Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

kuna video fulani niliiangalia zamani kidogo inamuhusu jose mourinho tokea akiwa ndie kocha wa manutd msimu wake wa pili, ilikuwa ni siku mbili baada ya kufungwa na sevilla kupitia michuano ya champions league, jose mourinho alitumia takribani dakika 12 kuizungumzia hali halisi iliopo ndani ya klabu ya manchester united kwa takribani miaka 8 pamoja na timu nyenginezo.

jose alisema ya kwamba ni sahihi kulaumiwa kwa sababu ya matokeo mabovu dhidi ya sevilla lakini kufungwa kwetu na timu ya sevilla si jambo la ajabu kwa sasa kwa sababu man utd imeshakosa football heritage, hivyo basi inahitajika mipango madhubuti yenye kuambatana na muda wa kutosha kuijenga upya manchester united ili irudi tena katika ubora wake.

mara ya mwisho kwa man utd kucheza fainali ya champions league ilikuwa ni msimu wa 2010/2011 chini ya sir alex ferguson, kiupande wangu nathubutu kusema ndio fainali iliokuwa nyepesi zaidi kumtambua bingwa kabla ya mechi kuchezwa kwa kulinganisha ubora wa vikosi vya timu mbili hizo, msimu huo mchezaji bora wa ligi pamoja na klabu yetu alikuwa ni nemanja vidic.

Licha ya kubeba ubingwa wa ligi kuu msimu huo kwa tofauti ya alama 9 dhidi ya chelsea na manchester city lakini kiwango chetu cha jumla kilikuwa ni cha kawaida sana na ndio maana haikuwa ajabu kutoa suluhu mechi 11 japokuwa tulifanikiwa kukusanya alama 80 pungufu ya alama 2 tulizokusanya msimu wa 2017/2018, ukimuangalia jirani yetu imewachukua miaka miwili tu kuweza kujenga timu ambayo iliweza kujiingiza kwenye kinyang'anyiro cha kuchukua ubingwa (man city walishaonyesha dalili za kuwa tishio ila bahati mbaya mashetani wekundu wakaendelea kulala).,

mwaka mmoja baadae (msimu wa 2011/2012) man united tulipangwa kundi moja na timu nyepesi za basel, benfica, galati kutoka romania kwenye michuano ya UEFA, cha ajabu makamo bingwa alitolewa hatua ya makundi. Hatukuishia hapo tu pia tulitolewa kwenye hatua ya mtoano wa league ya europe dhidi ya athletic bilbao ya marcelo bilesa kwa magoli 5-2, msimu huo athletic bilbao walishika nafasi ya 10 kwenye ligi ya hispania. Miaka minne baada ya city kununuliwa na matajiri wa kiarabu hatimaye msimu huo walifanikiwa kubeba ubingwa kwa tofauti ya magoli dhidi ya man utd.

msimu wa 2012/2013 man utd tunafanikiwa kubeba ubingwa kwa utofauti wa alama 11 dhidi ya man city huku ukiwa ni msimu wa tano tokea man city inunuliwe na matajiri wa kiarabu kama nitakuwa nipo sahihi, ndani ya miaka mitano man city walizidi kujenga emperor yao na kuwa dominance kwenye top 3 ya ligi kuu, hatukuishia hapo tu pia msimu huo tulitolewa hatua ya 16 bora kwenye michuano ya ligi ya mabingwa dhidi ya real madrid ya jose mourinho. hatimaye sir alex akastaafu kufundisha soka.

ina maana miaka mitatu ya mwisho ya sir alex ferguson ilionyesha muelekeo wa timu kupanda juu (2010/2011), kushuka chini zaidi (2011/2012) baadae ikapanda kidogo (2012/2013),

