Mkuu ni kweli mwishoni baada ya Ronaldo hatukusajili sana, ila nilikuwa namjibu tu jamaa kwamba alipoondoka kenyon still timu ilikuwa inasajili vizuri 2003 mpaka 2008 yalikuja majembe mengi sana.
Kwa wasiofahamu Fergie Alikuwa ni team manager na sio kocha kama tulio nao sasa. Mara nyingi kocha msaidizi ndio alikuwa kila kitu man u, kwa kipindi hiki nilichotaja msaidizi alikuwa ni Carlos Queiroz ambaye ndio aliwaleta wareno wenzake, na jamaa ndio yupo responsible kumkuza Ronaldo hadi kuwa legend, aliwaleta watu kama Nani, Anderson, Kleberson etc timu yetu ilijaa wareno/watu wanaongea kireno wengi.
Queiroz aliondoka 2008 nafasi yake ikachukuliwa na phelan pamoja na Rene maulensteen kama first team coach,na Approach ikabadilika Rene yeye ni mholanzi tukaanza kuona kina Butner, Rvp etc na phelan nae na waingereza wake ndio ukaona na usajili nao umebadilika.
Wengi wanamlaumu Fergie ila alituachia watu 24 waliokuwa nyuma yake wanaoijua club nje ndani, moyes alipokuja kitu cha kwanza aliwafukuza na kuja na watu wake hapa ndio tukapoteza mwelekeo kabisa, na Ed yeye hajali anaangalia tu mapato taratibu timu ikapoteza mwelekeo na identity tukawa tunasajili sajili tu hatueleweki, Man u ikafanywa tu sehemu ya watu kuchukua mishahara minono na kuondoka.
Na kutomsajili Tevez nafikiri lilikuwa ni suala zuri, 3rd party ownership ilikuwa ni cancer kwenye mpira, na fergie siku zote alikuwa against na vitu kama hivi ndio maana alikuwa hazipandi na Raiola, tevez alivyoenda city walifungana magoli na Berbatov wakashare kiatu, na Rooney pia Alistep up misimu miwili mmoja alifunga goli 39 na mwengine 40 ama 41 kama kumbukumbu zipo sahihi, hivyo forward yetu haikuwa mbaya kivile japo pengo la Ronaldo lilikuwepo.
View attachment 1230778
Ila kwenye midfield ndio ilikuwa tia maji tia maji, nakumbuka kuna kipindi hadi giggs akawa midfield ya kati, tukamrudisha na scholes alipokuwa amestaafu, Na kipindi kile ndio fergie akasema duniani anaona midfield watatu tu wanaoweza kucheza pale united (tetesi ni Modric, Ericksen na sneidjer)