Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ss imagine ndo angekua kwny hii team.. Si ndo wakina Sanchez au Di Maria?
Kwa hali ya Timu yetu Sasa Hivi bila wasiwasi nakubali di Maria na kiwango chake Cha era ya LVG na assist zake. Na ole mwenyewe anamhusudu Dybala hivyo pengine alikuwa na plan zake tofauti na kina Sanchez na Di Maria ambao walinunuliwa na Woodward.
 
IMG_6415.JPG
 
KWA TAARIFA YENU:- OLE hatimuliwi makubaliano ni kwamba dirisha dogo january anasajili mastriker 2 na winga 1 na ahakikishe timu inamaliza top 4.
Mpaka timu ifike January hakuna sehemu hii timu itakuwa.

Hata akipewa wachezaji wote wazuri anaowataka, top 6 hana uwezo wa kuingia.

Itamaanisha ashinde mechi zote zilizobaki kitu ambacho hakiwezi na hata kaa aweze.
 
JANUARY

- Kane
- Mbappe
- Bruno
Hakuna mchezaji ananunulika hapa.

Hao wote hawanunuliwi.

Mtaletewa takataka za kingereza kina Longstaff kama mlivyoletewa kina Maguire, Bissaka na James. Ataendelea kuwapanga kina Rashford wake.

Hata akipewa timu nzima ya PSG au Juventus au Barca, tactis zake ni za hovyo, hakuna sehemu zitampeleka.
 
Dybala ilikuaje?..hakuna mtu anaweza acha champions league kuja kwny club ambayo inacheza Europa.,, achilia mbl kucheza Europa yan m2 kuja kwny club ambayo haina muelekeo ni kazi ngm sna asa awa vjn wa saiv ambao weng hawana uvumilivu wa kusbr kujenga team
Ataenda kuokota takataka za kingereza kina Longstaff ndo wenye ndoto za kucheza United.
 
AMECHOKA

KUMBE hata Ole Gunnar Solskjaer anachoshwa na kikosi chake cha Manchester United. Kocha huyo raia wa Norway amekiri kuangushwa na safu yake ya ushambuliaji ambayo inaongozwa na Marcus Rashford.


Solskjaer alidai kuwa wakati mwingine eneo la ushambuliaji limekuwa likishindwa kutimiza majukumu yake ya kufunga mabao licha ya nafasi nyingi kutengenezwa.


Hata hivyo, alisema kuna uwezekano mkubwa timu hiyo ikashusha straika mwingine mpya ili kuwaongezea nguvu akina Rashford, Anthony Martial na kinda Mason Greenwood.


Mapema msimu huu, mabingwa hao wa zamani wa England walimuuza straika wao Romelu Lukaku kwenda Inter Milan kwa kitita cha pauni milioni 73, pia, walimtoa kwa mkopo Alexis Sanchez kwa wababe hao wa Italia.


Solskjaer hakusajili mchezaji yeyote katika safu ya ushambuliaji zaidi ya kuongeza nguvu kwenye eneo la ulinzi na kiungo kwa kunasa saini za Harry Maguire, Aaron Wan-Bissaka na Daniel James.


Tetesi za usajili barani Ulaya zinaihusisha timu hiyo na kutaka kusajili straika mmoja kati ya Mario Mandzukic wa Juventus na Callum Wilson wa Bournemouth.


“Ni kweli, tuliwaruhusu Sanchez na Lukaku kuondoka, wala hauhitaji mtaalamu wa sayansi kujua kama tutafanya usajili katika eneo la ushambuliaji, tutajaribu kufanya hivyo.


“Ulikuwa muda wa Lukaku kuondoka hapa, hata yeye alijua hilo, jambo muhimu ni kuziba nafasi hiyo kwa kusajili mchezaji sahihi ambaye atakuwa hapa kwa muda mrefu.


“Sokoni kuna wachezaji wengi, tunahitaji straika mwenye uwezo, atakayeendana na falsafa za Manchester United, lazima tuzingatie hilo,” alisema.


Kocha huyo aliendelea kuitoa kasoro safu yake ya ushambuliaji kwa kusema wanachangia kwa kiasi kikubwa kuirudisha klabu hiyo nyuma kwa kushindwa kutimiza majukumu yao ya kufunga.


“Unaweza kujionea mwenyewe, eneo pekee ambalo lina shida ni ushambuliaji, safu ya ulinzi tupo vizuri, sisi ni moja ya timu tulizofungwa mabao machache England.


“Hakuna utulivu kwenye ushambuliaji, hakuna anayeweza kufanya maamuzi sahihi, tunahitaji muda kulifanyia kazi hilo, najua tutakaa sawa baadaye,” alidokeza Solskjaer.


Katika michezo saba ya Ligi Kuu England, safu ya ushambuliaji ya Manchester United wamefanikiwa kufunga mabao nane.​
Akili za Championship.

Huyo striker wa Bournemouth amefunga magoli mangapi?
 
According to stone (Mwandishi wa habari wa BBC na mtu wa karibu wa Ed Woodward), Ole amemuambia Ed Woodward anahitaji wachezaji 9 Ili Man UTD ikae vizuri, na maneno haYa Ed ameambiwa kabla Dirisha la usajili halijafunguliwa.

Mkuu tuna matatizo makubwa as a club, Structure nzima ipo ovyo, huo usajili si tatizo Sana Kushinda issue ya Majeruhi, Nasikia Dogo Greenwood na yeye ameumia, kila mchezaji akija tu Man United anakuwa injury prone, mpaka AWB Sasa nae amekuwa hivyo hivyo, dalot karudi mechi 1 tayari nae Majeruhi, martial tuliambiwa kaumia kidogo mwezi wa Pili unaisha, pogba, lindelof, lingard, Shaw etc kila unapogusa Ni Majeruhi tu, issue hii IPO toka Fergie aondoke man U 2013 na Mpaka Leo haijatatuliwa.

Nyepesi nyepesi nyengine Ni kwamba Ed anamtoa kwa mkopo Matt judge akapate uzoefu zaidi, timu Kama Man U ndio kichwa chetu hicho tunakitegemea kusajili watu.
Ole ange resign, asisubiri afukuzwe.
 
Chief kuna kitu kimoja unakosea... klopp imemchukua misimu mitano kujenga Liverpool ndo maana unaona mafanikio yao leo.. so ole aachwe apewe muda ajenge TEAM afumuee kila kitu then tuone matunda... hata kocha wa spurs kuingia final UCL sio jambo dogo.. took them 7 years.
Hata akipewa karne nzima. Sajili zake zinatia aibu.
 
Back
Top Bottom