umeona formation ambayo Guardiola aliwapelekea Crystal Palace pale kwao Selhurst Park? Sasa nne mnaponaje kwa mfano na tena mnakutana na Kevin Debruyne yupo katika form ?

Naongea hivi nikirefer ubovu wenu sasa hivi
 
Yaani chelsea arsenal na Liverpool tunapata matokeo khalafu tunafungwa na Newcastle wolves na crystal palace hapo ndipo pananichanganya
 
Tukikutana na timu inayopaki bus lazima tustruggle kwa sababu hatuna key striker
Yaani chelsea arsenal na Liverpool tunapata matokeo khalafu tunafungwa na Newcastle wolves na crystal palace hapo ndipo pananichanganya
 
Manchester United niliyoiona juzi ni mbovu kwelikweli kuliko niliyoiona msimu uliopita

Namuona Guardiola akiwapiga 4+ mwenye uwezo aje kufukua hii comment jamani siku ikifika
Hayo Maneno yalianzaa kwa Chelsea, ikaja Leicester, ikaja Arsenal alafu Liver then mnahamia Man City. Her funny!!
 
Wazee kwa kutiririka....
IMG-20191022-WA0035.jpg
 
Hivi Man. Utd kuliko kutoa pesa kwa Mandzukic si bora tuchukue Lewandowski maana kila kukicha huyu mzee lazima afumanie nyavu. Ktk umri wa miaka 31 ni mzuri sana akija pale OT anakaa pale kati alf wale watoto pembeni naimani itakuwa hatari sana yule Rashford mzuri sana akitokea pembeni. Huyu mzee ana mkataba hadi June 2023 ila tukivunja kibubu anaweza tua kutupa support. Akifikisha miaka 33 naimani itakuwa tushapata striker mwingine mdogo labda msimu ujao tunaleta kachalii kanaanza kupiga vi-carabao vile mwisho wa siku Lewandowski anasepa anaingia mtu mpyaaa. Hii barua sijui Solskjær na Ed-Woodward wataiona!
 
Back
Top Bottom