huu ndio usajili alioufanya sir alex ferguson miaka mitano ya mwisho.
chris smalling = amefeli kuwa mrithi wa ferdinand tokea nyakati za fergie mwenyewe mpaka leo
phil jones = amefeli kuwa mrithi wa vidic tokea nyakati za fergie mwenyewe mpaka leo
alexander buttner = amefeli kuwa mrithi wa patrice evra tokea nyakati za fergie mwenyewe na leo hatujui yuko wapi
ashley young = alicheza vizuri mechi za mwanzo ikiwemo ile ya ushindi wa magoli 8 dhidi ya arsenal, baada ya hapo alipata majeruhi na hakuonyesha tena uwezo wake tuliouzoea tokea akiwa wattford na aston villa iliokuwa ikifundishwa na martin oneill, kutoka kuwa winga machachari hadi kuwa mlinzi wa pembeni
chicharito = alicheza vizuri sana lakini baadae akapoteza nafasi walipokuja walimu wengineo ambao hawakuvutiwa na uchezaji wake
robin van persie = ulikuwa ni usajili wa muda kutokana na umri wake kuwa mkubwa.
shinji kagawa = alishindwa kufikia matarajio ya klabu ndani ya uwanja.
bebe = sijui yuko wapi huyu bwege.
antonio valencia: alisajiliwa kwa dhumuni la kuziba nafasi ya ronaldo yule aliyeondoka manchester akiweka rekodi ya kufunga magoli 40 kwa msimu mmoja, kituko usajili huu haukuwahi kutupa hata magoli 5 kwa msimu mmoja, miaka yake 10 amefunga magoli 17 tu, Baadae aligeuzwa kuwa mlinzi wa pembeni.
gabriel obertan = sijui hata aliishia wapi huyu dogo.
michael owen = mfugaji farasi mwenziwe aliamua kumsitiri
david degea = huu ndio usajili pekee wa fergie unaoendelea kutupa faida ile tulioitegemea tokea kusajiliwa kwake.

kwa mtazamo wangu hawa ndio wachezaji ambao walishaanza kuonyesha dalili za kuchoka kisoka miaka mitatu ya mwisho ya utawala wa sir alex ferguson na bahati mbaya kama nilivyosema hapo juu walishindwa kupatikana warithi sahihi wa nafasi zao tokea fergie akiwa madarakani.
ji sung park
rio ferdinand
nemanja vidic
ryan giggs
darren fletcher
patrice evra
paul scholes: (alistaafu akarudishwa kana kwamba timu haina pesa)
darren gibson
tom cleverley
anderson: (kiwango chake ilikuwa ni sawa na maji kupwa na maji kujaa)
luis nani: hakuwahi kucheza vizuri mechi 10 mfululizo.

anguko letu lilianzia hapa
acha uongo... mchezaji bora wa klabu msimu wa 2010/11 alikuwa ni chicharito na mchezaji bora wa ligi alikuwa ni gareth bale.
 
Sisi tumezikuta story za Blackburn rovers kwamba ilikuwa team bora.. Hii itazungumzwa kwa man untd 5 years ahead.
 
acha uongo... mchezaji bora wa klabu msimu wa 2010/11 alikuwa ni chicharito na mchezaji bora wa ligi alikuwa ni gareth bale.
1570847781316.png


PFA Awards 2011: Gareth Bale Named PFA Player Of The Year.
hapo kwa chicharito umepatia
 
Na hichi kikosi hakikuundwa tu na watu wa zamani wakongwe kulikuwa na damu mpya zilizokuja baada ya kenyon kama vile Carlos Tevez, christiano ronaldo, Owen hagreaves, Edwin van de sir, patrice Evra, Nemanja Vidic, wayne Rooney, michael Carrick etc. Kifupi zaidi ya nusu ya timu walikuwa wachezaji wapya.

David Gill alikuwa vizuri sana, haonekani ila alikuwa anafanya mambo makubwa, alipoondoka ndio Ed anatuonesha umuhimu wa Gill.
chief tatizo letu kubwa lilianza baada ya kuwaingiza michael owen, gabriel obertan na antonio valencia kwa dhumuni la kuziba nafasi za ronaldo na carlos tevez ambao wote waliondoka msimu mmoja.

muondoe ronaldo basi angalau msajili frank ribery
ni sawa unamuondoa tevez kwa dhumuni la kumpa nafasi zaidi dimitar berbatov ili athibitishe thamani yake, lakini chief klabu ilishampoteza mwanadamu mwenye uwezo wa kukupa goli 50 kwa msimu hivyo basi si vibaya kama klabu ingelikamilisha usajili wa tevez japokuwa usajili wake ulikuwa na matatizo.

tukumbuke tevez alipokwenda man city ndiye aliyekuwa mfungaji bora.

unaizungumziaje ishu ya luka modric?
unaizungumziaje ishu ya roberto lewandowski?
how about wesley sneijder?
juan mata kutoka valencia?
david silva kutoka valencia?
hazard kutoka lille?

tulizipoteza lulu kwa makusudi huku tukiwaachia wapinzani wetu waendelee kujijenga kidogo kidogo kwa hoja dhaifu ya mishahara ya gharama na fedha nyingi za usajili.

yaliopita si ndwele tugange yajayo
 
Ukweli ni kwamba kulegalega kwenye usajili Man united ilianza zamani tu mathalani usajili wa Wesley Sneider, na Luca Modric ulikuwa uzembe wa mabosi wa united.

