Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kumbuka pia wachezaji hao wakati wanasajiliwa Liverpool walikuwa na viwango vya juu.

Sakho alikuwa alipitwa timu ya taifa ya ufaransa.

Lovren ni regular starter wa national team yake mpaka leo

Iago Aspas alikuwa ni mchezaji kama wanne hivi kufunga goal nyingi laliga.

Lalana na Lambert walikuwa wakiitwa national team ya England na waliifiksha Southmpton nafasi ya 8 kwenye ligi ikiwa imepanda daraja tu.

Fabio Bolini nae alikuwa mchezaji kinda aliyefanya vizuri serie A

Laza Marckovic alikuwa mchezaji bora kwenye ligi ya ureno wakati anakuja Liverpool
Wewe unapata wapi ujasiri wa kuwaita magarasa?

Basi usiwalalamikie Rashford na Lingard nao Waliitwa Timu ya Taifa ni Mabonge ya Machezaji
 
Kweli ndo man united yetu ilipofikia..
IMG_20191007_175459.jpeg
 
Big Sam: Manchester United wasipojitazama wanashuka daraja

Staa wa zamani wa Man United, Lee Sharpe anaamini Harry Kane atakwenda kuwa suluhisho la matatizo ya Man United, hivyo wakamsajili tu bila ya kujali kwamba atawagharimu karibu Pauni 300 milioni huko.

. UNAMJUA Sam Allardyce? Yule kocha mwili jumba, Waingereza wenzake wanamwita Big Sam, hakutaka kuwaficha Manchester United na kuwaeleza ukweli, watashika daraja kama hawatafanya haraka kusajili mshambuliaji wa kuja kuwafungia mabao.

Man United wapo pointi mbili tu juu ya kuangukia kwenye shimo la kushuka daraja baada ya kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa kwa Newcastle United.



Wababe hao wa Old Trafford wamefunga mabao tisa tu msimu huu, manne waliyapata kwenye mechi yao ya kwanza dhidi ya Chelsea, lakini sasa straika aliyeaminiwa, Marcus Rashford amekuwa hovyo, hajui hata goli lilipo.

Big Sam, ambaye amepata umaarufu kwamba wa mtu anayefuatwa kuokoa jahazi timu inapokuwa kwenye hali ya kushuka daraja, anasema kwamba kocha Ole Gunnar Solskjaer anatakiwa kutafuta suluhisho la haraka, la sivyo mambo yatamchachia.



"Hili jambo halipo nje ya uwanja wake na kwamba wapo kwenye hali hiyo kutokana na kusumbuliwa na majeruhi wengi. Wachezaji wanaonekana kushindwa kuwa fiti kwa wakati na hilo ndio tatizo," alisema Big Sam na kuongeza.

"Kuna usumbufu pia wa huyu (Paul) Pogba kutaka kuondoka. Nadhani hakuchagua njia nzuri ya kuliwasilisha hilo na si kusema, nataka kuondoka. Shida yao kubwa Man United haipati mabao, wakimaliza hilo, wamemaliza kazi."

Staa wa zamani wa Man United, Lee Sharpe anaamini Harry Kane atakwenda kuwa suluhisho la matatizo ya Man United, hivyo wakamsajili tu bila ya kujali kwamba atawagharimu karibu Pauni 300 milioni huko.
 
Solskjær's job at #mufc is safe even if the club suffer a bad defeat to Liverpool. The board are determined to be patient with him, acknowledging the scale of the role he has taken on #mulive [times]
 
Hizi update unatuletea hapa ili iweje maana kwenye uzi wenu wa Arsenal huzipeleki ?
Breaking | Lyon President Aulas confirms in a telephone press conference this morning that José Mourinho turned down the vacant managerial role because he's about to take a new job elsewhere.
 
Wachezaji 9???
Wakati mwengine munamlaumu tu Ed lakini Hakuna timu inayoweza Kumsajili wachezaji 9 kwa dirisha 1 tena wote wa kikosi cha kwanza.

Wawili tu wa kikosi cha kwanza Maguire na Bissaka wamecost more than £130m+ , Sasa hao 9 Mkuu si wangefika £1B.

Hapo angeliishia kusajili 4 wa kikosi cha kwanza na 5 magarasa ikisha mukaishia kumtukana kuwa kaleta Wachezaji wabovu.
Tatizo ni kuretain wachezaji wengi takataka.

Imagine una wachezaji kama Young. Jones. Lingard. Smalling kwa misimu kama 9 hivi.

Ingekuwa hawa wanaondolewa tungeshakuwa kwenye nafasi ya kufanya sajili hata mbili au tatu za uhakika.

Unataka wachezaji 9 kwasababu wote ni uozo.
 
Back
Top Bottom