Hazard alichagua kwenda Chelsea ndiyo man united wakaenda kumsajili Shinji Kagawa. Haya ya woodward ni mwendelezo tu wa incompetence ya Man united kwenye usajili.
chief tatizo letu kubwa lilianza baada ya kuwaingiza michael owen, gabriel obertan na antonio valencia kwa dhumuni la kuziba nafasi za ronaldo na carlos tevez ambao wote waliondoka msimu mmoja.

muondoe ronaldo basi angalau msajili frank ribery
ni sawa unamuondoa tevez kwa dhumuni la kumpa nafasi zaidi dimitar berbatov ili athibitishe thamani yake, lakini chief klabu ilishampoteza mwanadamu mwenye uwezo wa kukupa goli 50 kwa msimu hivyo basi si vibaya kama klabu ingelikamilisha usajili wa tevez japokuwa usajili wake ulikuwa na matatizo.

tukumbuke tevez alipokwenda man city ndiye aliyekuwa mfungaji bora.

unaizungumziaje ishu ya luka modric?
unaizungumziaje ishu ya roberto lewandowski?
how about wesley sneijder?
juan mata kutoka valencia?
david silva kutoka valencia?
hazard kutoka lille?

tulizipoteza lulu kwa makusudi huku tukiwaachia wapinzani wetu waendelee kujijenga kidogo kidogo kwa hoja dhaifu ya mishahara ya gharama na fedha nyingi za usajili.

yaliopita si ndwele tugange yajayo
 
Hazard alichagua kwenda Chelsea ndiyo man united wakaenda kumsajili Shinji Kagawa. Haya ya woodward ni mwendelezo tu wa incompetence ya Man united kwenye usajili.
upo sahihi brother eden hazard aliichagua chelsea badala ya man utd lakini haiondoi ukweli offer ya chelsea kivyovyote ilikuwa ni kubwa kuliko man utd ndio maana aliichagua chelsea kwa hoja dhaifu ya kwamba chelsea wametoka kushinda UEFA.

Eden Hazard has revealed that he held personal conversations with both Sir Alex Ferguson and Roman Abramovich before deciding that he wanted to join Chelsea rather than Manchester United.

I spoke with Abramovich, he is very simple and loves football,” Hazard said. “We were on the same wavelength, he wants to confirm Chelsea’s position at the top. Chelsea have made a good investment for me but I did not put any pressure on them.”

Chelsea issued a statement to confirm that they had agreed a fee with Lille and personal terms with Hazard, which are expected to be as much £170,000 a week over a five-year contract.

mkuu umeuona utofauti hapo juu katika bold?
abramovich anapenda soka kuliko fergie?
 
kuna video fulani niliiangalia zamani kidogo inamuhusu jose mourinho tokea akiwa ndie kocha wa manutd msimu wake wa pili, ilikuwa ni siku mbili baada ya kufungwa na sevilla kupitia michuano ya champions league, jose mourinho alitumia takribani dakika 12 kuizungumzia hali halisi iliopo ndani ya klabu ya manchester united kwa takribani miaka 8 pamoja na timu nyenginezo.

jose alisema ya kwamba ni sahihi kulaumiwa kwa sababu ya matokeo mabovu dhidi ya sevilla lakini kufungwa kwetu na timu ya sevilla si jambo la ajabu kwa sasa kwa sababu man utd imeshakosa football heritage, hivyo basi inahitajika mipango madhubuti yenye kuambatana na muda wa kutosha kuijenga upya manchester united ili irudi tena katika ubora wake.

mara ya mwisho kwa man utd kucheza fainali ya champions league ilikuwa ni msimu wa 2010/2011 chini ya sir alex ferguson, kiupande wangu nathubutu kusema ndio fainali iliokuwa nyepesi zaidi kumtambua bingwa kabla ya mechi kuchezwa kwa kulinganisha ubora wa vikosi vya timu mbili hizo, msimu huo mchezaji bora wa ligi pamoja na klabu yetu alikuwa ni nemanja vidic.

Licha ya kubeba ubingwa wa ligi kuu msimu huo kwa tofauti ya alama 9 dhidi ya chelsea na manchester city lakini kiwango chetu cha jumla kilikuwa ni cha kawaida sana na ndio maana haikuwa ajabu kutoa suluhu mechi 11 japokuwa tulifanikiwa kukusanya alama 80 pungufu ya alama 2 tulizokusanya msimu wa 2017/2018, ukimuangalia jirani yetu imewachukua miaka miwili tu kuweza kujenga timu ambayo iliweza kujiingiza kwenye kinyang'anyiro cha kuchukua ubingwa (man city walishaonyesha dalili za kuwa tishio ila bahati mbaya mashetani wekundu wakaendelea kulala).,

mwaka mmoja baadae (msimu wa 2011/2012) man united tulipangwa kundi moja na timu nyepesi za basel, benfica, galati kutoka romania kwenye michuano ya UEFA, cha ajabu makamo bingwa alitolewa hatua ya makundi. Hatukuishia hapo tu pia tulitolewa kwenye hatua ya mtoano wa league ya europe dhidi ya athletic bilbao ya marcelo bilesa kwa magoli 5-2, msimu huo athletic bilbao walishika nafasi ya 10 kwenye ligi ya hispania. Miaka minne baada ya city kununuliwa na matajiri wa kiarabu hatimaye msimu huo walifanikiwa kubeba ubingwa kwa tofauti ya magoli dhidi ya man utd.

msimu wa 2012/2013 man utd tunafanikiwa kubeba ubingwa kwa utofauti wa alama 11 dhidi ya man city huku ukiwa ni msimu wa tano tokea man city inunuliwe na matajiri wa kiarabu kama nitakuwa nipo sahihi, ndani ya miaka mitano man city walizidi kujenga emperor yao na kuwa dominance kwenye top 3 ya ligi kuu, hatukuishia hapo tu pia msimu huo tulitolewa hatua ya 16 bora kwenye michuano ya ligi ya mabingwa dhidi ya real madrid ya jose mourinho. hatimaye sir alex akastaafu kufundisha soka.

ina maana miaka mitatu ya mwisho ya sir alex ferguson ilionyesha muelekeo wa timu kupanda juu (2010/2011), kushuka chini zaidi (2011/2012) baadae ikapanda kidogo (2012/2013),

huu ndio usajili alioufanya sir alex ferguson miaka mitano ya mwisho.
chris smalling = amefeli kuwa mrithi wa ferdinand tokea nyakati za fergie mwenyewe mpaka leo
phil jones = amefeli kuwa mrithi wa vidic tokea nyakati za fergie mwenyewe mpaka leo
alexander buttner = amefeli kuwa mrithi wa patrice evra tokea nyakati za fergie mwenyewe na leo hatujui yuko wapi
ashley young = alicheza vizuri mechi za mwanzo ikiwemo ile ya ushindi wa magoli 8 dhidi ya arsenal, baada ya hapo alipata majeruhi na hakuonyesha tena uwezo wake tuliouzoea tokea akiwa wattford na aston villa iliokuwa ikifundishwa na martin oneill, kutoka kuwa winga machachari hadi kuwa mlinzi wa pembeni
chicharito = alicheza vizuri sana lakini baadae akapoteza nafasi walipokuja walimu wengineo ambao hawakuvutiwa na uchezaji wake
robin van persie = ulikuwa ni usajili wa muda kutokana na umri wake kuwa mkubwa.
shinji kagawa = alishindwa kufikia matarajio ya klabu ndani ya uwanja.
bebe = sijui yuko wapi huyu bwege.
antonio valencia: alisajiliwa kwa dhumuni la kuziba nafasi ya ronaldo yule aliyeondoka manchester akiweka rekodi ya kufunga magoli 40 kwa msimu mmoja, kituko usajili huu haukuwahi kutupa hata magoli 5 kwa msimu mmoja, miaka yake 10 amefunga magoli 17 tu, Baadae aligeuzwa kuwa mlinzi wa pembeni.
gabriel obertan = sijui hata aliishia wapi huyu dogo.
michael owen = mfugaji farasi mwenziwe aliamua kumsitiri
david degea = huu ndio usajili pekee wa fergie unaoendelea kutupa faida ile tulioitegemea tokea kusajiliwa kwake.

kwa mtazamo wangu hawa ndio wachezaji ambao walishaanza kuonyesha dalili za kuchoka kisoka miaka mitatu ya mwisho ya utawala wa sir alex ferguson na bahati mbaya kama nilivyosema hapo juu walishindwa kupatikana warithi sahihi wa nafasi zao tokea fergie akiwa madarakani.
ji sung park
rio ferdinand
nemanja vidic
ryan giggs
darren fletcher
patrice evra
paul scholes: (alistaafu akarudishwa kana kwamba timu haina pesa)
darren gibson
tom cleverley
anderson: (kiwango chake ilikuwa ni sawa na maji kupwa na maji kujaa)
luis nani: hakuwahi kucheza vizuri mechi 10 mfululizo.

anguko letu lilianzia hapa
Luis Nani alikuwa akisumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara lakin ktk usajili wa kipaji pale united huyu bwana mdogo alikuwa vizur sir alex hakukosea kiasi kwamba akirud kutoka majeruh fom yake inapotea ila alikuwa akikaa sawa ni hatar sana

Sir alex alitoa boko kwa bebe,valencia, owen na veron
 
Ukweli ni kwamba kulegalega kwenye usajili Man united ilianza zamani tu mathalani usajili wa Wesley Sneider, na Luca Modric ulikuwa uzembe wa mabosi wa united.

Hazard alichagua kwenda Chelsea ndiyo man united wakaenda kumsajili Shinji Kagawa. Haya ya woodward ni mwendelezo tu wa incompetence ya Man united kwenye usajili.
Sababu ninayojua kuachwa kwa hazard ni kagawa upatikanaji wake

Msome babu yako alivyocheza kamar


What Sir Alex Ferguson said about Eden Hazard when Manchester United missed out on signing him in 2012

Chelsea landed Hazard from Lille back in 2012, beating Manchester United, City and Real Madrid to the forward's signature.

United were very keen on signing him at the time, and even made an offer for his services, but the Red Devils were not prepared to pay the transfer fee Lille quoted.
Speaking about the Hazard transfer, shortly after it had been completed back in 2012, Ferguson said: "There is a borderline in terms of what you would think is a good signing for United.

"I see some values on players, like Hazard for instance. To me it was a lot of money. He's a good player, but £34 million?
"What we're finding anyway, the climate for buying these top players - not just the transfer fees, the salaries, agents' fees - is just getting ridiculous now.

"In the Hazard deal, Chelsea paid the agent £6 million. The [Samir] Nasri situation was the same."
He continued: "It's all about what you think is value for a player. I am not envious of those deals at all. We placed a value on Hazard which was well below what they were talking about.
"So if it doesn't work, well we're not worried about that. We think we've got good value in [Shinji] Kagawa."
By today's market £34million is a drop in the ocean


Pia sababu hiyo alimuacha Lucas Moura
 
Hii weekend mpo na amani sana kwavile EPL hamna ,kuleni utawala maan weekend zijazo hamtokaa kwa aman tena
Kabla ya 2017 hayo ndo yalikuwa maisha ya liverpool naona hutu tu miaka tuwili mmepozwa na ka champions league basi nanyie mnaona mmetusua maisha wakat naona miaka miwili mbele mnarudi kwenye tabu tena
 
The class 92 makinda chini ya Ferguson pengine ndio kikosi bora na maarufu cha vijana kuwahi kutokea katika soka la kiingereza.

Leo sidhani kama Sir Alex Ferguson angefanikiwa, leo timu zinatoa pesa nyingi katika vikosi vyao.

Hauwezi kuwa na Mason Greenwood wakati watu wengine wana KUN AGUERO, KEVIN DE BRUYNE, PEIRE AUBAMEYANG, HARRY KANE na Wengineo

Haiwezi kutamba na kina Greenwood katika dunia ambayo timu zinamilikiwa na pesa za warusi na waarabu. Ndicho ambacho Wenger alichemsha.

Chanzo. Mwanasport gazeti
Harry kane ni mchezaj mbovu sana sema hao wengine ni shida tunatakiwa kupata playres kama hao kariba ya kun aguero au aubameyang hao best player ktk ligi ila sio harry kane
 
Back
Top Bottom